Betting ni mchezo unaoweza kukuletea umasikini hata kukuua!

Betting ni mchezo unaoweza kukuletea umasikini hata kukuua!

Ben-adam

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2023
Posts
1,043
Reaction score
2,309
Sidhani kama kuna mtu anabeti/alibeti kunishinda mimi!

Betting ina addiction ile mbaya, ikikukumba siyo rahisi kuacha.

Hongera nyingi kwa aliegundua hii michezo, alitumia akili kwelikweli! Nimetumia kila mbinu, kila hesabu ninazozijua lakini kipigo kiko palepale.

Pia niwape pole wale mnaoamini kwamba ipo siku watatusua kwenye Betting, mnajidanganya, mtaambulia hasara kiuchumi na kiafya. Namuona mtu mmoja anataka kusema ati "beti kwa starehe tu" "bet what you can afford to lose" pole sana.

Kadri unavyopoteza ndivyo unavyozidi kupambana ili uokoe ulichopoteza, aidha kwa kuongeza dau au odds. Wazee wa hizo kazi wananielewa. Kwasasa accounts zangu zote za kubetia nimeshazifunga japo kuna wakati nashawishika sana kufungua account mpya (addiction hiyo)najizuia.

Baadhi ya vitu vilivyofanya niamue kuachana na betting;

Nilikuwa napoteza muda mwingi hata wa kazi kutengeneza mkeka (uchambuzi)

Maumivu makali ya kihisia baada ya timu moja kunichania mkeka niliotumia muda mwingi kuutengeneza, (na hiyo timu iliyochana italaaniwa sana sana😮‍💨)

Niliona kabisa hapa nikiendelea hivi, presha na kisukari vile palee. Hakuna wakati mgumu kama pale timu uliyoipa ushindi inafikia dakika ya 70'au 80' ubao unasoma 0-0, mapigo ya moyo yanaenda mbio, umekaa tu cha ajabu unatokwa jasho kama vile unapanda mlima.

Ilifika hatua nikawa napumzika kwa muda mchache sana, muda wa kulala mimi niko live, siyo kwamba nachati wala nini, ni nabetika.

Hata ukinitumia ujumbe WhatsApp usitegemee kujibiwa, ukipiga simu kama sio mtu ambae namheshimu sana jibu ni moja tu "nitakupigia badae kidogo, nipe dakika tano" mpaka pale tukio ninalofuatilia litakapokamilika (tabia mbovu sana hii)

Leo nimemsikia mtu anasema anatafuta mtaji aanze kubeti😆😆 Kama hujawahi kubeti, wala usitake kujifunza.

Kweli betting ni haramu ni heri uraibu mwingine wowote ila sio betting/kamari, betting ni mufilisi janjaruka mapema.

Soma Pia: Vijana tuacheni kubeti, kindege (aviator) kimenimaliza milioni 7 yote ya mtaji
 
Kila la heri
Sidhani kama kuna mtu anabeti/alibeti kunishinda mimi!

Betting ina addiction ile mbaya, ikikukumba siyo rahisi kucomoka!

Hongera nyingi kwa aliegundua hii michezo, alitumia akili kwelikweli! Nimetumia kila mbinu, kila hesabu ninazozijua lakini kipigo kiko palepale!

Pia niwape pole wale mnaoamini kwamba ipo siku watatusua kwenye Betting, mnajidanganya, mtaambulia hasara kiuchumi na kiafya!


Namuona mtu mmoja anataka kusema ati "beti kwa starehe tu" "bet what you can afford to lose" pole sana.


Kadri unavyopoteza ndivyo unavyozidi kupambana ili uokoe ulichopoteza, aidha kwa kuongeza dau au odds. Wazee wa hizo kazi wananielewa


Kwasasa accounts zangu zote za kubetia nimeshazifunga japo kuna wakati nashawishika sana kufungua account mpya (addiction hiyo)najizuia.


Baadhi ya vitu vilivyofanya niamue kuachana na betting;


-Nilikuwa napoteza muda mwingi (hata wa kazi) kutengeneza mkeka (uchambuzi)

-Maumivu makali ya kihisia baada ya timu moja kunichania mkeka niliotumia muda mwingi kuutengeneza, (na hiyo timu iliyochana italaaniwa sana sana😮‍💨)


-Niliona kabisa hapa nikiendelea hivi, presha na kisukari vile palee!

Hakuna wakati mgumu kama pale timu uliyoipa ushindi inafikia dakika ya 70',80' ubao unasoma 0-0, mapigo ya moyo yanaenda mbio, umekaa tu cha ajabu unatokwa jasho kama vile unapanda mlima!!



-Ilifika hatua nikawa napumzika kwa muda mchache sana, muda wa kulala mimi niko live, siyo kwamba nachati wala nini, ni nabetika!

Hata ukinitumia ujumbe WhatsApp usitegemee kujibiwa, ukipiga simu kama sio mtu ambae namheshimu sana jibu ni moja tu "nitakupigia badae kidogo, nipe dakika tano" mpaka pale tukio ninalofuatilia litakapokamilika (tabia mbovu sana hii)

Leo nimemsikia mtu anasema anatafuta mtaji aanze kubeti😆😆
Kama hujawahi kubeti, wala usitake kujifunza.

Kweli betting ni haramu ni heri uraibu mwingine wowote ila sio betting/kamari, betting ni mufilisi janjaruka mapema.
 
Pia niwape pole wale mnaoamini kwamba ipo siku watatusua kwenye Betting, mnajidanganya, mtaambulia hasara kiuchumi na kiafya!
Sio lazima kutusua, ila walau ya supu haikosekani. Hapa nipo ninaweka mzigo mdogo mdogo katika Virtual ya BetPawa, nilianza na sh. 4000 ila hata saa moja haijaisha nishapata 20 na nadhani kwa leo inatosha

1722699641976.png
 
Ila shetani ana ushawishi sana nilipoamua kuacha kubeti mikeka yangu ya mwisho nlikula yote...ila nikaamua kwa dhati kuachana nayo.

Wakamaria wapo hatarini kupata magonjwa ya shinikizo la damu,msongo wa mawazo,kisukari na hata kujiua.

Simshauri mtu kujifunza kubeti ni uraibu mbaya sana. Yaani inafika kipindi huwezi kupata usingizi usiku. Unabeti kuanzia ligi za america kusini na kaskazini Usiku mpk alfajiri. Ukimaliza unaamia ligi za Australia, newzealand na japan asubuhi, ukimaliza upo ligi za india,nepal,iran mchana..jioni unaamia za uarabuni,usiku upo ulaya.

Kamari inaharibu mahusiano yako ya kifamilia na kijamii,kiuchumi,kiiamani n.k
 
Ila shetani ana ushawishi sana nilipoamua kuacha kubeti mikeka yangu ya mwisho nlikula yote...ila nikaamua kwa dhati kuachana nayo.

Wakamaria wapo hatarini kupata magonjwa ya shinikizo la damu,msongo wa mawazo,kisukari na hata kujiua.

Simshauri mtu kujifunza kubeti ni uraibu mbaya sana. Yaani inafika kipindi huwezi kupata usingizi usiku. Unabeti kuanzia ligi za america kusini na kaskazini Usiku mpk alfajiri. Ukimaliza unaamia ligi za Australia, newzealand na japan asubuhi, ukimaliza upo ligi za india,nepal,iran mchana..jioni unaamia za uarabuni,usiku upo ulaya.

Kamari inaharibu mahusiano yako ya kifamilia na kijamii,kiuchumi,kiiamani n.k
 
Back
Top Bottom