Biashara kutoka China

Biashara kutoka China

Gurder

New Member
Joined
Apr 13, 2014
Posts
3
Reaction score
0
Ndugu zangu naomba yeyote mwenye uzoefu na bidhaa za stationary kutoka China anijuze, nina millioni kumi, na kuna mtu kaniambia naweza fanya hiyo biashara na nikapata faida kubwa zaidi.Nimeshapata stationary kumi, ambazo ni kubwa na wanahitaji niwe nawazambazia vitu kama madaftari,penseli na kalamu
 
Ndugu zangu naomba yeyote mwenye uzoefu na bidhaa za starionary kutoka china anijuze, nina millioni kumi, na kuna mtu kaniambia naweza fanya hiyo biashara na nikapata faida kubwa zaidi.Nimeshapata stationary kumi, ambazo ni kubwa na wanahitaji niwe nawazambazia vitu kama madaftari,penseli na kalamu

biashara ya ki 'mbebez' hiyo!!..waachie mbebez waifanye!!..miafrika kwa uvivu siiwezi mweh!!..ndo tatizo la kunywa ''kibuku' asubuhi.
 
kwann umjibu hivyo? sio busara..jaribu kutoa wazo lako,hata kama hujui either ni mkweli au laa..lakini ww itakujenga kuwa na hekima katk mawazo yako..jitahidi ka..
Mi ninachoweza kukushauri mkubwa hapo juu..fanya kutafuta investiment ndogondogo hata tatu kwa mtaji wako,ili hata kama ikitokea bahati mbaya unakuwa na namna yakumudu..na nivema ukaanza chini ukawa unaenda juu..au hatakama unawazo la china nenda na aspect mbili..but in reality mtaji mdogo kwa ww kwenda china..
Nihayo..labda wengne.
 
Ndugu zangu naomba yeyote mwenye uzoefu na bidhaa za starionary kutoka china anijuze, nina millioni kumi, na kuna mtu kaniambia naweza fanya hiyo biashara na nikapata faida kubwa zaidi.Nimeshapata stationary kumi, ambazo ni kubwa na wanahitaji niwe nawazambazia vitu kama madaftari,penseli na kalamu

Salaam,
Kwanza, nimekuwa na uzoefu kwa muda juu ya biashara za China na Japan. Kwa mtaji wa 10mil ni kama nusu ya mtaji wa kuanzia kwa sababu kuna mambo matatu hapo. 1. Usafiri na malazi, 2. Ununuzi wa bidhaa na uhifadhi, 3. Upakiaji na Usafirishaji.

Biashara uliyopanga kuifanya naamini umeshafanya utafiti na kugundua ni nini kinachotakiwa. Unachopaswa kufanya kwa kuanza (kulingana na mtaji wako) tafuta wakala (online au wenye ofisi Tanzania) uweke order kulingana na mahitaji yako kisha mzigo ukifika unaanza kazi ya ku supply kwa hao wateja wako.

Ukifanya hivyo Mara nne au mara tano tayari utakuwa na uwezo wa kwenda mwenyewe na kujionea fursa zaidi za biashara nchini China. Sambamba na hilo nakushauri usiwekeze pesa yote kwenye mtaji wakati wa kuanza biashara hiyo kwa ajili ya dharura za kibiashara na wateja wako.
 
Salaam,
Kwanza, nimekuwa na uzoefu kwa muda juu ya biashara za China na Japan. Kwa mtaji wa 10mil ni kama nusu ya mtaji wa kuanzia kwa sababu kuna mambo matatu hapo. 1. Usafiri na malazi, 2. Ununuzi wa bidhaa na uhifadhi, 3. Upakiaji na Usafirishaji.

Biashara uliyopanga kuifanya naamini umeshafanya utafiti na kugundua ni nini kinachotakiwa. Unachopaswa kufanya kwa kuanza (kulingana na mtaji wako) tafuta wakala (online au wenye ofisi Tanzania) uweke order kulingana na mahitaji yako kisha mzigo ukifika unaanza kazi ya ku supply kwa hao wateja wako.

Ukifanya hivyo Mara nne au mara tano tayari utakuwa na uwezo wa kwenda mwenyewe na kujionea fursa zaidi za biashara nchini China. Sambamba na hilo nakushauri usiwekeze pesa yote kwenye mtaji wakati wa kuanza biashara hiyo kwa ajili ya dharura za kibiashara na wateja wako.

hapo kwenye red ndiyo kazi ipo, labda utusaidie orodha ya mawakala waaminifu ambao wewe ulishawahi kufanya nao kazi.
 
hapo kwenye red ndiyo kazi ipo, labda utusaidie orodha ya mawakala waaminifu ambao wewe ulishawahi kufanya nao kazi.

Mkuu
Wapo kina Alibaba, hata hivyo kuna kampuni za wazawa ambazo zinafanya kazi hiyo au pamoja na kazi nyingine. Yeyote akikwahitaji anijulishe tu.
 
Kama upo serious tutafutane ,nakupm namba yangu
 
biashara ya ki 'mbebez' hiyo!!..waachie mbebez waifanye!!..miafrika kwa uvivu siiwezi mweh!!..ndo tatizo la kunywa ''kibuku' asubuhi.

Hizi ni akili za watu wasio na vision Kabisa maishani!
pole sana sikuwahi kufikiri Kama una fikira mkia wa mbuzi na umekosa busara kiasi hiki!
 
biashara ya ki 'mbebez' hiyo!!..waachie mbebez waifanye!!..miafrika kwa uvivu siiwezi mweh!!..ndo tatizo la kunywa ''kibuku' asubuhi.

Ebwana huyu jamaa yeye kila mtu akija na idea yake yeye anajifanya mjuaji na kutukana alafu hana mawazo mbadala na kusema waafrika kama yeye yako number one ktk matajiri ulaya.
Anamatizo sana anatabia za kujikweza na kuzalau wengine
 
nitakutafuta mkuu kwani hao mawakala wengi wamekuwa matapeli ndo maana tunasita kufanya nao biashara
Mkuu
Wapo kina Alibaba, hata hivyo kuna kampuni za wazawa ambazo zinafanya kazi hiyo au pamoja na kazi nyingine. Yeyote akikwahitaji anijulishe tu.
 
achaneni nae huyo ana matatizo ya kiakili anatakiwa ampate mwanasaikolojia amtibu ufahamu wake
maana yeye anafikiri kila jambo hapa jf ni la kimzaa kwani haoni majukwaa yaliyokweka mahsusi wa mijokes
Hizi ni akili za watu wasio na vision Kabisa maishani!
pole sana sikuwahi kufikiri Kama una fikira mkia wa mbuzi na umekosa busara kiasi hiki!
 
nitakutafuta mkuu kwani hao mawakala wengi wamekuwa matapeli ndo maana tunasita kufanya nao biashara

Kinachokosewa Mara nyingi kwa wanaoagiza mizigo ni kukubali kuingia mikataba myepesi na mawakala nao mawakala wasio waaminifu hutumia mianya hiyo kuwaibia wateja wao.

Inatakiwa ukishatoa order kwa wakala akupe Invoice na mkataba kabisa as if yeye ndiye anayekuuzia bidhaa hizo. Hii ipo kwa mujibu wa sheria za biashara kwamba wakala yeyote ndiye risk taker kwa 100% kwa kutegemea bima zao za biashara.

Kila la heri.
 
Mkuu
Wapo kina Alibaba, hata hivyo kuna kampuni za wazawa ambazo zinafanya kazi hiyo au pamoja na kazi nyingine. Yeyote akikwahitaji anijulishe tu.

huko alibaba si ndiyo kumejaa madalali na wasanii mkuu? kusema kweli biashara ya china ni muhimu sana kwenda mwenyewe kuexplore na kujitengenezea network.
 
huko alibaba si ndiyo kumejaa madalali na wasanii mkuu? kusema kweli biashara ya china ni muhimu sana kwenda mwenyewe kuexplore na kujitengenezea network.

Everything is how you make it. Kama ni madalali hata China wapo tena wabaya sana. Mara nyingi watu wamekuwa wakibambikwa bidhaa fake badala ya alizonunua, au pengine kubadilishiwa kabisa aina ya mzigo pale wanapofunga. Huko Alibaba mwanzoni mwa 2011 niliwahi kuagiza mizigo mara mbili nikaipata bila wasiwasi.

Labda kuna namna hao madalali wanawaharibia lakini ukiwasiliana nao direct na kuwa na mkataba nao mizigo yako unaipata kwa uhakika bila wizi wowote.
 
Everything is how you make it. Kama ni madalali hata China wapo tena wabaya sana. Mara nyingi watu wamekuwa wakibambikwa bidhaa fake badala ya alizonunua, au pengine kubadilishiwa kabisa aina ya mzigo pale wanapofunga. Huko Alibaba mwanzoni mwa 2011 niliwahi kuagiza mizigo mara mbili nikaipata bila wasiwasi.

Labda kuna namna hao madalali wanawaharibia lakini ukiwasiliana nao direct na kuwa na mkataba nao mizigo yako unaipata kwa uhakika bila wizi wowote.
Hivi mkuu inachukua muda gani tangu umeagiza mzigo mpaka unaupata? Na vipi kuhusu vifaa vya ujenzi? Hivi watu wanavifuata China, Hong Kong au Dubai?
 
Back
Top Bottom