Biashara tofauti za kuniingizia 50,000/= kwa siku

Biashara tofauti za kuniingizia 50,000/= kwa siku

Ndugu zangu nashukuru kwa michango yenu mizuri ,mm nilikuwa nalenga kupata biashara ambazo naweza kumpa mtu akafanya mm nikiwa napata faida yangu ya kila siku ambapo muda wangu wakwenda kuisimamia ni weekend .Nilitaka angalau nipate biashara tofauti za mtaji wa kawaida ambapo kwa siku faida nayoweza kupata kwa biashara zote angalau kuanzia hamsini.

Nilifikiria nitafute mtu ninaemuamini nimpe mradi wa kuuza juice ya miwa nayeye kila siku ananipa faida yangu ila sijajua mtaji wake kiasi gani.Sasa miradi nyingne yenye mtaji mdogo ambayo mtu atanipa maingizo yangu kila siku bila kusimamiwa sanaaaa .Naomba mjikite hapo kunisaidia ndugu zangu.

Mm huku ni mwajiliwa wa serikali ni mwlm nipo kijijini ,nikafikiria namna ya kuingiza 1,500,000/= kwa mwezi ambapo nikafikiria kupata miradi ya mtaji midogo ambayo hatimae nitaingiza kiasi cha fedha hiyo.
Kiukweli biashara znahitaj sn management, ss naona kwa juhudi zote unajitahd kukimbia kusimamia biashara yako mwnyw... Be care kuna ka haruf ka hasara nakackia usipobadl strategy...
 
Hhahah oya acha basi unawezaje kuweka mpunga wote mbna risk kubwa duh huwa unajitoa ufahamu au
Labda Betting
Mtaji=300,000
Odds=1.5
Kodi=15%

300,000×1.5=450,000

450,000×15÷100=67,500

450,000-67,500=382,500

Faida 82,500

Lakin sio kila siku utabet au utapata kuna kuangukia pua.
 
Asilimia kubwa ya biashara nyingi halali huzalisha faida ya kati ya 17% had 20% kwa mauzo. Faida ya 50,000 kwa siku ni mauzo ya kati ya 250,000 hadi 300,000 kwa makadirio. Kwenye hiyo faida tunatoa hapo gharama za uendeshaji ambazo siyo rafiki sana kwa nchi yetu. Unajikuta gharama za uendeshaji ni nusu ya faida unayopata. Hivyo inakulazimu kuuza walau 500,000 hadi 600,000 ili ulaze 50,000.

Tukija kwenye mauzo hayo, ni mtaji kiasi gani? Hapa itategemea na aina ya biashara na location. Mfano: Biashara ya jiko la chips, chomachoma, chapati za kisasa mix supu inakulazimu uwe na mtaji usiopungua 4 milion.
Umeongea ukweli mchungu sana. Huu ndo msimamo wangu pia
 
Back
Top Bottom