Ndio maana kwenye biashara hatoshi kumuajiri mtu tu, hadi mwenye biashara anatakiwa awe muajiriwa hata wa part time. Usiache biashara luzi kwa kuwa umemuajiri mtu.wengi walioshauri hawakufikiria hili....siku hizi huibiwi hela,wafanyakazi wanaleta vyao wanauza eneo lako ukija unaambiwa biashara ngumu na bidhaa zako unazikuta!!! huu huwakuta sana wenye baa.
Zero what if naamua kusimamia mwenyewe hapo inakuaje? Yani mimi as mmiliki ndo nakua mpokea hela hapo nakaa hadi muda wa kufunga.Huwa napokea PM nyingi sana za wadau wakitaka kujua mchanganuo wa biashara ya chipsi,
Yaani kuanzia vifaa, mtaji wake na Nk.
Kiukweli siwezi kujibu PM ya kila mdau kwa wakati sasa nimeona bora nipaste kile nilichowaambia baadhi ya wale waliotaka kujua hapa ili kila mtu anaehitaji kujua asome hapa,
Mchanganuo wa biashara ya Chipsi ni huu, hapa ni kwa ule mtaji wa kawaida kabisa,
Kwanza kabisa vifaa vyake muhimu
1: ile kabati ya kuhifazia chipsi inatakiwa iwe kubwa kiasi ngazi mbili au tatu itapendeza zaidi hapo kiasi ni 150k-250k
2:majiko mawili moja ya kuivishi chipsi nyingine ya kuchomea chipsi mayai mishikai N. K, hapo kila jiko itakost kuanzia 35k--45 kwa hiyo total pigia tu 90K,
3:vifaa vidogo vidogo kuna karai 10k--15k,sahani Dz 1 au 2 fanya 10K,koleo 3k,flampeni 2 5k, beseni dogo na kichujio chake kwa ndani 10K, vitu vidogo vidogo fanya 15K,
4:uje kwenye mazaga yenyewe.
Viazi gunia inategemeana na eneo ila bei kuanzia 45k--60k,mafuta ya kula ndoo ndogo 30k,mkaa gunia moja inategemeana na eneo ila approximately ni 25k--40k,mayai tray 3 24K
Kwa kifupi kama hauna kifaa ata kimoja unatakiwa usiwe na chini ya 500k, na hapa ni kibanda tu cha kishkaji.
Faida zake,
Chipsi zina faida sana kama ukikaa location inayoeleweka inayoweza kumaliza kuanzia nusu gunia la viazi mpaka gunia moja na uwe na msimamizi imara huwezi kosa kuanzia 25k--45k kwa siku kama faida,
Hapo weka vyuku vyuku mishikaki,juice na N.k faida inakuwa mara dufu
Onyo/NB.
kila biashara ina changamoto zake siwezi kuwa mchoyo wa kushindwa kukwambia haya, hii biashara ya chipsi ukitaka faida Usiwe na masihara ya kucheka na mademu, zingatia kipimo chako usisikie ya mteja anasema nini eti chipsi sishibi sijui chache mwambie aongeze hela umjazie ukileta utani unafunga kibanda.
CC Zero IQ
Vipi mrejeshoHuu mwongozo nimeukubali subir mrejesho tu
Sent from my iPhone using JamiiForums
U mean hata ukikaa hapo hapo wanaweza kukuibia???
Chipsi zinahela mkuu fanya utanjpa mrejeshoZero what if naamua kusimamia mwenyewe hapo inakuaje? Yani mimi as mmiliki ndo nakua mpokea hela hapo nakaa hadi muda wa kufunga.
Chipsi zinahela mkuu fanya utanjpa mrejesho
Kusimamia mwenyewe biashara ndio itakuwa stable kwa sababu kila kitu kitakuwa juu yako,Thanks. Nataka kujua changamoto za kusimamia mwenyewe ni zipi?
Mabeberu siyo watu wazuri!Ndo hapo mkuu, mabeberu sio watu wazuri, wamesha hack account ya Zero IQ huyu sio kabisa
Nimekuelewa. Asante sana.Kusimamia mwenyewe biashara ndio itakuwa stable kwa sababu kila kitu kitakuwa juu yako,
Sema kudumu na wafanyakazi itakuwa mtihani kwa sababu wengi wataona unawazibia mirija yao ya upigaji
Vipi mrejesho
Sijui nisemeje mkuu,
Hahaha dahOfcz...kama umezubaa wanapita na wewe...hasa ninyi wadada mnakuwa busy na smartphone
Kwanini? Imeenda poa sana ama imeenda vibaya
Daaaahhhhhh!!!!! Nashukuru broo kwa msaada wako !!!!
Ngoja nianze kuhangaika... baada ya wiki mbili nitaleta mrejesho hapa MUNGU AKIPENDA
Usinunue deep frier ya dukani ka una mipango ya muda mrefu kwenye hii biashara, Kachonge deep frier kubwa na zenye uimara na uwezo zaidi kwa wale wachonga majiko wa keko gerezani karibu na workshop ya Bakhresa