Biashara ya Day Care na shule za chekechea Arusha zimeshamiri kulikoni?

Biashara ya Day Care na shule za chekechea Arusha zimeshamiri kulikoni?

Maisha magumu sana, sasa hv mzazi unachagua usiende kazini then ukae na mtoto nyumbani au utafute dada amuachie mtoto nyumbani au umpeleke mtoto kwenye vituo vya kulea watoto (day care)
mwisho wa siku unaona ni bora umpeleke kwenye day care mana kule atapata muda mwingi kukaa na wenzake, kufanya michezo yao, kujifunza mambo mbalimbali, kuzoea mazingira ya kuishi na wengine. Hii ni tofauti na kama ukimuacha mtoto na dada wa kazi mana kuna mambo kama mtoto atakosa.
 
Siku hizi wadada wa kazi ni changamoto sana.zamani ilikuwa rahisi kuwapata kwani walikuwa hawaendi wengi sekondari kama sasa hivi.Lakini kwa sasa unakuta darasa zima wanachaguliwa kwenda sekondari mpaka vijijini huko na wanaobaki kidogo hawana wito na hizo kazi.
 
Daycare zimekuwa nyingi sana. Hakuna mtu wa kulea mtoto Mchana na kila mtu yupo bize na kazi na dada wa kazi ni majanga sana. Daycare zipo nyingi Dar,Arusha, Mwanza na Dodoma.
 
wakuu habarini za muda huu. Naomba kujua mwenye uzoefu wa hii biashara ya shule ya chekechea na day care anipe muongozo.

Naombeni kujua ni vigezo gani vinahitajika na mfumo wake wa elimu ukoje maana nimekaa arusha miaka miwili sasa lakini kila kukicha unakuta makaratasi njiani kila mahali ni day care na chekechea.

Je, hizi shule zimesajiliwa? na je zinalipa kodi? nauliza hivi kwakuwa hii biashara imeibuka kwa kasi ya ajabukwakuwa kuna moja nilikuta juzi maeneo ya sanawari wanachukua watoto kwa shilingi elfu kumi kwa mwezi huku wakisambaza vipeperushi na kuwaambia wananchi kwamba watoto watakuwa wanapata chakula bure kwakuwa mfadhili wao ni mzungu hivyo atawahudumia kwa mahitaji yote.

Hoja yangu kubwa ni kutaka kujua hawa wazungu wafadhili wanaosema watatulishia watoto bure Je wao wanapata nini kutoka kwetu?

Je, Serikali yetu inafuatilia kwa karibu hawa wazungu wafadhili wanaokuja kujificha kwenye vituo vya yatima na day care na chekechea kama kweli nia yao ni msaada au kuna biashara nyingine imejificha kwa undani? Na je TRA wanakusanya kodi zao au wanawaacha tu kwakuwa ni msaada?

Pia day care zingine na chekechea zina wafanyakazi wa nje ya nchi kama wazimbabwe, waganda na wakenya sasa vipi kuhusu vibali vya ajira kwa raia wa kigeni Uhamiaji wanawafuatilia watu wote wanaomiliki hizi day care na chekechea? Kwakuwa nyingi zimekuwa kichaka cha kuficha wahamiaji haramu na biashara zingine za ajabu.

Huwezi kusema unawasaidia wazazi wasiojiweza bila kuwa wazi kwamba wewe mfadhili unapata nini kutoka kwenye nchi yetu hii ya tanzania.

Kibaya zaidi wengine wameenda mbali kwa kukodisha nyumba mitaani na kufungua mashule. Nisaidieni kunielewesha kwamba ukitaka kufungua shule ni vigezo gani unatakiwa kuwa navyo na hizo day care ni masharti gani yanahitajika?.

Nawasilisha mada.
Swali lako limeegemea kikuda zaidi kuliko kuiangalia fursa iliyopo.

Demand ya hivyo vituo ni kubwa na kila mzazi anapeleka mtoto pale ana uwezo napo.

Haiingii akili mtoto under 5 years aanze kutafuna mamilioni kwenda day care, hawahawa wa mitaani wa 30,000/= kwa mwezi au 50,000/= wanatosha.
 
Side effects za jiwe kuwaambia fyatueni watoto wengi ndio zinaanza kuonekana sasa hivi.
Watu wamezaa kwelikweli halafu kulea watoto wao wanashindwa,
Wanakuja wafadhili kuwasaidia kulisha watoto wenu badala mshukuru mnataka hao wafadhili walipishwe makodi ya hovyohovyo.
Kweli mbongo ni sawa na gunia la msumari ukilibeba linakuchoma mgongoni.
 
Changamoto za wadada

Badala ya kukuta mtoto anajua miziki mipya kukata viuno na movie zote za kinigeria bora aende day care

Au hawa wadada ambao anaweza fungia mtoto ndani akasepa heri akashinde huko
 
uzungu mwingi
Si kweli tatizo ni wasichana wa kazi hawana uwezo wa kutunza watoto vizuri, hasa kwa parents ambao kuondoka ni asubuhi kurudi ni usiku. Sasa hizi day care ukipata za uhakika ni msaada mkubwa kwa kukaa na watoto, huku wakipata elimu, michezo na kuichanganya na wenzao.
 
Mlevi mmoja alisikika akisema dawa ni Katiba Mpya!
 
Back
Top Bottom