Biashara ya Duka la Rejareja: Ushauri, Mchanganuo, Changamoto na Namna ya Kutunza Kumbukumbu

Biashara ya Duka la Rejareja: Ushauri, Mchanganuo, Changamoto na Namna ya Kutunza Kumbukumbu

Una miumyo mzuri sana
Chumvi kubwa kwa huku 12000
Chumvi ndogo 5000
Ponpon 40000
Freestyle hizi ni ped ndogo nabkubwa 22000
Betri aina zote ndogo na kubwa wakati kubwa huku nilipo ni 110000
Sukari kg 50 ni 105000
Sukar kg 25 ni 54000
Ngano azam bora 25500
Kleesoft sabuni ya unga kg 15 ni 31000
 
Jibu makini
Nashukuru sana. Ila mimi hii biashara ya rejareja nimefanya utafiki kidogo hapa mtaani itanifaa sana maana hakuna duka la rejareja karibu lilopo liko mbali kidogo na service yake sio nzuri na linafungwa mara kwa mara na kuwalazima jamaa kutembea umbali mrefu kufuata huduma. Ni biashara ambayo nina passion nayo mda mrefu na sitauza vitu hivi tu ila nitaweka na gesi, huduma za kutuma na kupeka pesa na vocha za kurusha. Kwa sasa zinapatikana mbali kidogo kama gesi lazima upande boda boda kuifuata. Nadhani ni vizuri nikashauri kuwa nielekezwe na kushauriwa na wanaoifanya hii biashara na ushauri ujikite kwenye hii biashara maana nimeomba kusaidiwa list ya vitu kwenye hii biashara na sijaomba wazo la biashara. Hatua ya wazo la biashara nimeshatoka huko.
 
Pole sana Mungu alikuandikia hapo Na utafika mbali. JF kuna baadhi ya watu mpaka unajiuliza waliwahi kupitia chuo cha kamati ya Roho mbaya?

Yaani MTU anawaza Negative tu sio posive. Halafu unaweza kuta hata Kiosk hajawai uza.
Safi sana mkuu. Tatizo watanzania wengi tunapenda kukatishana tamaa. Kama hapo juu watu wanasema duka la rejareja achana nalo faida ni 10% tu. Hii sio sahihi.

Mimi nilianza na bidhaa za milion 1 laki 3 katikati ya mwaka huu. Nanunua hapo manzese tip top. Day one niliuza elf 26. Mpaka sasa nauza mpaka 160 elf, siku ikiwa mbaya siuzi chini ya 80. Na bidhaa zinazidi kujaa.

Ukitaka kufanikiwa kwenye biashara tafuta site isiyokuwa na sifa za ushirikina na husijihusishe kabisa na ushirikina, fanya mwenyewe usimwajiri mtu au uwe na usimamizi madhubuti, kama unategemea duka lenyewe kuishi punguza sana matumizi, jinyime usipende sana kula kula, fanya kwa malengo, jitahidi sana kuwa mfatiliaji wa mabadiliko ya bei za bidhaa.. Usijenge chuki na wafanyabiashara wenzio.

Mimi najiona mbali siku zijazo kutokana na kiduka changu. Japo nilifukuzwa kazi lakin sijuitii.
 
Mimi ushirikina ulinifanya nifunge duka,nilizungukwa na maduka ya washirikina cha moto nilikiona,Najipanga nitafute sehemu nyingine nifungue tena,Vina faida sana hivi vidude ukipata site nzuri!
Pole sana Mungu alikuandikia hapo Na utafika mbali. JF kuna baadhi ya watu mpaka unajiuliza waliwahi kupitia chuo cha kamati ya Roho mbaya?

Yaani MTU anawaza Negative tu sio posive Halafu unaweza kuta hata Kiosk hajawai uza. VP lakini
Ulikutana na vimbwaga gani?
 
Fact.
Hivi aliyesema ukiuza laki 3 unapata tu Elfu 10 faida nani?
So itategemeana Na wingi wa Biashara Na mzunguko?
Kuna watu wanaweza kukatisha tamaa humu.
We acha tu.
Kamati ya Roho mbaya
Naungana na ninyi mimi,nakumbuka nilianza na Kuuza Mchele tu na Mafuta ya alizeti tu,siku ya kwanza nakumbuka nirudi nyumbani na 15k..iliniuma sana ila nikapiga moyo konde,sema nilianza fanya connection na watu,kuwa makini na mabadiliko ya bei na kuwajenga wateja ,uaminifu.. nashukuru kwa sasa siuzi chini ya 60k..na faida naiona kwa kila week...tuache kukatishana wadau,unachofanya wewe huenda sio passion yangu na nnachofanya mimi huenda wewe sio passion yako
 
Mimi nauza vifuatavyo ambavyo vinatoka haraka;

mafuta ya kula,
sukari,
unga ngano(mara nyingi naisambaza kwa mama ntilie ili iuzike haraka),
sabuni ya kufulia(ya mche na unga),
pipi na jojo,
maharage,
majani chai,
mifuko ya kubebea,
viberiti,

angalau hivyo vina cash flow nzuri kwa upande wangu.
Haya sokoro weito
 
Prestige ndo nini

IMG_8184.JPG
 
Nipo kwenye hii biashara (rejareja).... Nimefanya kaubunifu flan ka kuongeza maziwa ya mgando ya mgando na cake tam baada ya kugundua kuna uhitaji....... Nasubri laini zang za figo pesa na Mpesa..... Vyote hv (maziwa, figo, m-pesa) nimefanya kwaajil ya kujiingizia pato tengefu au la pemben..... Mfano maziwa kwa mwez (predictably) napata si chin ya laki na nimeanza wik 3 zilzopta... Expecting to increase......kwa upande wa tigo na m-pesa sijajua maana sijawahifanya na lain zang hazijatoka bado miez 2 ss... Hvyo mwnye uzoefu naomba kujua pato lake kwa mwezi....

Hapa pia naomba kuongezewa ubunifu mwngine wa biashara nyingine simple kama ya hyo maziwa itakayo nipa kuanzia laki (100, 000) kwenda juu.....

Asanteni.....

Note:
Duka lina miez 3 ss.
Na mimi nasubiri majibu\ ushauri hapa
 
Tafuta fremu fungua duka....nenda TRA kaombe TIN number (siku moja tu unapata), watakupa tax clearance nenda halmashauri kaomba leseni ya biashara ndani ya siku saba unapata na gharama ni 70,000 tu. Then waulize hapo halmashauri bibi afya yuko wapi ili wakupe certificate ya afya maana wanasumbua baadae kama huna cheti cha afya. Kwangu walikuja wanataka kunipiga faini eti kwanini nauza unga na maharage sina cheti cha afya... uduanzi kabisa. Ila niliwafuata wakanipa. Then pale dukani nunua dust bin la uchafu la kuweka maganda ya pipi, chupa za maji nini nakadharika ili wasije jamaa kukupiga faini maana siku hizi pesa baba inatafutwa kama nini. Then fungua duka kula vichwa hapo....mambo ya kisheria yameishai hapo. Kitambulisho mimi sikuchukua maana mtaji wangu ni zaidi ya milioni 4 kwa mwaka na wala sitaki umasikini na kusumbuana na watu....

Ajabu juzi walikuja watu wa halmashauri ya ubungo wakawa wamejaza form eti wanasema nauza duka bila kulipa service levy. Na wakawa wamesaini kwenye karatasi eti nimekubali nilipe faini 380,0000/-. Nikawaambia kuwa kwa nini mimi nilikuja kuomba leseni pale Halmashauri hamkuniambia kuhusu mambo ya service levy? na iweje wewe usaini siani yako kwa kuandika jina langu alafu useme mimi nimekubali. Nikawaambia kuwa utaratibu ni nyie kunipa elimu alafu niende kama natakiwa kulipa service levy nilipe sio kuja na kunitisha na makaratasi mengi alafu unataka pesa on the spot 380,000/-. Tulizinguana wakaondoka hawajarudi mpaka leo na wala sijui kama natakiwa kulipa service levy au la!!! Ila acheni bana wafanyabiashara wanateswa na hawa watu wanajiita manispaa duhhhh....ila nakomaa nao tu ninapoelewa tunaenda sawa nisipoelewa mtiti kweli kweli mpaka nielewe, huwa sitoi pesa hivi hivi
Safi sana hawa manspaa wanajionaga wao ndo wao
 
Biashara ya duka la rejareja siyo ya kudharau hata kidogo. Inatunza familia kabisa na kusaidia kugharamia baadhi ya matumizi kwenye familia. Watu wengi waliotanguliaga kuifanya hii biashara wako mbali saaana, wenmgine wamejenga na kumudu hadi nyumba 'ndogo nyumba' kwa retail shop.

Wengi wameshaongea mengi mazuri kwenye kurasa zilizopita, na mimi sababu ni mzoefu kiduchu, wacha pia nitoe mawili matatu ambayo sijaona yakiorodheshwa hapa, huenda watu wanafanya katika maduka yao au hawafanyi, kama hufanyi unaweza tendea kazi.

USIACHIE FURSA. Kamwe usiuze 'HAKUNA'
Kitu kikubwa katika maduka ya rejareja ni kuhudmia hitaji la kila mmoja kadri uwezavyo. Kamwe usiuze hakuna ikiwa inawezekana icho kitu/bidhaa inaweza kuuzika katika duka lako. Hata kama mhitaji ni mmoja, mletee anachotaka. Ili mradi kile anachohitaji kipo kwenye uwezo wako na unaridhia kuuzika kwako.

Biashara ya vilevi na sigara.
Siagara, Angalia eneo lako la biashara kama kuna watu wanahitaji sigara wawekee.(ikiwa umeridhia na hufungwi na imani yako pia) Beer unaweza weka bia katika miundo miwili, kuuza take awa y(wanaenda kunywa nyumbani), au kama eneo linaruhusu, kukawa na kasehemu wakawa wanakunywa kwa ndani/bandani (duka-grocery). NB usieke pombe ya banana kama eneo lako ni la wastaarabu).

Pombe za kupima kwa shot
Pima K-Vant, Valuu, Konyagi n.k kuendana na eneo shot 500/1000. Weka vipombe vichupa vidogo: Azura/Rivella/Zed/Highlife/Konyagi ndogo/KVant ndogo, ukinunua kwa caton utapata faida kubwa zaidi, ukinunua kwa maduka ya jumla pia utapata pia.

Mfano kwa maduka ya jumla Azura/Rivella n.k unanunua 1600 unauza 200O kwa piece.
K-Vant unanunua 3000-3100, kuuza ni 4000
Konyagi 2700-2800, kuuza ni 3500 n.k.

Vitu vya kupima pima
Kuna mchangiaji ameshaeleza kuhusu Prestige za kupima kwenye kurasa zilipita. Labda niongezee
Maziwa: Kuna maziwa ya kupima, ya fresh/chai na ya mtindi, itategemea zaidi na eneo ulipo sababu ya usafi/usalama kwa wateja wako. Maziwa bei ya kununua na kuuzia itategemea na maziwa unayapata kwa bei gani. Kuna vitu vingine dukani vinatembea fasta pia, kama unga wa lishe, unaochanganya mwenyewe pia. Ila kwa lengo la kuzungusha hela na kueka ubora unaeza nunua kwa watu na kisha ukaweka marhin kidogo ukauza dukani kwako.

Vitu kama sembe, dona kama unaeza saga mwenyewe, margin inakuwa kubwa zaidi kuliko kununua.

NB: Hakikisha unatoa bidhaa bora inayofanana na hizi unga za special, wateja wengine hawaangalii brand, wanaangalia ubora/ladha basi.

Changamoto:
Changamoto za serikali anzia za kata (Bwana Afya), Manispaa (Ushuru) na TRA -Kodi haivikwepeki, kutana nao utajua jinsi ya kudili nao.

Udokozi wa muuzaji
: Usipokuwa makini na stock zao utashangaa binti/kijana wa dukani anabadili nguo,saa na vitu vingi kwa kukuibia, kama hufanyi stock kwa kubanwa na muda, funga camera hata mbili tu, zinawaogopeshaga kuiba.
 
Biashara ya duka la rejareja siyo ya kudharau hata kidogo. Inatunza familia kabisa na kusaidia kugharamia baadhi ya matumizi kwenye familia. Watu wengi waliotanguliaga kuifanya hii biashara wako mbali saaana, wenmgine wamejenga na kumudu hadi nyumba 'ndogo nyumba' kwa retail shop.

Wengi wameshaongea mengi mazuri kwenye kurasa zilizopita, na mimi sababu ni mzoefu kiduchu, wacha pia nitoe mawili matatu ambayo sijaona yakiorodheshwa hapa, huenda watu wanafanya katika maduka yao au hawafanyi, kama hufanyi unaweza tendea kazi.

USIACHIE FURSA.,,,,Kamwe usiuze 'HAKUNA'
Kitu kikubwa katika maduka ya rejareja ni kuhudmia hitaji la kila mmoja kadri uwezavyo. Kamwe usiuze hakuna ikiwa inawezekana icho kitu/bidhaa inaweza kuuzika katika duka lako. Hata kama mhitaji ni mmoja, mletee anachotaka. Ili mradi kile anachohitaji kipo kwenye uwezo wako na unaridhia kuuzika kwako.

Biashara ya vilevi na sigara.
Siagara, Angalia eneo lako la biashara kama kuna watu wanahitaji sigara wawekee.(ikiwa umeridhia na hufungwi na imani yako pia)
Beer unaweza weka bia katika miundo miwili...Kuuza take away(wanaenda kunywa nyumbani),,,au kama eneo linaruhusu, kukawa na kasehemu wakawa wanakunywa kwa ndani/bandani (duka-grocery). NB usieke pombe ya banana kama eneo lako ni la wastaarabu).

Pombe za kupima kwa shot...pima K-Vant, Valuu, Konyagi n.k kuendana na eneo shot 500/1000
Weka vipombe vichupa vidogo,,,Azura/Rivella/Zed/Highlife/Konyagi ndogo/KVant ndogo, ukinunua kwa caton utapata faida kubwa zaidi, ukinunua kwa maduka ya jumla pia utapata pia.

Mfano kwa maduka ya jumla Azura/Rivella n.k unanunua 1600 unauza 200O kwa piece.
K-Vant unanunua 3000-3100....kuuza ni 4000
Konyagi 2700-2800 ....kuuza ni 3500
n.k ....n.k.

Vitu vya kupima pima...Kuna mchangiaji ameshaeleza kuhusu Prestige za kupima kwenye kurasa zilipita. Labda niongezee
Maziwa: Kuna maziwa ya kupima, ya fresh/chai na ya mtindi, itategemea zaidi na eneo ulipo sababu ya usafi/usalama kwa wateja wako. Maziwa bei ya kununua na kuuzia itategemea na maziwa unayapata kwa bei gani.
Kuna
Kuna vitu vingine dukani vinatembea fasta pia, kama unga wa lishe, unaochanganya mwenyewe pia. Ila kwa lengo la kuzungusha hela na kueka ubora unaeza nunua kwa watu na kisha ukaweka marhin kidogo ukauza dukani kwako.

Vitu kama sembe, dona kama unaeza saga mwenyewe, margin inakuwa kubwa zaidi kuliko kununua NB,,,hakikisha unatoa bidhaa bora inayofanana na hizi unga za special, wateja wengine hawaangalii brand,,,wanaangalia ubora/ladha basi.

MAGENDO:
Kuna watu huwa ni wapagazi/wasambazaji wa ma super dealer, huwa sijui wanaibagaje, ila wanaletaga bidhaa walizokwapaua kwa mabosi zao, sana sana nilichowahi nunua zaidi ni sukari, mchele mafuta na sabuni, bei zao huwa zinakuwa chini sana, mfano mfuko wa sukari wa 50Kg wanakuuzia 85,000. Angalizo, wakidakwa umedakwa, ;JELAAA'

changamoto:
Changamoto za serikali anzia za kata (Bwana Afya), Manispaa (Ushuru) na TRA -Kodi haivikwepeki, kutana nao utajua jinsi ya kudili nao.
Udokozi wa muuzaji: Usipokuwa makini na stock zao utashangaa binti/kijana wa dukani anabadili nguo,saa na vitu vingi kwa kukuibia, kama hufanyi stock kwa kubanwa na muda, funga camera hata mbili tu, zinawaogopeshaga kuiba.
Asante ndugu
 
Brother
Hongera kwa wazo zuri
Kiukweli natambua japo sio kiundani sana kuhusu duka la vyakula
Yaan reja reja
Kila kitu kina faida yake na hiyo faida ni kuanzia 20 au zaidi
Mm nina duka la vyakula
Nakupa mfano wa vitu vichache vinavyotoka na vina faida zaidi ya 20%
Karanga 50kg ni 125000 nauza 3000*50=150000 faida ni 25000/
Azam poa (unga wa ngano ) nanunua 30 nauza 37500 faida =7500
Makande nanunua 50kg kwa 60,000 nauza 75000
Faida 15000
Sunkist unga wa ngano
Nanunua 28000 nauza 36000 faida 8000
Mafuta ya safi lt 20 nanunua 57000 nauza 70000 faida ni 13000
Huo ni mfano tu vipo vingi vyenye faida pasu kwa pasu
Mfano
Bambino
Wembe
Sindano
Uzi za viatu
Mifuko
Uzi za nguo
Nk
Hivyo usimamizi ukiwa mzuri na location nzuri utapata faida
Ila kumbuka kuuambia moyo wako utulie mjini kuna vya watu
Kila la heri mkuu
 
Naona bora hata duka la vyakula lina maslah kuliko duka la kawaida maana kuna bidhaa inakupa faida ya 8000 sasa kwny duka la kaawaida kuna baadh ya takeaway unanunua sh 417 unakuja kuuza 500 kweli utatoka?
Brother
Hongera kwa wazo zuri
Kiukweli natambua japo sio kiundani sana kuhusu duka la vyakula
Yaan reja reja
Kila kitu kina faida yake na hiyo faida ni kuanzia 20 au zaidi
Mm nina duka la vyakula
Nakupa mfano wa vitu vichache vinavyotoka na vina faida zaidi ya 20%
Karanga 50kg ni 125000 nauza 3000*50=150000 faida ni 25000/
Azam poa (unga wa ngano ) nanunua 30 nauza 37500 faida =7500
Makande nanunua 50kg kwa 60,000 nauza 75000
Faida 15000
Sunkist unga wa ngano
Nanunua 28000 nauza 36000 faida 8000
Mafuta ya safi lt 20 nanunua 57000 nauza 70000 faida ni 13000
Huo ni mfano tu vipo vingi vyenye faida pasu kwa pasu
Mfano
Bambino
Wembe
Sindano
Uzi za viatu
Mifuko
Uzi za nguo
Nk
Hivyo usimamizi ukiwa mzuri na location nzuri utapata faida
Ila kumbuka kuuambia moyo wako utulie mjini kuna vya watu
Kila la heri mkuu
 
Back
Top Bottom