OK,, mtaji ni wewe mwenyewe nguvu zako tu,mtaji mkubwa faida kubwa.So mtaji inaweza kuwa hata laki tano na mpaka billion kadhaa.
Biashara iko hivi:Kipindi msimu unaanza wakulima (tulio wengi) huwa hatuna hata ela ya kununua chumvi halafu kipindi hiki ni kipindi ambacho cha kuokota na kuziweka ili zipelekwe ghalani kwa ajili ya mauzo.Wakulima wanakuwa bize sana kwenye kazi za shamba wakati hakuna ela wanayoingiza.
Hivyo,kwakuwa hali ya uchumi inakuwa ngumu sana kwa kipindi hiki,baadhi hugawa sehemu ya kipato chao huuza nje ya utaratibu Wa Mnada kwa watu wenye ela.Mkulima atakujia atakuambia Nina gunia zangu mbili pale Nina shida ya ela nisaidie.Wewe ukiwa na ela unampa anakupa mzigo.
Kwa mfano Ikiwa umenunua kila kilo kwa Tsh.1300/=,
Ule mzigo wewe ukipeleka mnadani utauza kwa Tsh.3500,utakuwa umepata faida ya sh.2200.
Na kwakutumia mfumo Wa mnada ela haziji haraka kwa wakulima,mfano mkulima amepeleka mwezi Wa kumi sokoni korosho zake lakini mpaka mwezi Wa kumi na moja bado hajapewa ela zake.Kwahiyo mwezi mmoja mkulima hana ela hata kama amepeleka mapema.Hivyo basi watu huuza sana chomachoma.
Na kama mkulima akauza mapema sana mzigo wake na akapata ela kwa wakati anao uwezo Wa kuizungusha hata Mara tatu au tano mpaka msimu unaisha.Kwahiyo ukianza na mtaji Wa kueleweka mpaka unaishia msimu utakuwa umezungusha sana ela yako kwa manufaa.