Biashara ya Kuchakata na Kufungasha Unga wa Mahindi (Sembe na Dona)

FIDO DIDO

Member
Joined
Mar 6, 2012
Posts
24
Reaction score
7


Hellow wanaJF,

Nina wazo la kuanzisha biashara ya kusaga unga wa sembe na ku-pack kwa ajili ya kuuza. Jamani naombeni mawazo yenu.


WADAU WENGINE WANAOHITAJI KUJIFUNZA KUHUSU BIASHARA HII
Habari zenu wadau,

Ninaomba kama kuna mzoefu wa biashara hii aweze kunisaidia mawazo jinsi ya kuanzisha biashara ya kusaga, kukoboa na kuuza unga pamoja na kujua ni mashine aina gani zinafaa kwa kazi hii pamoja na bei zake.

Natanguliza shukrani.


MICHANGO YA WADAU KUHUSU BIASHARA HII
 
Wazo lako ni zuri, kwani kuwekeza ktk chakula na ukahakikisha unakidhi viwango na mahitaji ya walaji wako utanufaika na kunufaisha wengi, binafsi nakushauri endelea na mpango wako.
 
Ni biashara nzuri, tafuta location nzuri ambayo distribution itakuwa within that radius, then capture the market with quality product and competitive price.
 
Asante mkuu nipo na Dar na nimetafuta location maeneo ya kimara kwa ajili ya kufunga mashine but sijapata kampun ya uhakika ya kunitengenezea mifuko kwa ajili ya ku-pack.
 
Ahsante mkuu nipo na dar na nimetafuta location maeneo ya kimara kwa ajil ya kufunga mashine but sijapata kampun ya uhakika ya kunitengenezea mifuko kwa ajil ya ku pack.

Watafute Hill Packaging. Huyu jamaa mmiliki anaitwa Hillary ni mjasiriamali mzuri sana, ana kiwanda cha kutengeneza viroba kipo mapinga Bagamoyo mwanzo kabisa karibu na Bunju.
 
Vizuri sana mkuu, Tanzania inahitaji watu kama wewe.
 
Mkuu hiyo ni plani nzuri sana na hata mimi nina huo mpango na naendelea kuuvutia kasi.

MKUU HII BIASHARA UKIWA SIRIAS UNAWEZA KUWAFIKIA WAKINA AZAM MAKE NA WAO HAWAKUANZIA JUU

- Ila unatakiwa kuwa mbunifu sana na kufanya watu wanunue bidhaa zako na si za wengine make wanaofanya hii business wako wengi so ni kwa nini wanunue kwako na si kwa wengine?
 
Watafute Hill Packaging, huyu jamaa mmiliki anaitwa Hillary ni mjasiriamali mzuri sana, ana kiwanda cha kutengeneza viroba kipo mapinga Bagamoyo mwanzo kabisa karibu na Bunju

Mkuu LAT hawa Jamaa wanafanya kazi ya Ku pack kwenye chupa pia? Nina mpango wa kuanzisha kiwanda cha juice na ninahitaji watu wa kunifanyia Packaging mkuu.
 
Mkuu LAT hawa Jamaa wanafanya kazi ya Ku pack kwenye chupa pia? Nina mpango wa kuanzisha kiwanda cha juice na ninahitaji watu wa kunifanyia Packaging mkuu.

Hapana, wao ni viroba tu.

Mkuu, kwanini usifanye sourcing ya mashine ya ku pack juice china, ukanunua pep bottles na kupack mwenyewe, very very convinient.
 
Asante mkuu nipo na dar na nimetafuta location maeneo ya kimara kwa ajil ya kufunga mashine but sijapata kampun ya uhakika ya kunitengenezea mifuko kwa ajil ya ku pack.
Ebwana, hongera sana, nami nilikuwa na wazo kama lako, vitu vingine utanishauri na vingine tutapata kwa wadau humu JF.

Mimi pia nataka niwe nakoboa na kusaga unga wa sembe, na nitafuga nguruwe, kuku wa kienyeji na ng'ombe kadhaa wa maziwa ambao nitakuwa nawapatia hizo pumba nitakazokuwa nazipata.

Naomba unisaidie kujua ni vitu gani ambavyo natakiwa niwe navyo na (estimated cost) ili nifanikishe ku-implement huo mradi.

Na je, naweza kuweka mashine ya kutumia mafuta badala ya umeme. Je, mashine zinazotumia solar zinapatikana? (Msinicheke jamani ktk swali hili)

Mtaji na soko siyo tatizo kwa sababu tayari nina reliable market ya ku-supply kg 150 kwa siku
 

Mkuu, 150 kg ni viroba vitatu vya 50kg!
 
Mkuu, 150 kg ni viroba vitatu vya 50kg!!!!!!!!!!!!

Eeh mkuu, ni sawa na viroba 90 kwa mwezi (hapo sijachanganya zile za jumla kwa wale wenye viduka vidogo vidogo).

After all, hii ni shughuli ambayo nataka nimpatie ndugu yangu ambaye anazubaa zubaa mtaani, mimi nitakuwa natumia pumba kwa kulisha nguruwe nitakaowaweka.
 

Mkuu, unahitaji kuwa na supply ability kubwa kwani biashara hii ina demand kubwa. Kuna bwana mdogo mmoja hapa dar mwananyamala ana mashine ambapo anasaga unga wa sembe na kuuza takriban viroba 120 kila siku. Pumba anauza kwa jumla.

Jiandae mkuu hii project ni nzuri sana na siyo ya kumuachia mtu anaye zuba zubaa, itakupeleka mbali I promise you
 
Hellow wa jf na wazo la kuanzisha biashara ya kusaga unga wa sembe na ku pack kwa ajil ya kuuza, jaman naomben mawazo yenu .

Kwa ushauri wangu hilo eneo la kimara ungelifanya eneo la kusambazia yaani front office, na eneo ambapo malighafi zinapatikana ukaweka mitambo kwa ajili ya kupack hivyo vifurushi yaani back office.
 
Mkuu asante sana kwa ushaur wako nitaufanyia kaz soon then tutapeane updates, I hope mambo yataenda shwari.
 
Na je, naweza kuweka mashine ya kutumia mafuta badala ya umeme
Je, mashine zinazotumia solar zinapatikana? (Msinicheke jamani ktk swali hili)

- Unatakiwa uwe na machine nzuri sana ya kukoboa na kusaga (unaweza kusaga unga kwa mara ya pili ili kupata unga laini zaidi)
- Uwe na mahindi mazuri ambayo hayajaliwa na wadudu (lengo unga usiwe na harufu ya uozo)

- Sehemu nzuri ya kuhifadhi unga ili usiharibike (kusiwe na joto sana wala unyevunyevu), njia nzuri na rahisi ya kumaintain quality ya unga ni kuuanika juani baada ya kusaga kabla ya packaging (ukipigwa jua siku 3 au 4 utadumu muda mrefu sana)
- machine za mafuta zipo (kerosine) huwa zinatumika sana vijijini.

- Solar machine sijawahi kusikia & am sure haiwezekani c'se energy consumption ya machine ni kubwa sana, kupunguza consumption unatakiwa kusaga mahindi mengi bila kuzima zima machine

Challenge: Unahitaji watu waaminifu sana kusimamia machine yako na watu wa kuyasafisha mahindi vinginevyo utaibiwa vibaya sana
 
Safi mkuu n vizuri kama una wazo kama langu na unatakiwa uwe na mashine mbili moja ya kukoboa na nyingine ya kusaga, then mashine nzur yenye horse power 50 at least pia viroba ya ku pack unga +plus log na muonekano mzur wa packaging style, pia packaging machine, ma tank ya kuweka maji ya kutosha kwa ajil ya kusafisha yale mahind yawe saf pia itasaidia ata unga uwe saf, store saf .

Alafu mkuu me naona pia ku pack na unga wa dona coz kuna watu wengine hawapend sembe.n hayo mkuu mengine n marketing techniques ambayo hapa JF tumeshapata na tutaendelea kupata.

Thanks
 
Bila kusahau kuweka machine ktk location nzuri iliyo mbali na makazi ya watu. Lengo ni kuondoa matatizo na majirani ambao ni lazima watalalamia kuhusu kelele za machine yako, kusababisha nyufa kwenye nyumba zao na uchafuzi wa mazingira.
 
bila kusahau kuweka machine ktk location nzuri iliyo mbali na makazi ya watu. Lengo ni kuondoa matatizo na majirani ambao ni lazima watalalamia kuhusu kelele za machine yako, kusababisha nyufa kwenye nyumba zao na uchafuzi wa mazingira

Yap hiyo nayo wazo lingine mkuu much respect.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…