Biashara ya Kuchakata na Kufungasha Unga wa Mahindi (Sembe na Dona)

Biashara ya Kuchakata na Kufungasha Unga wa Mahindi (Sembe na Dona)

By experience!

Nenda mikoa ya Iringa au Mbeya, nunua mahindi moja kwa moja kwa wakulima, sogeza mahindi kwenye mashine ya kusaga iliyo karibu ili kupunguza carriage cost!
NB: hapa uwe umeshaongea na watu wa mashine, ikiwezekana uwe unawaachia pumba ili gharama ya usagishaji iwe chini zaidi (chini ya 5000/= kwa gunia)

Mahindi yakifika kiasi unachotaka, anza kusaga na kupaki(kwa kuanza unaweza kuwa unatumia mashine ya kushonea ya kukodi na mifuko yenye nembo ya mtu mwingine (mtafute)!

Gharama ya mfuko tupu usio na nembo ni around 200-350 bei ya jumla na 400-600 wenye nembo)

Kipimo kiwe kilo 5, 10, 25 na 50 (gharama ya upakiaji kwa makuli ni around 700 kwa kila kilo 50!

Tafuta magari yanayosafirisha mizigo mikubwa, ongea nao wakuunganishie mzigo wako kwa wasafirishaji wengine (madalali are so good in this)!

Mzigo ukifika mkoa wako wa soko waombe wakushushie sehemu ambayo ni rahisi kwako!

Zambaza mzigo kwa wateja wako!

Nzuri ukiwa unasaga kwenye mashine zako ili kudhibiti viwango.
 
Mkuu habari za majukumu, nimevutiwa sana na maamuzi yako ya uthubutu! Na hakika utafanikiwa!
 
Watu wameulizwa bei za mashine wanakazana kutaja ubora wa mashine kama amjui bei si mkae kimya tu.
 
Hawa hapa Wanajiita CP 0684 611 167..Kwa hapa Dar...OFFICE zao ..ziko Mlimani City ila juzi nilitoka Moro nimewakuta 88

Mkuu Hii CP kirefu chake Ni nini? Maana najaribu kugoogle sijawapata
 
MKUU MIMI NINAZO MACHINE MPYA ZA KUSAGA NA KUKOBOA.ZIPO SET 2 ZA KUKOBOA NA SET 2 ZA KUSAGA.ZIPO COMPLETE KUANZIA MOTORS ZAKE NA ACCESORIES NYINGINE ZOTE.NAZIUZA KWA BEI RAHISI.BEI YA SET MOJA YA MACHINE HIZO DUKANI KWA SASA NI 3.7 MIL(VAT INCL).MIMI NAUZA SET MOJA KWA 2.5MIL TU.MACHINE HIZI NI BRAND NEW.HAZIJATUMIKA.NA MIMI NILIZINUNUA KWA AJILI YA KUANZISHA PROJECT YA KUSAGA NAFAKA,BAHATI MBAYA ALIYENIAHIDI MTAJI HAKUTIMIZA TENA AHADI YAKE.MACHINE HIZI ZIPO DSM MBEZI BEACH.MKUU,KAMA UTAKUWA INTERESTED TUTAFUTANE KWENYE 0767 610068
 
Bei ya kutengeneza kinu cha kusagia mahindi cha panga 8 ni 1.5ml bila mortar (sina uhakika na spelling za mota kwa kizungu) kinu cha kukoboa ni 1.3 mpaka 1.4 bila mortar. Mortar ya 40HP ni 1.3mil that means utahitaji mbili kwa mashine zote i mean kusaga na kukoboa.

Bag sealer (mashine ya kuishonea viroba) hizi ni cheap we andaa kama 250000 mpaka 300000 kwa mashine moja ila za india ni nzuri zaidi. If you need more info we ni pm mkuu nipo huko kwa muda sasa.
Nisaidie kazi seriously hata ya kupepeta mahindi mkuu
 
Mashine zipo kwa size,nashauri kwa kusaga sembe kinu cha kusaga utumie size 100,na chakukoboa tumia roller 3 au roller 4,Vinu imara kwa hapa bongo ni vya kuchonga kwenye viwanda vidogovidogo vya bongo ndio vizuri, coz madukani vingi ni vya kihindi mabati yake ni laini mno hua havidumu,lakini pia sijawahi ona kinu cha roller 3 cha India.Mashine zote hizi zinahitaji motor ya hzp 40 ambazo moja ina range 1.3-1.5 Tsh inategemea jinsi utavyoipata,Mimi niko huko kitambo na wiki iliopita nilitengeneza chakusaga size 100 kwa 1.4 na chakukoboa kwa 1.2,vinu hivi vinauwezo wakusaga 1tone/hrs.
Siwezi kupata kazi hata ya kupepeta mahindi mkuu.
 
T
Safi sana Lutifya.

Hawa wanapatikana wapi mi niko temeke? Na je nikinunua lazima niwapelekee au watakuja kiwandani? Na je hii biashara inanilazima kusajiri TFDA na TBS?
FDA na TBS ni lazima
 
Piga hizo namba. CP nadhani ni kifupi cha Kampuni yao.
Wadau CP wamefunga ofisi Dar tangu Oct 2016 waliingia mgogoro na serikali awau hii kuhusu kulipa vat kwenye miradi yao walikuwa kiwanda cha chakula cha kuku kule chang'ombe na shamba kuku Kibaha! Walishaanza kazi ilikuwa nzuri sana wanakupa mkataba unawatunzia kuku wanakupa kila kitu bure mnakatana mwisho na wao wanakuja wanunuzi wa kuku wote! Sasa issue za kupewa unafuu wa kodi kwenye mazao kilimo na mifugo wakashindwana wakaona hailipi! Wamesepa!!!
 
Wadau CP wamefunga ofisi Dar tangu Oct 2016 waliingia mgogoro na serikali awau hii kuhusu kulipa vat kwenye miradi yao walikuwa kiwanda cha chakula cha kuku kule chang'ombe na shamba kuku Kibaha! Walishaanza kazi ilikuwa nzuri sana wanakupa mkataba unawatunzia kuku wanakupa kila kitu bure mnakatana mwisho na wao wanakuja wanunuzi wa kuku wote! Sasa issue za kupewa unafuu wa kodi kwenye mazao kilimo na mifugo wakashindwana wakaona hailipi!!!! Wamesepa!!!
Asante ndugu kwa taatifa, huu ni Msiba jamaa walikuwa wanamaanisha kwakweli, na wengi walinufaika sana Ila ndio watakatifu hawataki kuona watu wanainuka. [emoji16] [emoji16]
 
Mashine zipo kwa size,nashauri kwa kusaga sembe kinu cha kusaga utumie size 100,na chakukoboa tumia roller 3 au roller 4,Vinu imara kwa hapa bongo ni vya kuchonga kwenye viwanda vidogovidogo vya bongo ndio vizuri, coz madukani vingi ni vya kihindi mabati yake ni laini mno hua havidumu,lakini pia sijawahi ona kinu cha roller 3 cha India.Mashine zote hizi zinahitaji motor ya hzp 40 ambazo moja ina range 1.3-1.5 Tsh inategemea jinsi utavyoipata,Mimi niko huko kitambo na wiki iliopita nilitengeneza chakusaga size 100 kwa 1.4 na chakukoboa kwa 1.2,vinu hivi vinauwezo wakusaga 1tone/hrs.
Mkuu gimmy's uko poa? Business inaendaje? Ebwana na mie napiga hatua za kuingia kwenye business hii sasa hivi, ndo nimechukua mashine zote mbili na Mungu akibariki basi mwisho wa mwaka huu niingie kwenye production!
Please tunaomba ma legend wa hii biashara muwe mnashea uzoefu wenu ili wachanga tusifanye mistakes zisizo za lazima!
 
Back
Top Bottom