Mkuu ni vyema kweli kujifunza hata mimi hapa najifunza kutoka kwa walionitangulia na kunishawishi niingie huku kwa kweli kuna watu wako juu kiasi kwamba wao mchele wao ni wa kimataifa simu wanazopokea ili wapeleke mzigo ni kutoka Rwanda, Kenya na wanapeleka kweli ila nasi ndo tunawapatia mzigo na tunapata faida ya kutosha.
Kizuri zaidi ni kupiga zote mchele mpunga vyote nunua kama una nafasi na una sehem nzur ya kuhifadhi kwani kuna wakati mpunga unakuwa chini sana kati ya 35 000/- na 55,000/- tu katika mikoa ya Katavi na shinyanga respectively lakini baada ya muda fulani unauza kwa 85000/- hadi 100,000/ - na ukikoboa inakuw zaidi ya hapo.
Hapa mwenzako ni kuzunguka tu mikoani kama mtalii wa ndani ila watu wanakusanya punga na hata shambani naingia.
Hakuna kitu kitamu kama hii game mkuu vigari vya M20 kwako itkuwa kawaida tu hadi natamani serikali iache amsha amsha inayofanya kwa vijana kuhimiza wajiajiri-waachwe waendelee kusubiri ajira za kuagizwa maana wao waziona hizi kazi ni kizamani. Kusema kweli namuona mbunge mmoja yuko kwenye kilimo na anapiga gunia 5, 000/- na anapeleka sijui nje na ana trecta zake kwa kweli hata wananchi wakimpiga chini ubunge hana njaa kabisa.