Biashara ya Kununua na Kuuza Mazao (nafaka): Jifunze Mbinu za Kuanzisha na Kusimamia

Biashara ya Kununua na Kuuza Mazao (nafaka): Jifunze Mbinu za Kuanzisha na Kusimamia

Wadau naomba ujuzi weno kwenye hi biashara, Je nikianza na shilingi milioni 5 itanitoa? Je kuna changamoto zipi nitarajie kukutana nazo.Binafsi napenda sana kujiajiri.Robert Kayosaki anasema kwenye kitabu chake cha poor dady & Rich dady ya kwmba a highly paid slave is still a slave.WanaJF naomba kuwakilisha Hoja.
mkuu jua tofauti kati ya KUWASILISHA na KUWAKILISHA.hapa una WASILISHA na sio KUWAKILISHA
 
Labda niseme tu,Soko la mazao mfano Mchele linahitaji huwe na mitaji miwili,ni kiwa na maana kwamba Wanunuzi karibu wote wa mchele hasa Dar hawawez kukulipa Cash Pesa ,so kuepuka usumbufu lazima uwe na Stock na mtaji utaofaya mda wote uweza kukusanya Mzigo
 
Habari zenu wapendwa mim ni mgeni hapa wilaya ya mbozi nimefika hapa katika harakati za kutafuta maisha niko na mtaji kiasi kidogo hivi kama milion moja naomba mnipe mawazo nimewaza kuanza kufanya biashara ya nafaka nanunua vijijini na kuja kuuza town lakini sna uzoefu nipeni ushauri ni nifanye ili niweze kufanikiwa nina imani nikiwa na discipline hicho kidogo nilichonacho knaweza nitoa npeni ushauri.​
 
Nahitaji mawazo yenu ni muhimu xna kwangu
 
Naona watu wako kimya kumbuka ukinishaur unakua umetengeza ajira kwa watu wengi kwani mim nikifanikiwa ntasaidia wengine na kwa kuwaajiri
 
  • Thanks
Reactions: m2u
Unaweza ukanunua mpunga.then ukakobolesha mwenyewe.katika machine za Ku grade alafu ukawa unasafirisha na kuuza Michele...iyo ndo inalipa...pana gunia la mpunga utanunua sh 60,000 kukoboa gunia 3,500. Kwa mpunga mkubwa litatoa kilo 70-72.hivyo kama una mtaji Wa laki sita utapata gunia 10,ambazo ukikoboa..utapata kilo 700-720...kwa kilo utauza sh 2000,,hivyo utakuwa na income ya sh.1,400,000..karbu morogoro.
Morogoro sehemu gani kaka
 
Nisaidie mawazo kwa mwenye uzoefu na biasha ya kuuza nafaka kam unga, mchele, ngano, karanga, ulezi, maharage na vingin ving. Angalau jinsi ya kuanza na changamoto zinazoweza kujitokeza
 
Hivi kwa anaefungua fremu la kuuza nafaka ni lazima awe na TIN pamoja na leseni ya biashara?
 
mh, hata kama mchele unatoka hapa hapa tz karatasi za tfda na afya zinahitajika?
Tatzo sio mchele unatoka wap,hawa wametubana sababu unauza chakula,so cheti cha afya unakipata na tfda lazima haina mjadala
 
Habari zenu wana jamvi.

Naomba ufafanuzi kidogo kwa watu waliowahi kuuza/wanaofanya biashara ya nafaka mkoani mwanza. Napenda kufahamu ni maeneo gani hasa wanatoa mchele, maharage, choroko, dengu, njugu na nafaka nyingine kama hizo kwa bei nafuu. Pia ningependa kujua ni masoko yapi hapa mwanza biashara ipo vizuri kuanzia soko la Buhongwa mpaka igoma eneo lipi ni zuri zaid. Na pia changamoto ya biashara hii.

Naomba kuwasilisha.
 
Back
Top Bottom