Ntwa A. Katule
JF-Expert Member
- Jan 4, 2017
- 239
- 230
Sikuipata bure hiyo database mkuu. Si lazima kuishare mkuu. Nilifanya jitihada kupata. Simlazimishi yeyote. Siku njemaYaani ndio maana bongo kuendelea kazi ipo. Wewe si umsaidie mwenzako akupe mrejesho baada ya kuuza maana unataka cha juu utadhani dalali.
Jamaa wa nchi jirani wanafanya Export ya kufa mtu, why not Tanzania?Njioni mtupe elimu. Imekaa vizuri sana. Kenya wana export sana Maua, kahawa na Chai. Uganda ana export chai na kahawa pia ndizi za matoke anapeleka UK.
Jana nilienda kununua chai sehemu nikaona majani ya chai kutoka Rwanda. Sasa kumbe hadi Rwanda ana export kwenda duniani kwa nini na sisi tusifanye?
Ulishawahi kufika kigari ukakosa bidhaa ya tanzania? Au South Africa?Jamaa wa nchi jirani wanafanya Export ya kufa mtu, why not Tanzania?
Aisee MUNGU akubariki, hio ya ufuta nasikia ni hot cake kwa Japan. DahHakika ni biashara nzuri sana. Wengi wanashindwa kufikia matakwa ya Viwango yanayotakiwa katika masoko hayo.
Jambo la kwanza; fanya utafiti mdogo wa uhitaji wa mazao yanayotakiwa katika Nchi unayotaka kupeleka. Pamoja na kujua bei lakini mambo muhimu katika soko ni pamoja na; Viwango vya ubora vya nchi hiyo; mfano (tu) Japan wanataka ufuta wenye ubora (usio kuwa na taka taka) wa aslimia isiyopungua 95, endapo ufuta huo utatumika katika uokaji.
Viwango hivyo hutofautiana kulingana na aina mazao, soko/nchi, na matumizi ya bidhaa hizo kwa mlaji; Vivyo hivyo, wanaangalia viwango vya vimelea kama backteria, mabaki ya sumu za madawa yaliyotumika katika uzalishaji, na kuvu (fungus) nk. nk. katika mazao hayo.
Jambo hilo ni muhimu sana katika masoko ya Ulaya, Amerika na Japan. Nafuu kidogo inapatikana ukiuza katika nchi zingine kama za Uarabuni na Africa.
Hata hivyo, vitahitajika endapo mnunuzi katika nchi hizo nafuu, atataka auze Ulaya. Ni, kwa ufupi tu. Pamoja na maelezo yangu mafupi, yote hayo yanawezekana, na kuna watu wengi hapa kwetu wanafanya; kwa mazao ya chakula na viwanda. Pasi shaka, ukikaza nia utafanikiwa pia.
Kivipi?? Hebu weka nyamaChangamoto yake kubwa ni urasimu wa Serikali
http://pdf.usaid.gov/pdf_docs/Pnadx940.pdfKivipi?? Hebu weka nyama
Ndugu, ninakubaliana na wewe kwa asilimia zote. URASIMU. Mimi nilipata tenda ya kupeleka chakula cha mifugo hapa jirani tu, Kenya.Changamoto yake kubwa ni urasimu wa Serikali
Nilipata Dili flani la kupeleka Mzigo Mwingi tu Commoro nikakusanya Nguvu za Jamaa zangu Kama wawili tukakusanya Mtaji wetu mdogo tu Kama 20 Million.
Tukashauriwa Tufuate Vibali halali
Tu kaanza kuelekezwa tuanze board of external Trade, huko ikapigwa Danadana twende Chamber of Commerce kule wakatueleza kazi yao ni kutoa Vibali tu tukitaka kujua kitu gani kinaruhusiwa kipi hakiruhusiwi twende Wizara ya Mifugo au Kilimo ndio wenye orodha ya Mazao yanayoruhusiwa kusafirishwa Nje ya Nchi!
Niliwauliza wale Watu wa Chamber of commerce pale Kwny Barabara ya Morogoro na Samora ( PPF House) kwanini hiyo orodha ya vitu vinavyoruhusiwa kwanini wasikae nayo pale kupunguza Urasimu Jibu wanatoa huo ndio utaratibu 'Mzee usilete Ujuaji fuata taratibu'
Tulipofika Wizara ya Kilimo ndio balaaa Urasimu mpaka tukaamue tusafirishe kienyeji
Ndugu, ninakubaliana na wewe kwa asilimia zote. URASIMU. Mimi nilipata tenda ya kupeleka chakula cha mifugo hapa jirani tu, Kenya.
Kwa "ujinga" wangu nilitaka kurasimisha shughuli yangu kwa kufuata taratibu zote husika, wizara ya kilimo na mifugo aliyenipokea nadhani hajui hata kilichomuweka hapo, nikarushwa niende TFDA. Huko nako, wakaanza kunishangaa tu kama vile nimepotea njia. Hawajui kama wanahusika na biashara yangu. Nikarushwa niende TRA. Huko nako wakasema nipate kwanza kibali toka wizara ya kilimo na mifugo, pamoja na TFDA.
Nikaanza zoezi upya kupitia hizo office. Hakuna nilichoambulia, zaidi ya dharau kutoka kwa watumishi wa serikali.
Kwa vile mzigo ulikuwa tayari mteja ameshalipia na kutuma lori kwa ajili ya uchukuzi, tulipakia mzigo na kumwachia dereva afanye maalifa yake mzigo ufike. Hatukuwa na namna, maana mamlaka zote husika ni kama vile hawajui kwamba biashara ya nje kwa maana ya export inaleta pesa za kigeni kwa taifa.
Hapa bado kunatatizo kubwa sana! Sijui nani ataweza kutusaidia angalau kuwe na mamlaka moja inashughulika na biashara ya nje, ambapo unaweza kupata vibali na taratibu zote husika ukitaka kufanya hiyo biashara.