Cybergates
JF-Expert Member
- Dec 2, 2016
- 697
- 1,474
Nimesema walio wengi. Sijasema hakuna changamoto. Kwani wewe unafanya biashara gani?Ungenijua wala usingenitathimini hivyo, sijawai kuaajiliwa au kufanyakazi ya kibarua toka nizaliwe njoo kwenye changamoto za biashara ili ubebe uhusika ujue ulasimi wa tahasisi za kiserekali
Ninakuunga mkono> Jukumu moja ,linapewa zaidi ya vitengo 3,na kila mmoja anaogopa mwenzake!Ukifuata njia "halali" utazeeka, hii Tanzania bana, watu hawajuwi majukumu yao na hawajuwi kama hawajuwi...watakufanya deal na usipate faida.
Duh hii kaliMkuu ukihangaika na vibali utatembea hadi soli ya kiatu iishe. Wewe fanya yako kienyeji. Nina experience ya kisafirisha bidhaa za ngozi to Europe bidhaa nyingine nchi za kusini mwa africa. Nilizungukia vibali nikasumbuka sana. Nikaamua kufuata nyayo za wazee wa cross nikasafirisha bila vibali. Tz bado sana
Duuuuh kama utaratibu ndio huu nchi hii kuendelea itakuwa historia, nahisi wafanyakazi wanapoajiriwa huwa hawaelekezwi kazi kufanya au wanaelekezwa wanasahau nn wanakiwa wafanye kaaah taabu kwel kwelI.Ndugu, ninakubaliana na wewe kwa asilimia zote. URASIMU. Mimi nilipata tenda ya kupeleka chakula cha mifugo hapa jirani tu, Kenya.
Kwa "ujinga" wangu nilitaka kurasimisha shughuli yangu kwa kufuata taratibu zote husika, wizara ya kilimo na mifugo aliyenipokea nadhani hajui hata kilichomuweka hapo, nikarushwa niende TFDA. Huko nako, wakaanza kunishangaa tu kama vile nimepotea njia. Hawajui kama wanahusika na biashara yangu. Nikarushwa niende TRA. Huko nako wakasema nipate kwanza kibali toka wizara ya kilimo na mifugo, pamoja na TFDA.
Nikaanza zoezi upya kupitia hizo office. Hakuna nilichoambulia, zaidi ya dharau kutoka kwa watumishi wa serikali.
Kwa vile mzigo ulikuwa tayari mteja ameshalipia na kutuma lori kwa ajili ya uchukuzi, tulipakia mzigo na kumwachia dereva afanye maalifa yake mzigo ufike. Hatukuwa na namna, maana mamlaka zote husika ni kama vile hawajui kwamba biashara ya nje kwa maana ya export inaleta pesa za kigeni kwa taifa.
Hapa bado kunatatizo kubwa sana! Sijui nani ataweza kutusaidia angalau kuwe na mamlaka moja inashughulika na biashara ya nje, ambapo unaweza kupata vibali na taratibu zote husika ukitaka kufanya hiyo biashara.
Bado kuna nafasi ya kufanya jamboTatizo mi naona Sera na sheria hutungwa bila ya kuwahusisha wadau wote wa sekta husika
Wewe pia hapa umelalamika hujatoa suluhisho au kwa kuwa na wewe ni Mtanzania?Tatizo letu Watz tunalalamika badala ya kuchukua hatua.
Kulalama sio suluhu ya urasimu.
Tuweke mikakati na mipango shupavu kudadavua hii changamoto.
Tutamia njia za panya mpaka lini?
Tutatoa rushwa mpaka lin?
Tutalalamika mpaka lini?
Tusimame pamoja tuweke mipango imara kukwamua hivi vikwazo.
Tutafute namna serikali ijue effort yetu kwenye kilimo kuendeleza maisha yetu na nchi yetu.
Tuungane.umoja ni nguvu
Bado nchi yetu iko locked sana na sheria na Sera ambazo ukiziondoa hata serikali ibane matumizi vp watu wataendelea kupiga pesa kwa kufanya export mi naona tufanye movements campaign ya hivi vikwazo vya kibiashara ili viondolewe maana wao wanataka kodi lakini nchi haina mazingira mazuri ya biashara.Bado kuna nafasi ya kufanya jambo
Mmmh kwa mfano mm nipo mtwara kila ninapotaka kusafirisha mazao kwenda msumbiji inatakiwa nije tena dodoma kufatatlia kibali c usumbufu huu, kwa utaratibu huu kupata pesa za kigeni nchini mwetu itakuwa ishu, yaani serekali badala ya kuweka wepesi katika ishu kama hizi, bado wanataka kutumia utaratibu wa kijima, tubadilike tuache ujima wa kutumia mavifingu ya mwaka 68 huko.
Wizara ya kilimo ni mambumbumbu watupu, siku moja naona habari (itv) balozi wa pakistani(kama sijasahau) alitaka kusafirisha machungwa ila akataka wizara iwe kama mdhamini wake.Ndugu, ninakubaliana na wewe kwa asilimia zote. URASIMU. Mimi nilipata tenda ya kupeleka chakula cha mifugo hapa jirani tu, Kenya.
Kwa "ujinga" wangu nilitaka kurasimisha shughuli yangu kwa kufuata taratibu zote husika, wizara ya kilimo na mifugo aliyenipokea nadhani hajui hata kilichomuweka hapo, nikarushwa niende TFDA. Huko nako, wakaanza kunishangaa tu kama vile nimepotea njia. Hawajui kama wanahusika na biashara yangu. Nikarushwa niende TRA. Huko nako wakasema nipate kwanza kibali toka wizara ya kilimo na mifugo, pamoja na TFDA.
Nikaanza zoezi upya kupitia hizo office. Hakuna nilichoambulia, zaidi ya dharau kutoka kwa watumishi wa serikali.
Kwa vile mzigo ulikuwa tayari mteja ameshalipia na kutuma lori kwa ajili ya uchukuzi, tulipakia mzigo na kumwachia dereva afanye maalifa yake mzigo ufike. Hatukuwa na namna, maana mamlaka zote husika ni kama vile hawajui kwamba biashara ya nje kwa maana ya export inaleta pesa za kigeni kwa taifa.
Hapa bado kunatatizo kubwa sana! Sijui nani ataweza kutusaidia angalau kuwe na mamlaka moja inashughulika na biashara ya nje, ambapo unaweza kupata vibali na taratibu zote husika ukitaka kufanya hiyo biashara.
Tatizo haliko tuu kwa wafanyakazi wa Serikali jamani, tatizo letu kama nchi ni CCM CCM CCM na SERA zao za BIASHARA!Duuuuh kama utaratibu ndio huu nchi hii kuendelea itakuwa historia, nahisi wafanyakazi wanapoajiriwa huwa hawaelekezwi kazi kufanya au wanaelekezwa wanasahau nn wanakiwa wafanye kaaah taabu kwel kwel
Mmmmhh ! Mimi sijaelewa kwani awataki usafirishe au ?wizara ya kilimo ni mambumbumbu watupu, siku moja naona habari (itv) balozi wa pakistani(kama sijasahau) alitaka kusafirisha machungwa ila akataka wizara iwe kama mdhamini wake
nilicho sikitika wizara haijui ifanye nini? yule balozi alimchana yule boya pale pale na kushangaa wizara gani wapuuzi vile.
Wananunua pesa ngapi? Hawana import restrictions za vyakula?Kuna mtu ambae anaweza kupata viazi vitamu akavipeleka Lusaka akachukua hela yake ya maana tu!?
Uzi mzuri sana huu. Big up mleta mada kwa kuanzisha mjadala huu. Ku-export mazao, nchi hii ni urasimu tu ndicho kinachowakwamisha wengi. Ubabaishaji mwingi kwenye office za Serikali. Maofisa hawajuwi hata majukumu yao kama mdau alivyochangia hapo juu.
Nadhani kuna haja ya kulipigia kelele suala hili, kwamba kuwe na taasisi MOJA tu ambayo ihusike na utoaji wa vibali na clearance zote kwa mtu anayetaka kuexport bidhaa nje ya nchi.
Mie natafuta mzoefu wa biashara hii ya mazao awe 'mentor' wangu... anipe A to Z jinsi ya kufanya & kuexcel kwenye biashara ya nafaka/mazao kwa soko la hapa hapa nchini.
-Kaveli-