Habarini za muda huu ndugu zangu
Mimi ni ni kijana mwenye umri wa miaka 25, Katika kujikwamua na umasikini na tatizo la ajira Niko na wazo kwa muda mrefu la kuanzisha biashara ya Icecream, nimekuja kwenu kuomba mawazo yenu kwa anaeifahamu biashara hii anipe ufafanuzi kidogo.
Ufafanuzi ninaoomba ni huu;-
i) Changamoto za biashara hii ni zipi
ii) Mtaji wake (malighafi pamoja na mashine vinagharimu kiasi gani)
iii) Kipi kizuri Kati ya kumpa mtu awe anatembeza mtaani kwa kuweka kwenye ndoo kama wanavofanya wengi ama kununua kibaiskeli kama cha Azam
iv) Ili biashara iende ni population ipi niitargert Kati ya wanafunzi wa secondary, primary ama chuoni.
Na mengine niliyosahau unaweza kunisaidia ukawa mzoefu wa hii biashara
Mahali nilipo ni Mwanza , na nimekuja kwenu baada ya kujaribu kufuatilia kwa wanaofanya hii biashara ila ushirikiano wao ulikua ni zero, nilienda pale Salma cone maana ndio sehemu pekee nayoifahamu kwa Mwanza wanaofanya biashara hii.
Nitashukuru Sana kwa atakaenisaidia kwa haya niliyouliza,,. Ahasanteni!!!!!