Biashara ya kutengeneza na kuuza "Askrimu" (Ice Lollies)

Biashara ya kutengeneza na kuuza "Askrimu" (Ice Lollies)

Nina wateja ila kugandishia kwenye friji inanigharimu sana kwanza nafasi ni ndogo naweka vikopo havizidi 50, wapi wanakopesha Freezer mfano ile size ya kati ya 700-750K niwe nalipa Taratibu Taratibu?
 
Friji iwe ndogo kabisa! Nipe makadirio ya mtaji wa chini kabisa Cc; amu
 
Friji tafuta used utapata mpaka kwa 250k, ubuyu au ukwaju wa buku, maji lita kumi, vifuko buku vinaa 100 sukari ya ice cream (namrecommend mudy chuma kariakoo sokoni sukari tamu sana paketi jero), cmc vijiko 3 vya chakula(kariakoo kwa kipara inauzwa kwa kupimwa nusu, kilo au robo) nitarudi shoga kutype nimechoka
 
Kama una friji haifiki hata 40,000 labda kama utataka kununua cooler box al maarufu deli.
Acha utani mwenzako anazungumza icecream we unazungumza barafu, kiroba cha ule unga wakutengeneza icecream bei yake imesimama kweli kweli.
 
Uchira 1 Soma comment ya chipukizi uelewe nimeandika nini hizo taragram unaoita unga wewe naufahamu sana, sipo hapa kuonesha nachokijua(kwa ufupi najua vingi sana kwenye hii biashara) ila kumtajia makemikal mtu ambae keshasema anataka mtaji usiozidi 40,000 ni kuwa nje ya anachohitaji.
 
Kama una friji haifiki hata 40,000 labda kama utataka kununua cooler box al maarufu deli.
Hv mama hz cooler box kuna za dizain tofaut tofaut au ubora tofaut tofaut? dar wanauzaje kwa yale ya size ya kat nahsi ltr 30 kama sijakosea
 
Uchira 1 acha umang'aa soma comment ya chipukizi uelewe nimeandika nini hizo taragram unaoita unga wewe naufahamu sana, sipo hapa kuonesha nachokijua(kwa ufupi najua vingi sana kwenye hii biashara) ila kumtajia makemikal mtu ambae keshasema anataka mtaji usiozidi 40,000 ni kuwa nje ya anachohitaji.

Endelea kutupa somo mkuu, nimekaa hapa nakusubiri. Pia kama hutojali ningependa nikuulize maswali zaidi pm.
 
wakuu hebu acheni utani yani mtuu uko na wazo unataka watu wakumwagie plans, akumwagie strategy, akupen na budget zote, hebu tuwe na mitizamo mirefu jamani hilo swala utakalo ni swala la utafiti tena kwenye tasnia husika na hakuhitaji majibu mwepesimepesi
Mkuu hivi unaelewa maana ya "jukwaa" la biashara? Hapa kila mtu anatoa mawazo yake leo wewe umetoa beneficial ideas kwa mwenzio kesho anakupa yeye here we go...
 
Mkuu hivi unaelewa maana ya "jukwaa" la biashara? Hapa kila mtu anatoa mawazo yake leo wewe umetoa beneficial ideas kwa mwenzio kesho anakupa yeye here we go...
Kweli mkuu ila ilazima uje na vitu vichache vichache si kutaka kujua vyote kwa mkupuo na ukizingatia hii ni biashara kubwa , mi nadhani mlengwa angesema vipengele vichache angepata comment nyingi zaidi.
 
Uchira 1 Soma comment ya chipukizi uelewe nimeandika nini hizo taragram unaoita unga wewe naufahamu sana, sipo hapa kuonesha nachokijua(kwa ufupi najua vingi sana kwenye hii biashara) ila kumtajia makemikal mtu ambae keshasema anataka mtaji usiozidi 40,000 ni kuwa nje ya anachohitaji.
Anyway nadhani ni mtizamo tuu ka mtu anataka kutengeneza icecream kwa mtaji usiozid 40 elfu nadhani ni jambo ambalo haliwezekani, labda hivyo viwe ni kwaajili ya malighafi tu, pia biashara inahitaji uhalisia zaidi.
 
Habarini za muda huu ndugu zangu

Mimi ni ni kijana mwenye umri wa miaka 25, Katika kujikwamua na umasikini na tatizo la ajira Niko na wazo kwa muda mrefu la kuanzisha biashara ya Icecream, nimekuja kwenu kuomba mawazo yenu kwa anaeifahamu biashara hii anipe ufafanuzi kidogo.

Ufafanuzi ninaoomba ni huu;-

i) Changamoto za biashara hii ni zipi
ii) Mtaji wake (malighafi pamoja na mashine vinagharimu kiasi gani)
iii) Kipi kizuri Kati ya kumpa mtu awe anatembeza mtaani kwa kuweka kwenye ndoo kama wanavofanya wengi ama kununua kibaiskeli kama cha Azam
iv) Ili biashara iende ni population ipi niitargert Kati ya wanafunzi wa secondary, primary ama chuoni.
Na mengine niliyosahau unaweza kunisaidia ukawa mzoefu wa hii biashara

Mahali nilipo ni Mwanza , na nimekuja kwenu baada ya kujaribu kufuatilia kwa wanaofanya hii biashara ila ushirikiano wao ulikua ni zero, nilienda pale Salma cone maana ndio sehemu pekee nayoifahamu kwa Mwanza wanaofanya biashara hii.

Nitashukuru Sana kwa atakaenisaidia kwa haya niliyouliza,,. Ahasanteni!!!!!
 
Back
Top Bottom