Mimi nataka kufahamu,bei ya jumla na bei ya rejareja ili nijue faida Kwa Kila mtungi.Madini yapo humu humu boss uliza maswali kuptia thread za kwenye jukwaa la biashara Utapata majibu stahiki utakayoshiba na akili yako.
Umeongea pointi sana!Asee una vitega uchumi halafu wife hakua na biashara unafeli wapi bwasheee,unakubalije bi mkubwa Kadi ya ATM ikose M kadhaaa,ukidondoka paaaa Hatoteseka yeye tu ila na wanao Pia.
Mfungulie Boss usiuweke tena fanya chap chap,hawa wake zetu waliotuletea viumbe ni wakuwawekea mazingira ya hela hadi wazizoeee wakitaka kwenda pelekea viben ten shauri zao,nachojua hawezi kubali mwanangu ateseke.
Hii nayo ni pointiMk
Mkuu CONTROLA Naomba kupatiwa Layout ya ndani ya Duka la Gas,yaan mpangilio wa mitungi,kabati,na shelves kama zipo...ili kuleta muonekano wa kisasa.
Mkuu CONTROLA asante kwa kunirudia japo kwa kuchelewa sana. Hii biashara niliianza lakini kwa small scale,niliweka mitungi ya gas na uwakala wa fedha. Mitungi ya gas imekuwa na faida kidogo sana kiasi kwamba imebidi nifanye evolution ya biashara kwa kuongeza nguo za ndani za wadada khanga na vitenge. Kwa sasa pesa ya gas inatumika tu kupata chakula cha dada w dukani. Mtungi mmoja una faida kiduchu,kupata pesa ndefu ni mpaka uuze mitungi mingi sana. Biashara ipo Mlandizi kibaha.
Uko sahihi mkuu,Gas ni biashara yenye pesa lakini Kama tu utawekeza kwa Ukubwa sana.Mkuu CONTROLA asante kwa kunirudia japo kwa kuchelewa sana. Hii biashara niliianza lakini kwa small scale,niliweka mitungi ya gas na uwakala wa fedha. Mitungi ya gas imekuwa na faida kidogo sana kiasi kwamba imebidi nifanye evolution ya biashara kwa kuongeza nguo za ndani za wadada khanga na vitenge. Kwa sasa pesa ya gas inatumika tu kupata chakula cha dada w dukani. Mtungi mmoja una faida kiduchu,kupata pesa ndefu ni mpaka uuze mitungi mingi sana. Biashara ipo Mlandizi kibaha.
Kitu kingine nilikuja gundua hii biashara gas haina bei,kila mtu anakutajia bei yake ya jumla.Ilifika hatua nilikuwa nafanya window shopping ya bei kwa mawakala naenda ja karatasi naandika,lakini siku ya kuagiza mzigo mtu ananiruka anasema "wewe hiyo bei umetoa wapi mimi siuzi hivyo"?
Kuwa wakala mkuu mtaji kiasi gani?Huwezi kwenda depo (kiwandani) kule wanaenda mawakala Wakuu TU.
Mtaji wa kuwa wakala Mkuu sio wa kuanza kudiscuss hapa, Fanya tu biashara ya gas kwa level hyo hyo uliyopo Mkuu.
Bado faida utaiona vyema wala hutopata stress,Komaa anza na ulichonacho.
Cha muhimu Kuwa makini,wauza gas namaanisha wasambazaji madereva wanaosambaza gas kwa wateja Huwa wanaongeza sana vi buku buku na vijero jero...
Usije ukatajiwa bei yakununua ni 19,000 ukaona ndogo ukawa unatoa hela, wakat huo wenzio mahali wananunua kwa 17,000...
Gas ni biashara hutakiwi kuagiza kwa mtu 1 unatakiwa akili iwe inafanya utafiti kila iitwapo leo, Maana ina madalali wengi sanaa kuanzia kwenye gas yenyewe mpk kwenye Vifaa vyake.
ili uone faida vyema zuia upoteaji wa vile vijero jero na vibuku buku wanavyokuongezea wauzaji wasambazaji.
Ukiuza Gas 22,000
Jirani ako akiuza gas 21,500 nakuhakikishia wewe utamlaumu sana Mungu kwann wateja hawakuoni...
Ofa INAENDELEA upande huu HUKU
View attachment 2176534
Unaweza ukawa na Pesa 1B na usipewe uwakala.Kuwa wakala mkuu mtaji kiasi gani?
Hii comment ni ya mwaka 2022, Mimi nafahidikia nayo Leo kwa kuipitia hapa na kuvuna maarifa. Thank You brotherAmen Kubwa ndugu yangu kiboboso nautamani sana utajiri, naamini kwa baraka hizo alie Juu atanipa tu maana ndio shauku yangu siku 1 kuketi na wafalme wa Dunia hii.
Kusaidia wengi na wanaopta ktk mazingira magumu,najua This word is a better place for everyone, and i will make it real.
if not everyone but atleast anyone around me, To Put a smile kwenye kila sura ya kiumbe kitakachonifahamu CONTROLA .
mkuu nimejifunza jambo kutoka kwako,mimi nataka kuanza kwa mtaji wa milioni 1Biashara ikikubali kakate kibali cha fire 45,000 tu japo vibali vinatoka kwa sqm so idadi ya mitungi yako ndio ita determine wewe kibali chako kiwe cha sh ngapi.
Mwanzo nilifanyaga mafekeche nikawa nimekata kbali kdg tu ila mitungi kibaooo,baadae roho ikanisuta nikaona nikija kuotewa ntaumia basi nimekubali ongeza dau kibali bei ya juu kdg,ila wewe cha 45k ndio size yako.
Kingine Fire extinguisher kwisha habari ukshapata certificate ya fire na hyo fire extinguisher umemaliza Hao fire inpectors wakipta eneo la ofisi yako watapta kwa mbaliii kama hawakuoni.
Kupata Kibali cha Fire ni LAZIMA uwe na leseni ya biashara plus TIN number,imeisha hiyo mkuu.Kapambane.
naomba hii picha tena mkuu kwangu haifunguki