Biashara ya mashine ya kusaga na kukoboa nafaka- Fahamu bei zake, uendeshaji wa biashara hii pamoja na faida na hasara zake

Biashara ya mashine ya kusaga na kukoboa nafaka- Fahamu bei zake, uendeshaji wa biashara hii pamoja na faida na hasara zake

Hii biashara ndio nimeianza naomba mwenye uzoefu wa masoko tuwasiliane ili tuungane.
JPEG_20200927_121348_8440871456439145719.jpg
 
Unga unashida gani kwenye kuuza ndg yangu?nilishawahi kuwa agent wa kiwanda fulani kilichokuwepo maandazi road karibu na veta nakumbuka nilikuwa nauuza kweli kweli
Msosi in general hauwezi kukosa soko. Ishu kubwa ni sehemu ya kuweka bidhaa husika
 
Mkuu mashine ya kusaga na kukoboa sijaagiza kutoka nje. Hii niliinunua kutoka kwa mstaafu mmoja wa Relwe(TRC) mwaka 2010 nikiwa chuo. Nilinunua kinu cha kukoboa na kinu cha kusaga na mota moja niliyoifunga katikati kwa vinu vyote. Mota yangu ni ya 20hp nilinunua kwa sh.700,000.Hivyo vitu vingine nilinunua kwa milion 2 wakat huo.

Kwa sasa niliagiza mashine ya kupima uzito,kujaza na kufunga mifuko(VFFS) kutoka China. Hii ilinicost mil 4.5 mpk kufika Bongo.Hapo ondoa gharama za shipping kwakua nilipakia katika kontena la mtu.

Natumai nimekujibu.
Mkuu, mashine yako ya packaging bado ipo? ni model gani? Nami nahitaji sana ili kufikia mwisho wa mwaka huu nianze kazi.
 
Hii biashara inaonekana ni kimeo, watu wakishaanza wanapotea kimya kimya.
Mkuu, unaposikia neno biashara, jua biashara ni kazi kama kazi zingine na inahitaji dedication na knowledge (kwa kusoma au uzoefu) kama zilivyo biashara zingine.

Biashara yoyote ukiingia kichwa kichwa kwa kusikia story za watu bila kuwa na taarifa sahihi pamoja na self drive/passion inakula kwako.
 
Tunaomba feedback!

Tatizo la JF ni mtu kuanzisha mada ya kuomba msaada halafu baadaye hata hasemi kama alifanikiwa, alikutana na changamoto, au hakuanza kabisa.

Hii tunaiona sana na ikiendelea hivi basi kunakuwa hamna faida ya kupeana ushauri. Wengine tunahamasika pale tunapoona wenzetu wamefanikiwa. Lakini hata pale ambapo mafanikio hayajapatikana, bado kuna kitu cha kujifunza.
Na feedback inaleta matunda sana kwa sisi ambao tuna ndoto za baadae
 
Nimefanya hii biashara kwa miaka kadhaa.Ni biashara nzuri sana.Kinacho 'matter' zaidi ni location.Ukipata location nzuri kwa siku moja unaweza kwenda mpaka units 60,70 na zaidi.Kwa wastani unit moja ni Sh 1350.Uzuri wa hii biashara ni kwamba sio pasua kichwa.Haina usumbufu mwingi wa maintenance.Zaidi sana labda kubadili chekeche,oil na mikanda tena inaweza kuwa mara moja tu kwa mwaka.
 
Nimefanya hii biashara kwa miaka kadhaa.Ni biashara nzuri sana.Kinacho 'matter' zaidi ni location.Ukipata location nzuri kwa siku moja unaweza kwenda mpaka units 60,70 na zaidi.Kwa wastani unit moja ni Sh 1350.Uzuri wa hii biashara ni kwamba sio pasua kichwa.Haina usumbufu mwingi wa maintenance.Zaidi sana labda kubadili chekeche,oil na mikanda tena inaweza kuwa mara moja tu kwa mwaka.
Mkuu, unaposema unit, unamaanisha ni unit za umeme?
 
Biashara nzuri sana hiyo,jamaa yangu kaacha kazi serikalini,anakomaa kuuza unga,anasaga halafu anapaki,aisee anapata hela sana.
 
Pamoja na kutokuwa na uzoefu wa biashara aina hiyo, lakini nimeshuhudia uendeshwaji wa biashara hii nikiwa katika kampuni inafaa sana tu.

Jaribu kubadili kidogo mtazamo na matarajio ya biashara yakio na geukia upande wa pili kwa kujenga dhamira ya kujiamini zaidi ili ufanye makubwa.

Usifikirie watu wakuletee mahindi ili ukoboe na kusaga, ila hilo liwe second target.
  • Kwanza fikiria kuwa na chanzo cha uhakika cha kupata mahindi na ikiwezekana kulima shamba lako mwenyewe na ya kununua iwe nyongeza tu.
  • Pili fungua macho yako kwenye taasisi na vyuo na fanya utafiti utaona wanaweza kuwa soko lako ya uhakika ukiingia mkataba nao
  • Tatu buni packaging ambayo itakuwa labeled na shirika la viwango ili kurudufu ubora wa bidhaa yako unaweza kuwa na soko hata kwenye supermarkets
  • Nne wateja wengine wawe extra income baada ya kujiridhisha kuwa na uhakika wa kuendesha biashara yako hata kama unakuwa na upungufu wa wanaokuja kutumia vinu vyako.
Nikuhakikishie tena jiamini na jenga moyo wa kufanya makubwa, Kama Mungu yuko upande wako hakuna lisilowezekana, ila uwe tayari kuruka vihunzi kabla hujafikia mafanikio.

Penye nia pana njia
Kiongozi, umewahi kufanya biashara na taasisi za kibongo? Unawauzia huduma yako leo, wanakulipa baada ya mwaka mmoja
 
Back
Top Bottom