Biashara ya nguo kwa mtaji wa Tsh. milioni 1

Biashara ya nguo kwa mtaji wa Tsh. milioni 1

Cha kuzingatia uendane na mahitaji ya eneo lako ma wahitaji.....wanachuo unajua wanavyovaa unaweza kuwaletea nguo zote kuanzia za kwendea out hadi za kuvaa lecture room...... watu wazima magauni mazuri pia wananunua....

kwamfano kipindi hiki cha baridi kali unaweza ingiza mzigo wako wa koti za korea, ukawa unazimwaga pembeni ya vituo vikubwa kuanzia saa 10 ukauza kwa bei ya elfu 5 yale mafupi na makubwa ukauza elfu 7 kama umenunua kwa belo haitaziri laki 4 (350) ukiuza kwa bei hizo unapata mchanganyiko utauza sana na faida yake ni kubwa pia....

Pia unaweza ingiza zile pullneck sokoni kwa bei ya elfu 5 zinauzika mbaya.....na uzuri wa hizi bidhaa unaweza kuta wabush huko amekuja town anajumua karibu koti 60 hapo unampunguzia kutoka elfu 5 hadi 4000 ila faida inakuwapo.....

Au kipindi cha baridi unaweza ingiza stock za visocks virefu kwa watoto na wadada watu wazima au ukauza mizura kwa bei ya elfu 3 mmoja kama mizuri utaifurahia biasharaView attachment 1816153View attachment 1816154View attachment 1816156
Mkali hebu tutafutane..mimi nataka vinainai na skin jeans za maana na jamsuit
 
Huu uzi umenifungua pakubwa kwenye sekta ya biashara hii.

Mimi nipo mbali geita mjini huku nauli ya kutoka huku kuja dar ni 45000 kwenda Bado kurudi na matumizi mengineyo.

Kwa watu wa meoneoyaliyo zungukwa na vyuo na wapo katibu na dar hii idea imekaa poa. Mm nataman ila huku hamna hata chuo kimoja
 
Nilichosahau kwenye brouse na masweta kuna sehemu za kuangalia ukiidaka tu, angalia sana kwapani kusiwe kumepauka, angalia shingoni, angalia mikononi kusiwe kumelegea sana pia angalia upindo wa chini upoje

Kwenye skin jeans angalia kiunoni isiwe na kiuno kikuubwa, angalia kwenye msamba kusiwe na msamba mkubwa au uliochakaa, angalia zipu vizuri na angalia chini upindo usiwe umetanuka sana pia isiwe imepauka alafu pia angalia size ya skin zako kuna skin za kuvaliwa na watoto wa secondary, kuna skin za kuvaliwa na chuo ma wadada wakubwa wewe achana na wanafunzi nunua za wanachuo size inaluwa kubwa kiasi na somehow wanavaliana na wadada wakubwa......

alafu angaliaga na rangi isiwe imepauka kwenye skin

Kwenye vipochi kwanza kagua ndani vile vitambaa huwa vimeisha vingine hadi uzuri unapotea, angalia zipu vizuri, angalia mikanda ipo vozuri na angalia chini ya vipochi hata mabegi kama hakujapauka sana ndio ulipie

Pia jua rangi za nguo na rangi za mabegi na vipochi zinazopendwa na wadada.....rngi za nguo zisiwe uniue sana kama purple iwe general tu black, white kiasi, red yellow amd blue ziwe chache ukizunguka sana sio rahisi kukuta mrembo amependeza amevaa yellow japo wapo kwenye vishifon blouse sio mbaya

angalia zile mguo zenye rangi nyingi wewe chukua zinaoendwa sana hata kwa wanaume tshirt zenye rangi nyingi za kuchukua zinauza sana....
 
Mkuu usisubiri vyuo Geita inawageni wengi wengine wanatoka hukohuko Dar
Huu uzi umenifungua pakubwa kwenye sekta ya biashara hii.

Mimi nipo mbali geita mjini huku nauli ya kutoka huku kuja dar ni 45000 kwenda Bado kurudi na matumizi mengineyo.

Kwa watu wa meoneoyaliyo zungukwa na vyuo na wapo katibu na dar hii idea imekaa poa. Mm nataman ila huku hamna hata chuo kimoja
 
Nilichosahau kwenye brouse na masweta kuna sehemu za kuangalia ukiidaka tu, angalia sana kwapani kusiwe kumepauka, angalia shingoni, angalia mikononi kusiwe kumelegea sana pia angalia upindo wa chini upoje

Kwenye skin jeans angalia kiunoni isiwe na kiuno kikuubwa, angalia kwenye msamba kusiwe na msamba mkubwa au uliochakaa, angalia zipu vizuri na angalia chini upindo usiwe umetanuka sana pia isiwe imepauka alafu pia angalia size ya skin zako kuna skin za kuvaliwa na watoto wa secondary, kuna skin za kuvaliwa na chuo ma wadada wakubwa wewe achana na wanafunzi nunua za wanachuo size inaluwa kubwa kiasi na somehow wanavaliana na wadada wakubwa......

alafu angaliaga na rangi isiwe imepauka kwenye skin

Kwenye vipochi kwanza kagua ndani vile vitambaa huwa vimeisha vingine hadi uzuri unapotea, angalia zipu vizuri, angalia mikanda ipo vozuri na angalia chini ya vipochi hata mabegi kama hakujapauka sana ndio ulipie

Pia jua rangi za nguo na rangi za mabegi na vipochi zinazopendwa na wadada.....rngi za nguo zisiwe uniue sana kama purple iwe general tu black, white kiasi, red yellow amd blue ziwe chache ukizunguka sana sio rahisi kukuta mrembo amependeza amevaa yellow japo wapo kwenye vishifon blouse sio mbaya

angalia zile mguo zenye rangi nyingi wewe chukua zinaoendwa sana hata kwa wanaume tshirt zenye rangi nyingi za kuchukua zinauza sana....
Mkuu wewe hii kazi Ndio yako huko ulikoajiriwa unapoteza muda LOL
 
Sorry for late reply.....za dukani utapata ila utapata mzigo mdogo...... Za mtumba zinauzika sana hasa za kina dada tena unaweza anza na za mtumba za laki 3 tu alafu laki 3 nyingine wekea viati vya kina dada.....vingi vinauzika kwa elfu 5 yani kariakoo unanunua 2500 unakuja uza 5000......

Laki 4 ibaki pembeni kama akiba na nguo ufanye pointing kuliko kununua belo, sehemu za kufanyia pointing kwa dar ni ilalaboma na karume huko nguvu yako ya kuchagua ndio itafanya upate nguo nzuri kwa bei ya kuanzia 1000 - 4000 kwa ilalaboma kama ukiwahi alfajiri....

Utaratibu wa kupata meza, unategemeana na mkoa, ila sehemu nyingi ni nguvu ya kuwahi na kujuana na majirani zako kibiashara na tozo wanalipa 2000 kwa siku hiyo ni Moro.....kwa iringa huku ni bure kabisa kwa machinga......

Ukiwa smart utatoka mapema, kupitia nguo zakike na viatu kulaza 50 itakuwa kawaida na ninauhakika katika hili....

nimekushauri upoint ili usipate maronya mengi pia uzoee deals zinaendaje ili ukizoeana na unaeona anapata mabelo mazuri na muaminifu akushike mkono ..... Changamoto zipo ila zinasolvika na ni ndogondogo sana.....

Mfano kipindi cha baridi hiki mikoako ukipeleka trench coats almaarufu kama koti za kikorea utauza sana kwa bei ya 5000 na zile ndefu mzuri 7000 hadi 8000.....
Hizo koti bei za jumla ni ngapi mkuu

Na viatu bei ya jumla havipo chini ya 2500??/nahitaj
 
Habari za humu ndani ndugu zangu.

Katika hali ya kuchakarika na kutafuta maisha hatimaye leo nimekuja na wazo langu ambalo nahitaji msaada toka kwenu wadau au kama kuna wazo zuri zaidi ya hili unaweza pia nishauri.

Nilikuwa na wazo la kufanya biashara ya nguo za wadada na watoto, kwa mzoefu au mwenye uono zaidi. Je mtaji wa Tsh. milioni 1 unatosha? Kama unatosha nini kifanyike hadi kufikia step ya kuweka mzigo sokoni?

Location niliiona iwe Mbagala Rangi 3 (ila Rangi 3 na huu ujenzi wa barabara panachangamoto sana) au hata K\Koo.

NAOMBA KUWASILISHA[emoji1666]
Moja kati ya uzi bora kabisa JF, ngoja waje wakuu wenye uzoefu wakupe vision iliyotulia....
 
Watu hawajaja hapa kwa kuwa nawe si mchangiaji.
ID yako ya 2015 lakin unaonekana c wa kujichanganya.

Hata nyuzi zako zina wachangiaji wachache sana.

Tembelea nyuzi zinazohusu biashara.
Ulichoandika tayari kishajadiliwa sana.
Ivoo tenaa
 
very thanks brother... much respect. ahsante sana... umenipa mwanga angavu sana. Ubarikiwe sana.. [emoji1666][emoji1666]
Hana shida kaka, ukipata jeans au tshirt kali za mtumba ni sw ma za dukani hiyo ni kwa wkiume, wakike ukipata gauni, shiffon blouse, skin za kutosha unaweza koti frame kwa mil 1 na mzigp ukawa umejaa na chini unapanga visendo vya wadada wanavyonunua nguo na sendo wanachagua utafika mbali
 
Back
Top Bottom