Biashara ya nguo kwa mtaji wa Tsh. milioni 1

Hizo koti bei za jumla ni ngapi mkuu

Na viatu bei ya jumla havipo chini ya 2500??/nahitaj
Koti za korea au trench coats naona bei zinatofautianakwa wauzaji ila 350 kwa belo uhakika..... Nachalufanya ni kwenda kw wachina direct (sina uhakika kama ni upanga au wapi yalipo maduka ya wachina wanaouza mabelo ya mtumba) utaweza pata mzigo mzuri .....

Ila kuna aliekuwa anauzia huku iringa alinichoresha ramani amenunua laki 250 tu na sio 350 kama nilivyoulizia kwa wauzaji......

Viatu ninavyozungumzia ni vya dukani zile sendo zote za kike bei nrio hizo za 1500, 2500 wamauza 5000 za 3000 na 4000 utauza 8000 biashara yao ipo hivyo na nauhakika sababu kuna wadogo zangu wanafanya ya viatu..... Tena biashara ya viatu vya kike inafaida maana faida ni nusu ya mtaji kama mtaji ni 200000 basi faida ni 400000 kwa sababu kwemye kuuza unadouble pesa na faida inarudi.
 
Mkuu mtu akikuomba umuagizje mzigo utakuwa na nafasi..sie wengin tupo mikoan
Mkuu nisiseme uongo, kwasasa haiwezekani kwakuwa huwa nakuwa mkoani pia......labda kwa mwezi wa 12 tarehe za mwanzo nitapoenda fuata mzigo wangu wa biashara nyingine.....napo itabidi tukubaliane nguo unazotaka kwa detail nzuri na tushauriane kwa experience yangu na wengine nguo zinazotoka haraka.....so kwa sahizi haitawezekana mkuu ila ukitaka naweza kupa detail zote tu za hizo chimbo labda niongeze na chimbo ya viatu vya kike kwa bei ya 2500 hadi 4000 kwa jumla
 
Msaada namba za hao jamaa wanaouza izo sendo za 2500 pale k.koo
Mkuu namba zao sina na nashauri sana kama ungeweza fika mwenyewe kariakoo underground uchague kwa macho yako......maana unaweza pata namba ya machinga wa nje akakupiga kwa kukutajia bei kubwa, pia ni vizuri kuwepo ili wasikuchanganyie na visendo old fashion yani upate mzigo mpya mpya na fashion za sendo za kisasa......mwanzoni kama mara 5 fuata mzigo mwenyewe baada ya hapo unaweza agiza kama utakuwa umezoeana na wauzaji
 
Asante mkuu kila la kheri katika biashara yako
 
hahahahaaaaaaaa bestito mbona kwenye mada zangu kule mmu ulikuwa mstariwambele
 
Kama mtaji wa 1ml ndo hapo hapo na kodi ya pango au ushatoa kodi ndo inabaki hiyo milion moja.

Kingine location nakushauri iwe nje ya k,koo according to your capital

Nakutakia kila la kheri mkuu
 
yaah kuna jamaa alichanganua biashara ya viatu humu jf nikamwelewa sana

nimejaribu kutuma mzigo mkoani naelekea mara ya tatu sasa faida yake ni visible kuliko kwenye nguo
 

Bushmamy Tupe madini hapa kuhusu hii bizne$$.
 
yaah kuna jamaa alichanganua biashara ya viatu humu jf nikamwelewa sana

nimejaribu kutuma mzigo mkoani naelekea mara ya tatu sasa faida yake ni visible kuliko kwenye nguo
Shukrani kwa kuongezea ni kweli japo inachosha sana kutafuta viatu latest na vinavyopendwa inahitji juhudi ila pesa ipo
 
Mmh unachokaje wakati ukienda pale kwa mchina unakutana na viatu vipya
Pia unafollow page za wauzaji viatu maarufu unaona vinavyptrend
kufuata mzigo toka mbalu ni shida in nimeshauri hapo kuwa mtu akionesha userious hata wauzaji wanakuw wepesi kukutumia mzigo ten mzuri
 
Mbona Sikuona Mkuu! Very sorry
Mkuu nimeshaanza biashara maeneo ya mbagala ila nimekutana na hali halisi ya mbagala..wateja wanataka chupi za buku na hawaangalii quality..na pia wanapenda chupi za mtumba..mimi nimekuja na chupi chambuu mana ndio zinafaida..lonya ya kuuza buku faida yake ni 3000 mpaka 2000 per dozen wakati chambuu ya 15000 inaweza kukupa 9000 mpaka 15000 kama faida kwa dozen moja.. sasa nikikaa golini kwa siku mauzo yanakuja 30000 mpaka 50000 per day wakati nikitembeza per day napata 90000 mpaka 120000 per day.. sasa shida ni jinsi ntakavyoweza kuongeza mauzo pale goloni..naomba mbinu



























































 
Umekuja na msamiati Mpya Chambuu kwenye Chupi ndo zipoje na zinapatikana wapi.?

Ili kuongeza mauzo dukani kwako ni kuleta bidhaa wanazozitaka kulingana na soko lako Mkuu

Hongera kwa kuthubutu nikija mjini nitakutembelea ofcn kwako 😉
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…