ngoja namimi nichangie huenda nikapata baraka pindi ukipata faida na ukapeleka fungu la kumi kwenye ibada,ila usisahau kuniombea niwe Kama mo dewji, fanya hizi kuteka soko, hapo mtaani watafute wadada wawili, mashangingi ya mtaani, yanaongee Sana,yakupigie promo kwa mtaani hapo, wape ahadi kuwa utasukwa buree,kila mwezi aje na Rasta zake tu. njia ya pili, kila panapokuwa na rusha roho,kigoma,beseni, mwali anatoka, ndoa, naupuuzi unaendana na huo,nenda kwa DJ, mpe buku tano tu,mwabie nipigie promo mwanzo mwisho, atatangaza kila mda juu ya salloon yako na ubora wako, njia ya tatu, mtafute mkongo wa kiume mweke awe msaidizi wako, njia nne, mtafute muha kutoka kigoma awe anapaka rangi huku unamlipa kwa mwezi, endapo mteja akija kusuka Rasta, basi mpe offer ya kupaka rangi mikono au miguu, mteja akija kuweka dawa,mpe offer ya kupaka mkono mmoja rangi.....naamini utapata wateja wengi tuu,mpaka utawakimbia....kumbuka ukufanikiwa nenda katoe fungu la kumi,huku ukiniombea Mimi niwe Kama MO WA SIMBA, ukigeuka agano hili la kutotoa fungu la kumi, utarudi kwenye zero.wasalaam wape salaaam MORSON KASIGN SIMBA