Biashara ya samaki

Mambo vi
Pi!? Una mawasiliano na wenye magari ya refrigerator!?
 
Naombeni mifano ya watu waliotajirika kwa kumiliki Mabucha
 
Team Watafutaji
Kama title inavyosema hapo juu, naomba kufahamu hii biashara kwa undani kidogo, yaani recently tuliambiwa kuwa kwa kipindi hiki cha miaka mitano samaki wetu wameongezeka urefu/ukubwa.

Sasa basi nikawa interested kufahamu kama mtu anaweza kununua samaki (Sato/Sangara) kutoka kwa Wavuvi in bulk na kuziuza kwa makampuni ambayo tumeambiwa wanasafirisha kwenda nje ya nchi moja kwa moja.

Au kuanza kuvua na kuuza moja kwa moja kwa haya makampuni badala ya kununua kama middleman.

Moja, je ni changamoto gani kubwa zipo kwenye hii sekta?

Pili, upatikanaji wa vibali ukoje!?

Tatu, je hivi viwanda vinanunua hao samaki kwa mfumo gani? Cash on delivery au on credit?

Nne, je mtu anaweza kuingia mkataba na hivi viwanda ili kuwa-supply mzigo?

Tano, ni fursa gani (fursa ndani ya fursa) zinaweza kupatikana kwenye hii biashara?

Sita, modality yao (kama ipo), ipoje? Je wanaweza kukudhamini vifaa ili mzigo uwapelekee wao na kukatana kidogo kidogo?

Saba, ni viwanda (kwa majina) vipo kati ya Mwanza, Bukoba na Musoma au around maeneo hayo ambao wanaweza kupokea mzigo?

Nane, je upatikanaji wa samaki una msimu? High season na low seasons?

Maswali yangu hayajakaa kwa mtiririko maalum hivyo tusaidiane tu kadiri tutakavyoona inafaa.

Kwa hili tutaweza kusaidiana na kuwasaidia vijana wetu/wenzetu pia
 
Cha kwanza kazi inayowezekana ni kuvua mwenyewe ukisema kulangua utaumia sababu watu wa siku hizi iwe wavuvi,wafugaji au wakulima hawakubali dalali au mchuuzi ale kirahisi tuu

Cha pili itakubidi uingie front mwenyewe na sio kutegemea kutuma vijana wakavue ukadhani utafanikiwa, kama utawatuma watakuzunguka hizo samaki watauzia huko huko ziwani na zana kama nyavu watauza wakisingizia zimeibwa

Kalaghabaho

Way forward to this business ingia mwenyewe , nunua boti ya kisasa bei ipo kwenye milioni 60 au 70 kwenda juu boti yenye horsepower za kutosha na injini kuanzia mbili kuendelea ili kama injini moja ikisumbua majini una washa ya backup
 
hakuna biashara inalipa kama ya samaki! hakuna biashara inakata mtaji kama samaki me naifanya nanunua nyumba ya Mungu nauza Moshi/Arusha
Mimi nimeifanya sana pale moshi mjiniii aisee achaa.

Ukiwa na wateja wa huakikaa utafurahii
 
hakuna biashara inalipa kama ya samaki! hakuna biashara inakata mtaji kama samaki me naifanya nanunua nyumba ya Mungu nauza Moshi/Arusha
Mkuu naomba unipe muongozo namaliza mwezi ujao niko Moshi hapa sina A, B, C kuhusu hii biashara nahitaji mentor wa kuniongoza na kunishika mkono kunionyesha masoko na sehemu wanapochukulia..
 
Mkuu naomba unipe muongozo namaliza mwezi ujao niko Moshi hapa sina A, B, C kuhusu hii biashara nahitaji mentor wa kuniongoza na kunishika mkono kunionyesha masoko na sehemu wanapochukulia..
Samaki wa bwawa la nyumba ya mungu wana sinyaa sana akikwekwa kwenye freezer. Ukipata walio vuliwaa fresh ila wakikaa kwenye deep freezer ni hatarii
 
Dah kudaadeki yaani vile viboti vinauzwa milioni 70.
Wakati milioni 70 nina uwezo wa kutengeneza lodge nikakaa tu mlangoni kusubiria wateja au nina uwezo wa kufungua maduka mawili ya hardware badala ya kununua boti halafu nikakeshe kwenye maji.
 
Habari wakuu natumai muwazima hapa. Nahitaji ndugu anayeleta Samaki kutoka nyumba ya Mungu
 
Broo mbona unakatisha watu tamaa Mimi nimeanza na mtaji wa shilling 160000 nimeanza kuuzia samaki kwenye deli ila kwa sasa Nina bucha ya samaki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…