richie ze best
JF-Expert Member
- Nov 4, 2013
- 600
- 1,023
Wakuu kwema?
Niende kwenye mada chap chap...
Mimi ni muajiriwa wa sekta binafsi,kazi yangu inakula mda wangu wote,sipati nafasi ya kusimamia ama kuendesha biashara zingine.
Ila nina hobby ya kupiga picha ni kitu napenda toka utotoni,nikaona ili kuhiendeleza nikasoma mitandaoni na hasa YouTube, naweza kujiita ni mpiga picha mzuri kwa mpaka nilipofikia na najua vitu vingi kupitia tasnia ya upigaji picha.
Nimeamua kujinunulia vifaa vya kupiga picha kama camera,lens,lighting na n.k...
Inanisaidia kwa maana kazi yangu kwa namna flani inaniwezesha kudaka wateja na wakati mwingine napiga kazi ya kampuni ama kukiwa na mteja wao wana mdirect kwangu japo wananikata 18%+5% ya ninachopata si haba.
Ila nafasi ya kufanya hiyo kazi ni kwa mbinde..
MADA KUU.
Nimefungua Stationary miezi sita iliyopita.
Nikaweka printer,computer,lamination mashine n.k,camera kwa ajili ya pasport size na baadae vitambaa vya kupigia picha na stand yake,pia niliongezea na line za uwakala,ila mpaka sasa hazijaanza kufanya miamala,sio ofisi kubwa.
Kimbembe kikaja kupata mfanyakazi,
Huku na huku nikapata binti niliyeunganishwa na rafiki yangu.
Tukakubaliana afanye kazi nitampa nauli na kula ili angalie biashara kwa mwezi mmoja then tukubaliane malipo.
Kweli alianza kukaa hapo nikampa na madaftari matatu la manunuzi,matumizi na madeni na mauzo..
Nikipata nafasi mara moja kwa week napitia mahesabu,si haba kwa mwezi unaweza kuta una laki 3.
Mwezi ukakata ujauliza mshahara na hatimaye miezi minne,binti haulizi pesa...nikaisi kuna kitu hakiko sawa.
Kwenye geti la Stationary kuna namba zangu,nikawa napokea simu nyingi nyakati za kazi wateja wanahitaj huduma na duka limefungwa,pia nimepata lawama nyingi za leo bei ya kuprint iko juu kesho iko chini...
Sikutaka kumuhoji sana sababu hata nikimtoa sina wa kuisimamia hiyo biashara...
Kimbembe kilianza siku nilipeleka karatasi za passport katika mahesabu nikakuta 22 hazipo na zilizobaki kuna mauzo ya 19 baada ya kukagua kwenye daftar,kuhoji binti akawa hana maelezo ya kueleweka zaidi ya kusema karatasi 22 zimearibika ndani ya week.
Sikumuhoji sana wala sikumkaripia,ikabidi nianze kufatilia mahesabu kwa karibu sana hata nikitoka usiku naenda kukagua...
Alipoona hivyo akasema anaumwa na hajarudi mpaka leo.
Biashara imefungwa kwa sasa.
Sasa nimekuja hapa natafuta kijana ambaye anaweza kubeba ownership, akaibeba kama yake,ikiwezekana malipo tulipane kwa asilimia,awe mwaminifu na anaweza kujisimamia,awe na taaluma ya Stationary.
Kupiga picha na passport nitamfundisha ila kama anajua itakua poa zaidi..
Pili nataka kujua ni vitu gani kuacha nilivyonavyo ninaweza kuongezea na vinatoka ki urahisi ili nimwekee mtaji wa kutosha.
Kama akiwa mwaminifu sitahitaji kumfatilia na tukifikia pazuri faida mimi na yeye tugawane 50/50 mana sina mda wa kufatilia.
Tuvumiliane kwa uandishi wangu mbovu.
Niende kwenye mada chap chap...
Mimi ni muajiriwa wa sekta binafsi,kazi yangu inakula mda wangu wote,sipati nafasi ya kusimamia ama kuendesha biashara zingine.
Ila nina hobby ya kupiga picha ni kitu napenda toka utotoni,nikaona ili kuhiendeleza nikasoma mitandaoni na hasa YouTube, naweza kujiita ni mpiga picha mzuri kwa mpaka nilipofikia na najua vitu vingi kupitia tasnia ya upigaji picha.
Nimeamua kujinunulia vifaa vya kupiga picha kama camera,lens,lighting na n.k...
Inanisaidia kwa maana kazi yangu kwa namna flani inaniwezesha kudaka wateja na wakati mwingine napiga kazi ya kampuni ama kukiwa na mteja wao wana mdirect kwangu japo wananikata 18%+5% ya ninachopata si haba.
Ila nafasi ya kufanya hiyo kazi ni kwa mbinde..
MADA KUU.
Nimefungua Stationary miezi sita iliyopita.
Nikaweka printer,computer,lamination mashine n.k,camera kwa ajili ya pasport size na baadae vitambaa vya kupigia picha na stand yake,pia niliongezea na line za uwakala,ila mpaka sasa hazijaanza kufanya miamala,sio ofisi kubwa.
Kimbembe kikaja kupata mfanyakazi,
Huku na huku nikapata binti niliyeunganishwa na rafiki yangu.
Tukakubaliana afanye kazi nitampa nauli na kula ili angalie biashara kwa mwezi mmoja then tukubaliane malipo.
Kweli alianza kukaa hapo nikampa na madaftari matatu la manunuzi,matumizi na madeni na mauzo..
Nikipata nafasi mara moja kwa week napitia mahesabu,si haba kwa mwezi unaweza kuta una laki 3.
Mwezi ukakata ujauliza mshahara na hatimaye miezi minne,binti haulizi pesa...nikaisi kuna kitu hakiko sawa.
Kwenye geti la Stationary kuna namba zangu,nikawa napokea simu nyingi nyakati za kazi wateja wanahitaj huduma na duka limefungwa,pia nimepata lawama nyingi za leo bei ya kuprint iko juu kesho iko chini...
Sikutaka kumuhoji sana sababu hata nikimtoa sina wa kuisimamia hiyo biashara...
Kimbembe kilianza siku nilipeleka karatasi za passport katika mahesabu nikakuta 22 hazipo na zilizobaki kuna mauzo ya 19 baada ya kukagua kwenye daftar,kuhoji binti akawa hana maelezo ya kueleweka zaidi ya kusema karatasi 22 zimearibika ndani ya week.
Sikumuhoji sana wala sikumkaripia,ikabidi nianze kufatilia mahesabu kwa karibu sana hata nikitoka usiku naenda kukagua...
Alipoona hivyo akasema anaumwa na hajarudi mpaka leo.
Biashara imefungwa kwa sasa.
Sasa nimekuja hapa natafuta kijana ambaye anaweza kubeba ownership, akaibeba kama yake,ikiwezekana malipo tulipane kwa asilimia,awe mwaminifu na anaweza kujisimamia,awe na taaluma ya Stationary.
Kupiga picha na passport nitamfundisha ila kama anajua itakua poa zaidi..
Pili nataka kujua ni vitu gani kuacha nilivyonavyo ninaweza kuongezea na vinatoka ki urahisi ili nimwekee mtaji wa kutosha.
Kama akiwa mwaminifu sitahitaji kumfatilia na tukifikia pazuri faida mimi na yeye tugawane 50/50 mana sina mda wa kufatilia.
Tuvumiliane kwa uandishi wangu mbovu.