Biashara ya Sungura imejaa utapeli wa hali ya juu sana

Biashara ya Sungura imejaa utapeli wa hali ya juu sana

Nyama ipo bomba tu haina shombo fresh kwa mpishi yote hasa kuchoma na haina tofauti sana na yakuku
Hio ndio safi ukiwafuga kama hobby tu,mimi siwezi kula Sungura.

Sent using Jamii Forums mobile app
IMG-20191231-WA0010.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Haaa angalia usije ingizwa Mkenge, Hao unao wafuatilia wangekuwa wanafaidika nao huo mkojo wangefanya kimya kimya. Nani ahangaike na Mkojo wakati kuna Organi fertilizer Madukani tena quality?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu huu mkojo hata maduka ya kilimo hai unauzwa sana kwasasa. Wataalamu wangu wa kilimo hai wamenishauri niutumie na umeleta mbadiliko ya haraka sana shambani. Usiwe na hofu fuatilia mtandaoni utaujua zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka huku kwetu Iringa watu walilimishwa "Paprika" aina fulani hivi ya Pilipili mwisho wa siku hata leo hii ukiwakumbusha wanabaki kucheka tu. Mambo ya kupanda miti ya mlonge yalichukua hela za watu wengi sana.

Sijui ni kwa nini watu huwa hawaulizi mambo ya msingi kabla ya kushiriki kwenye kujitapeli.
Sisi ni risk taker tuache

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Biashara zooote za wanyama wadogo kama kuku bata mende sungura ni mkakati wa kitapeli kuwavuta wengi waingie ili inspirational speakers wapate hela, wauza vyakula na madawa wa wanyama hawa wapate hela mengine wanakuachia wewe mwisho wa siku kama utabahatika utakuwa na wingi wa hao wanyama lakini huna pa kuuzia kurudisha hela. heti: kilo moja ya mende China ni laki tano??? Jamani muogopeni Mungu. Sasa ingia mkenge uanze kufuga hao mende utauziwa mende mmoja wa mbegu 15,000 nautaambiwa unatakiwa uanze na mende 10 kwa kiasi cha 150,000. Hiyo semina ya jinsi ya kufuga mende unalipia kiingilio kwa mtu ni 50,000 wakipatikana 20 inspirational speakers kaishaula. Utauziwa chakula special cha mende kilo 35,000 na utaambiwa mpaka wakue unatakiwa ununue kilo 10. Utaambiwa ununue madawa ya kufanya wazaliane, kuwakuza na kuwafanya wawe na uzito, n.k. Amaaa kweli nyakati hizi za mwisho watu wanapigwa na kubaki mafukara wa kutupwa
Hao mende ndio wanyama gani, ama ndio hawa hawa wa chooni???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umefanya utafiti ukagundua siyo dili? Naona hii thread imejaa post zenye negativity na hisia hisia tu. Ni kweli makampuni ya Kenya yalikuja kuamsha ufugaji wa sungura kisha yakapotea. Kwa mtu mwenye "mentality" ya kijasiriamali badala ya kubaki kulia lia kuhusu soko atakomaa alitengeze la kwake.

Naona majukwaa ya ujasiriamali hapa JF siku hizi yametawaliwa na comments kutoka kwa watu ambao ni dhahili kuwa hakuna kitu cha "uzalishaji" wamewahi kamilisha.

Mfano ni hii post ambayo mtumaji anadai mkojo wa sungura siyo dili. Very stupid. Mimi nafanya bustani na hutumia mkojo wa sungura kutoka kwa jirani yangu kama dawa ya kuua wadudu na mbolea simultaneously. Sasa unajiuliza, huyo anayedai siyo dili amefanya jitihada gani kuli-trap soko la wakulima?

Tatizo la mfumo wetu wa kubadilishana maarifa (elimu) haujikiti kwenye masuala (masomo) yanayotuzunguka kama vile ujasiriamali. Badala yake hutumia muda mwingi kukaririshana mambo ambayo yangekuwa ya ziada tu.

Matokeo yake ni waTz wengi kutokuwa na haiba za kijasiriamali kama wenzetu waKenya.
Pia wanawadanganya mkojo wa Sungura deal!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kabisa kiongozi.
Nimefuatilia sana kenya nikapata taarifa sahihi kwasababu wataalamu wetu kila ninapouliza nilikosa majibu yakueleweka. Hapa ni kweli kama unafanya kilimo hai au organic, una N,P na K ya kutosha sana na unaweza kuspray kwenye mmea wenye shida kuua wadudu. Ni nzuri sana kwa wanaofanya kilimo cha mbogamboga, ni soil conditioner na rafiki mzuri sana wa udongo ila
Ukibugi kwenye uchanganyaji unaua mmea jumla

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakwere wana msemo wao kwamba jambo la kuambiwa changanya na za kwako!!
Umefanya utafiti ukagundua siyo dili? Naona hii thread imejaa post zenye negativity na hisia hisia tu. Ni kweli makampuni ya Kenya yalikuja kuamsha ufugaji wa sungura kisha yakapotea. Kwa mtu mwenye "mentality" ya kijasiriamali badala ya kubaki kulia lia kuhusu soko atakomaa alitengeze la kwake.

Naona majukwaa ya ujasiriamali hapa JF siku hizi yametawaliwa na comments kutoka kwa watu ambao ni dhahili kuwa hakuna kitu cha "uzalishaji" wamewahi kamilisha.

Mfano ni hii post ambayo mtumaji anadai mkojo wa sungura siyo dili. Very stupid. Mimi nafanya bustani na hutumia mkojo wa sungura kutoka kwa jirani yangu kama dawa ya kuua wadudu na mbolea simultaneously. Sasa unajiuliza, huyo anayedai siyo dili amefanya jitihada gani kuli-trap soko la wakulima?

Tatizo la mfumo wetu wa kubadilishana maarifa (elimu) haujikiti kwenye masuala (masomo) yanayotuzunguka kama vile ujasiriamali. Badala yake hutumia muda mwingi kukaririshana mambo ambayo yangekuwa ya ziada tu.

Matokeo yake ni waTz wengi kutokuwa na haiba za kijasiriamali kama wenzetu waKenya.

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeongea maneno ya msingi sana mkuu binafsi nakuunga mkono. Wengi wamejawa na mawazo potof dhid ya sungura. Ndio maana wanaongea visivyo na ushahid

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa Sungura walipofika 50 ndipo kiswahili toka kwa ile kampuni iliyomuuzia sungura kwa ahadi ya kutafuta soko kilipoanza. Mpaka wanafika 200 hakuna soko na Kampuni ikawa imeshafunga shughuli zake hapa Iringa na kumwachia mzigo wa kuwasiliana na wafugaji wenzake mama mmoja ambaye naye walishamtapeli .
Mkuu nipe namba yake pm mimi ni mlaji sana wa nyama ya sungura na njiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa Sungura walipofika 50 ndipo kiswahili toka kwa ile kampuni iliyomuuzia sungura kwa ahadi ya kutafuta soko kilipoanza. Mpaka wanafika 200 hakuna soko na Kampuni ikawa imeshafunga shughuli zake hapa Iringa na kumwachia mzigo wa kuwasiliana na wafugaji wenzake mama mmoja ambaye naye walishamtapeli .
Awale nyama.. mwaka mzima kila siku mboga sungura😂😂
 
Unachanganya vip kiongozi, na je unapiga kwenye mimea baada ya muda gani

Sent using Jamii Forums mobile app
1. Kwenye maharage.. Kwa wiki Mara moja
2. Kwenye miti ya matunda... Kwa mwezi Mara moja.

Lita 1 ya mkojo kwa Lita 3 mpaka 5 za maji.

Kama ni dawa 1:3 mkojo:maji
Kama mbolea 1:5 mkojo:maji

Inategemea na kipindi.

Kama kipindi cha wadudu wengi ndio 1:3 ili harufu ya mkojo (ammonia) inuke shambani ili wadudu wakimbie.

Ila kwa kua nishapiga sanaa then nimestick na ratio ya 1:5

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi nimfugaji wa sungura toka 2013 hadi leo mim nafuga tu kwa 7bu.

Nawapenda kuwaona kula pia uwa nauza mim nafuga tu kienyeji ila wananikomboa vitu vidogodogo cja waikupata changamoto kihivyo eti soko hakuna mala njoo semina mim nilienda polini nikawinda hadi leo hii mim ninao na nauza bilashaka sas cjajua tatizo nin wanazengwe

Sent using Jamii Forums mobile app
Aisee unafuga sungura pori!
 
Kinadharia ufugaji wa sungura kibiashara ni jambo lenye kuleta matumaini sana, lakini kiuhalisia ni biashara yenye utata mkubwa sana kwa hapa kwetu Tanzania.

Makampuni mengi yanayohamasisha ufugaji wa Sungura ni kama yale makampuni ya uuzaji bidhaa kimnyororo (Supply Chain companies) ambako faida inapatikana kwa kuongeza washiriki kwenye biashara husika.

Unapoingia kwenye ufugaji wa kibiashara wa sungura, Makampuni mengi yaliyoko hukuuzia sungura wa kuanzishia mradi, kukujengea banda, kukuuzia chakula cha sungura mengineyo utajijua mwenyewe, kwani ahadi nyingi za kutafutiwa soko la sungura huwa ni UONGO WA KUPINDUKIA ULIOPANGILIWA KIAKILI SANA.

Nadhani wale wanaotaka kufuga sungura kibiashara wajaribu wenyewe kwanza kutengeneza soko la nyama ya sungura kabla ya kufuga sungura hao kwa wingi.

Watanzania tupimwe kama tu wazima, hao ni wafanya biashara wa:

- sungura wa mengi!
- Mabanda ya sungura
- chakula cha sungura

Kama pangekuwa na Soko la sungura, wana utalaam, wana mbegu na mabanda, Kwa ninj wao wasiwakuze wauze? Kutapeliwa kwingine kwa kweli ni aibu, tuwe na akili eti!
 
Biashara zooote za wanyama wadogo kama kuku bata mende sungura ni mkakati wa kitapeli kuwavuta wengi waingie ili inspirational speakers wapate hela, wauza vyakula na madawa wa wanyama hawa wapate hela mengine wanakuachia wewe mwisho wa siku kama utabahatika utakuwa na wingi wa hao wanyama lakini huna pa kuuzia kurudisha hela.

Heti: kilo moja ya mende China ni laki tano??? Jamani muogopeni Mungu. Sasa ingia mkenge uanze kufuga hao mende utauziwa mende mmoja wa mbegu 15,000 nautaambiwa unatakiwa uanze na mende 10 kwa kiasi cha 150,000.

Hiyo semina ya jinsi ya kufuga mende unalipia kiingilio kwa mtu ni 50,000 wakipatikana 20 inspirational speakers kaishaula. Utauziwa chakula special cha mende kilo 35,000 na utaambiwa mpaka wakue unatakiwa ununue kilo 10. Utaambiwa ununue madawa ya kufanya wazaliane, kuwakuza na kuwafanya wawe na uzito, n.k. Amaaa kweli nyakati hizi za mwisho watu wanapigwa na kubaki mafukara wa kutupwa
haha asantee
 
Back
Top Bottom