Biashara ya tution center italipa sana kuanzia 2016

NYINGWA

Member
Joined
Nov 29, 2015
Posts
55
Reaction score
27
Kutokana na suala la elimu bure na inaonekana kqbisa kwamba elimu yetu hasa kwa shule za serikali itakuwa chini hivyo wanafunzi watahitaji masomo ya ziada kwa kasi ya ajabu ili kujiinua darasani.

Hivyo kama nyinyi ni walimu, mnaweza mkajiunga na kutafuta eneo ambalo mnaweza mkafungua kituo kwa ajili ya kutoa huduma hiyo kwa maana ya kusaidia jamii na kujipatia kipato cha ziada.

Mimi tayari nimetoka kulipia leo kesho natafuta fundi kwa ajili ya madawati na kutengeneza mbao za kuandikia.

Jaribuni walimu wenzangu.
 

nalipa mia...kwa kuliona hiloo
 
Serious, hata kama siyo mwalimu unaweza wewe ukaratibu na ukaajiri walimu kufanya kazi hiyo. Must be walimu wenye weredi.
Lets say sisi ni walimu, tupo watatu ni kama kiasi gani cha pesa kinaweza kikakidhi?
 
JIPE MOYO TU:
kwa sasa elimu imeshuka sana, wazazi hawana mwamko wa elimu, wanafunzi ndo wamekata tamaa, walimu ndo usiseme,
TUISHE ILIKUWA MIAKA KUMI ILOPITA WANAFUNZI WALIKUWA WANAKIMBILIA WENYEWE
=> KWA SASA ANZISHA TUITION YA BURE HAWAJI HAWATAKI KABISA
=> HAPA MKURANGA KUNA TAASISI YA KIISILAM IMEANZISHA TUITION BUREEEEE CHA KUSIKITISHA WANAFUNZI HAKUNA ANAYEENDA
 

Mkuranga na alipo mtoa mada panalingana?
Pia Kuna tatizo la dini hapo, linaweza kuwa limechangia. Maeneo ya miji iliyochangamka tuition ina soko zuri tu
 

Hii kali sasa.ila kiukweli enzi zetu,mapindi ndio yalikuwa ndio mpango mzima.
 
Haaaa! We unazungumzia mkoa wa pwani!!! Ongelea sehemu ambazo watu wanatamani shule, sasa mkuu unazungumzia wazaramo hao na shule wapi na wapi?
 
Lets say sisi ni walimu, tupo watatu ni kama kiasi gani cha pesa kinaweza kikakidhi?

Inategemea vitu vifuatavyo:
1. Nyinyi walimu watatu mliojioganise mnafundisha masomo gani. Mnaweza jikuta wote mnafundisha kiswahili, hivyo lazima muajiri walimu wengine wa ziada.
2. Pia eneo ambalo mmepata lipo tayari kiasi gani kwa mradi nazungumzia miundo mbinu ya darasa na samani ya ndani ya darasa
3. Makubaliano yenu na mwenye jengo kimalipo au jengo ni la kwenu.
Jambo la msingi jitahidini eneo liwe center kati ya shule na shule
 
Mkuu mkoa wa Pwani hauna muamko kielimu acha mtoa mada ajaribu aliko huenda kuna fursa
 

Uko mji gani Nyingwa? Nina cousin wangu Mwanza ambae anaweza kukuunga mkono.
 
nimeshawahi kumlipa mwalimu tution sh laki moja kwa mwezi kwa Mirza sita nyakahoja pr school
 
Baada ya muda watu watazipiga marufuku,au kuzipangia kodi maalum.

Maana ni sawa na Daktari ukienda hospitali anakuambia uende kwenye Dispensary yake au Pharmacy yake ukanunue dawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…