Biashara ya Usafirishaji kwa Bajaji: Ueandeshaji, Changamoto, Faida na Ushauri

Ndgu wadau mimi n mkaz wa jiji la Mwanza ktk hali ya kutaka kujikwamua kiuchumi nimedhamiria kuanza biashara ya kusafirisha abiria kwa usafiri wa bajaji. Kwa hali hiyo kwa wenye uzoefu naomba msaada wa mambo yafuatayo:

1. Naomba kufahamu bei halisi ya kununua bajaji mpya.
2. Tahadhari muhimu za kuchukua/kuzngatia pindi naponunua bajaji mpya
3. Naomba kufahamu taratibu muhimu za kufuata kabla ya kuanza biashara hii.
4. Changamoto za biashara hii.
5. Ushaur juu ya mahali panapolipa zaid kwa wenye uzoefu na mazingira ya jiji la Mwanza
6. Ushaur kuhusu mengineyo.

Natanguliza shukran zangu kwa wote mtakao amua kutumia muda wenu kunisaidia kimawazo ktk harakat zangu hizi.
 
Ni biashara nzuri hasa ukimpata Dereva anaejali kazi.
Pia bei za bajaji zinatofautiana kulingana name Aina ya Bajaji uitakayo.
Zipo za bei poa mf mill 3, 4, 5, 6 mpka 7.
Ubora wa Bajaji ndiyo gharama inavyozidi kuwa juu.
Kiri kingine cha msingi ni barabara-mahala ambapo bajaji itakuwa inafanyia laziness, ukipata sehemu ya mjn ambayo barabara ni nzuri utafurahi lkn maeneo yenye barabara mbovu Italian mana bajaji itawahi kuchoka.
N. K
 
Bajaji mpya ni million 7.3 kwa TVs na Million 7 kwa R.E ni biashara nzuri ukipata Dereva mzuri , ukinunua kama ni mpya unakatia bima ukitaka comprehensive Tsh laki 5 na kidogo kwa bajaji mpya, na third party tsh 141600. But kila biashara inachangamoto..... Ukipata Dereva mzuri utafurahi na Roho yako........
 
Biashara uisikie kwny makaratasi na midomo ya watu.


Madereva mwanzo wanaanza vzr lkn baada ya muda mtapelekeshana sana....mm nshafanya biashara ya bajaj najua matatizo yake.


Ila kama umeamua kuingia ni sawa tu mkuu nakutakia kila kheri
 
biashara nzuri sana mkuu. Nunua Tvs King 7.2M hizi ndo imara na zinadumu weka msimamizi ye ndo atafute madereva atakao wamudu upigee pesaa yakoo mkuu. Uzuri wa bajaji unapiga iwe ni nje ya mji au mjini kati. kwa mwanza hesabu ni Tsh elfu ishirini

Uzuri wa bajaji.
  • Gharama nafuu za uendeshaji
  • Devera anajilipa mwenyewe cha msingi hesabu yako ikamilike
  • Kodi Tsh Laki moja na nusu kwa mwaka
  • Spare bei nafuu
 
Bajaji moja. Hapo hapo dereva ale na aibe.. hapo hapo msimamizi nae ale na aibe... na hapo hapo na bosi ule kweli...

Acheni mjaza ujinga mwenzenu.

Mimi namshauri kama hiyo bajaj ataendesha mwenyewe anunue fasta, ila kama anamkabidhi dereva ajiandae kisaikolojia kusumbuliwa na akiwa mkali wanampigia zengwe inaibiwa.

 
Uoga ndio umasikini wako acha sie tunaofanya tufanye mkuu hakuna biashara isiyokua na changamoto kila kitu kinahitaji uthubutu.
 
Nkondo 2
1. Naomba kufahamu bei halisi ya kununua bajaji mpya.

TVS-7.3M na RE BAJAJ-7M
2. Tahadhar muhimu za kuchukua/kuzngatia pindi naponunua bajaji mpya.
- Nunua mpya usichukue second hand
- Umesema unatokea Mwanza, kwa jiografia ya huo mji chukua RE-BAJAJ hizi zina nguvu lakini sio fuel efficiency, spare parts zake ni ghali compared to TVS KING

3. Naomba kufahamu taratibu muhimu za kufuata kabla ya kuanza biashara hii.
- Tafuta dereva mzuri, huyu kumpata unaweza fanya uchunguzi kupitia watu wanaoendesha naye
- Ikatie comprehensive insuarance tumia bima ya CRDB ni 6% ya bei ya chombo
- Itengee akaunti special hela itakapokuwa inaingia

4. Changamoto za biashara hii
- Uaminifu wa madereva(hesabu)
- Ajali barabarani
- Service on time kufanya
- Matumizi ya spare original

6. Ushaur kuhusu mengineyo
- Hakikisha unachukua hela kwa siku, usikubali uchukue hela kwa week mtasumbuana na dereva
- Siku ya service hakikisha unakuwepo wewe/muwakilishi kujiridhisha vifaa vinavyowekwa ni Genuine
- Kuna makampuni yana jishughulisha na kufanya service, usipende sana mafundi wa mitaani kuibiwa njenje
- mzuie/muonye dereva kukitoa chombo kukoroga/day waka
- Ukinunua chombo waweza kaa nacho miezi hata 6-8 then kitoe kwa dereva kama mkataba ili kisikusumbue saana

wick
 
Tafuta Dereva mwaminifu nA mwenye ujuzi wa kaz na mpe mkataba na awe anakuletea Tsh 140000 kwa week.
Zingatia "ujuzi" na "historia ya Uaminifu"

Nunua TvS King M 7.2
 
Safiii
 
Umefikia wapi???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…