Kanal Hilal
Member
- Feb 4, 2017
- 62
- 121
Nimefuatilia mijadala mbali mbali kuhusu ongezeko la gharama na tozo mpya za miamala ya kifedha kwa upande huduma wa mitandao ya simu za mkononi. Mjadala umekuwa mkubwa sana kwenye mitandao mbalimbali.
Wananchi wanalalamikia ongezeko la tozo hizi huku kiasi kikubwa cha makato (tozo) hizo kikienda kwa serikali, ambapo gharama za miamala kwa upande wa mitandao ya simu zikibaki vile vile.
Bibi yangu anasema hivi, "hili si swala la kuilalamikia au kuilaumu serikali. Ni swala la kufanya maamuzi tu ya pamoja kama wananchi, kwa sababu kuna njia mbadala za kutatua. Ikiwa gharama ni kubwa na hatuwezi kumudu tunapaswa kubadili mfumo. Badala ya kutumia huduma za kifedha za simu, tutumie huduma za kifedha za benki ambazo zimebaki vile vile na ni nafuu zaidi."
Maneno ya bibi yana uhalisia zaidi. Nadhani ndio muda muafaka wa mabenki kutimia hili kama fursa ya kujiimarisha kwa kusambaza mawakala wao maeneo kwenye maeneo mbali mbali nchini, mjini na vijijini. Hilo litatuhakikishia wateja kupata huduma mahali popote pale tutakapokuwa.
Tazama, kutoa pesa shilingi 200,000 hadi 299,000 kupitia Akaunti ya CRDB tozo yake ni shilingi 4,900 tu wakati TigoPesa, Airtel Money, M-Pesa na wengine tozo ni shilingi 8,240. Maana yake ni kuwa, kutoa pesa benki ni nafuu mara mbili zaidi ya kutoa pesa kwenye mitandao ya simu.
Nikiitafakari vema kauli ya bibi, nadhani sasa ndio wakati sahihi kwa wananchi kuanza kumiliki akaunti za benki na kuzitumia akaunti zao kama MUARUBAINI tatizo hili la kupanda kwa tozo za miamala.
Ingawa kuna dhana kuwa huduma za benki ni kwaajili ya wenye pesa (matajiri) tu-: hii si kweli. Hata mimi ni wewe tunaweza kutumiana pesa kupitia benki. Upatikanaji wa huduma ukiboreshwa ni rahisi na salama zaidi.
Wapo wanaosema eti bibi na babu zetu kule vijijini hawawezi kumudu huduma za kibenki kama ilivyokuwa kwenye simu. Katika hili nadhani hatujafanya utafiti (research) wa kutosha. Nenda vijijini ambako wazee wetu wanajishughulisha na kilimo, utagundua kuwa pesa zao zote za mauzo ya mazao wanaziweka kwenye AKAUNTI ZAO ZA BENKI.
Bibi yangu ana akaunti kwenye mabenki matatu tofauti na kote katunza pesa. Na yeye ndiye aliyeniambia nimtumie shilingi 10,000 ya sikuu ya Iddi el Hajji kwenye akaunti yake ya benki ili kuepuka makato mapya.
Ndugu zangu, tubadilike. Tunapaswa kubadili mfumo wa kutumiana fedha. Akaunti za benki kwa sasa zinalipa zaidi ya akaunti za simu za mkononi.
Na Hilal Kanal.
July 17, 2020.
Wananchi wanalalamikia ongezeko la tozo hizi huku kiasi kikubwa cha makato (tozo) hizo kikienda kwa serikali, ambapo gharama za miamala kwa upande wa mitandao ya simu zikibaki vile vile.
Bibi yangu anasema hivi, "hili si swala la kuilalamikia au kuilaumu serikali. Ni swala la kufanya maamuzi tu ya pamoja kama wananchi, kwa sababu kuna njia mbadala za kutatua. Ikiwa gharama ni kubwa na hatuwezi kumudu tunapaswa kubadili mfumo. Badala ya kutumia huduma za kifedha za simu, tutumie huduma za kifedha za benki ambazo zimebaki vile vile na ni nafuu zaidi."
Maneno ya bibi yana uhalisia zaidi. Nadhani ndio muda muafaka wa mabenki kutimia hili kama fursa ya kujiimarisha kwa kusambaza mawakala wao maeneo kwenye maeneo mbali mbali nchini, mjini na vijijini. Hilo litatuhakikishia wateja kupata huduma mahali popote pale tutakapokuwa.
Tazama, kutoa pesa shilingi 200,000 hadi 299,000 kupitia Akaunti ya CRDB tozo yake ni shilingi 4,900 tu wakati TigoPesa, Airtel Money, M-Pesa na wengine tozo ni shilingi 8,240. Maana yake ni kuwa, kutoa pesa benki ni nafuu mara mbili zaidi ya kutoa pesa kwenye mitandao ya simu.
Nikiitafakari vema kauli ya bibi, nadhani sasa ndio wakati sahihi kwa wananchi kuanza kumiliki akaunti za benki na kuzitumia akaunti zao kama MUARUBAINI tatizo hili la kupanda kwa tozo za miamala.
Ingawa kuna dhana kuwa huduma za benki ni kwaajili ya wenye pesa (matajiri) tu-: hii si kweli. Hata mimi ni wewe tunaweza kutumiana pesa kupitia benki. Upatikanaji wa huduma ukiboreshwa ni rahisi na salama zaidi.
Wapo wanaosema eti bibi na babu zetu kule vijijini hawawezi kumudu huduma za kibenki kama ilivyokuwa kwenye simu. Katika hili nadhani hatujafanya utafiti (research) wa kutosha. Nenda vijijini ambako wazee wetu wanajishughulisha na kilimo, utagundua kuwa pesa zao zote za mauzo ya mazao wanaziweka kwenye AKAUNTI ZAO ZA BENKI.
Bibi yangu ana akaunti kwenye mabenki matatu tofauti na kote katunza pesa. Na yeye ndiye aliyeniambia nimtumie shilingi 10,000 ya sikuu ya Iddi el Hajji kwenye akaunti yake ya benki ili kuepuka makato mapya.
Ndugu zangu, tubadilike. Tunapaswa kubadili mfumo wa kutumiana fedha. Akaunti za benki kwa sasa zinalipa zaidi ya akaunti za simu za mkononi.
Na Hilal Kanal.
July 17, 2020.