Bibi Titi Mohamed na akina Mama wa Bukoba 1950s

Bibi Titi Mohamed na akina Mama wa Bukoba 1950s

Picha hiyo hapo chini ya Bi. Titi na akina mama wa Bukoba wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika nimeletewa kutoka Bukoba na mmoja wa watu ambao nawaheshimu sana katika kuhifadhi kumbukumbu.

Kaniletea picha nyingi na In Shaa Allah nitaziweka hapa JF kwa faida yetu sote.

View attachment 1888827
Waliosimama kutoka kushòto Bìti Kaijage, Biti Sheikh, Biti Mwanandege walioketi kushoto Mama Boi, Bibi Titi na Biti Farahani. Hawa walikuwa viongozi wa Umoja wa akina mama wa TANU Bukoba.
Historia ya nchi hii amebebeshwa mtu mmoja tu wengine wakafichwa
 
U
Bukoka hii hii ambayo nilipita huelewi hata mji uko wapi?
Ivi unajuwa wabukoba wangapi wako nje wa nje lakini tokea kabla ya mkoloni hajaja bana.

Jk nyerere anaenda uno kudai Uhuru anadhania ndiye mtanganyika wa kwanza kufika uk.
Akashangaa kukutana na mtaa mzima wamejaa wahaya mpaka akashangaa kwa kilugha Chao akasema mbeeh.
Akawaogopa kinyama.
 
kuna tukio moja la wanawake wa UPARE ambao walipinga kodi ya mkoloni iliyoitwa MBIRU. tukio hilo ni vizuri likaelezwa kwasababu linashabihiana na kinachoendelea sasa hivi katika sakata la tozo za miamala.

Mwezi Januari mwaka 1945 kulitokea maandamano makubwa ya wenyeji wa wilaya ya Pare kupinga kodi(mbiru) iliyokuwa imeanzishwa bila ya wao kushirikishwa na mamlaka za Wakoloni na Machifu / Wafumwa.

Maandamano hayo yalianza kwa kuhusisha wanaume peke yao ambao walikusanyika kwa wiki kadhaa makao makuu ya wilaya Same mjini. Baadae wanawake nao wakajiunga na mkusanyiko huo wakimshinikiza DC na serikali wamalize mgogoro huo uliohusisha kodi.
 
kuna tukio moja la wanawake wa UPARE ambao walipinga kodi ya mkoloni iliyoitwa MBIRU. tukio hilo ni vizuri likaelezwa kwasababu linashabihiana na kinachoendelea sasa hivi katika sakata la tozo za miamala.

Mwezi Januari mwaka 1945 kulitokea maandamano makubwa ya wenyeji wa wilaya ya Pare kupinga kodi(mbiru) iliyokuwa imeanzishwa bila ya wao kushirikishwa na mamlaka za Wakoloni na Machifu / Wafumwa.

Maandamano hayo yalianza kwa kuhusisha wanaume peke yao ambao walikusanyika kwa wiki kadhaa makao makuu ya wilaya Same mjini. Baadae wanawake nao wakajiunga na mkusanyiko huo wakimshinikiza DC na serikali wamalize mgogoro huo uliohusisha kodi.
Saivi waandamaane basi hata mtandaoni
 
U

Ivi unajuwa wabukoba wangapi wako nje wa nje lakini tokea kabla ya mkoloni hajaja bana.

Jk nyerere anaenda uno kudai Uhuru anadhania ndiye mtanganyika wa kwanza kufika uk.
Akashangaa kukutana na mtaa mzima wamejaa wahaya mpaka akashangaa kwa kilugha Chao akasema mbeeh.
Akawaogopa kinyama.
Basi wajenge kwao
 
Siwezi kumsahau Bibi Titi alikuwa anatuuzia togwa mtaa wa Ngarambe. Alikuwa mtengenezaji mzuri sana wa togwa la mtama kwenye chupa za soda na Bwimbi.
Baadae akaanza kutuuzia mafuta ya taa, enzi hizo yaliadimika.
RIP.
Mhhhhhhhh mkuu mbona kama [emoji478][emoji506]
 
Mhhhhhhhh mkuu mbona kama [emoji478][emoji506]
Kwa mtu kama wewe utakuwa unaona ni maluweluwe.
Huyo bibi alikuwa humble sana, na nimepata bahati ya kuishi naye kama jirani yangu na wajukuu zake nimesoma nao mmoja wa kiume nimecheza nae mpira utotoni.
Ni vigumu kuelewa enzi hizo huwezi kuishi Dar bila vitambulisho. Sasa hivi mastar wenu kina Mwijaku, ndo lazima usielewe.
 
Makafiri wanapata taabu wanapoona majina ya kiislamu. Lakini huu ni ukweli usiyopingika, waislamu wana mchango mkubwa sana katika ukombozi wa nchi hii kutoka ktk mikono dhalimu ya wakoloni. Wengi wetu tumeathiriwa na historia aliyoiandika mzungu. Bila kutambua kwmb kuna uwongo mwingi ktk hiyo historia. Mfano mmoja wapo wa uwongo wa mzungu ktk historia, ni pale anapotufundisha kwmb "binaadamu hapo kabla alikuwa sokwe"
MAGAIDI yameshaharibu uzi
 
Dar...
Nime-document historia takriban yote ya kupigania uhuru wa Tanganyika kuanzia 1929 African Association ilipoundwa hadi 1961 uhuru ulipopatikana.

Ingia: mohamedsaidsalum.blogspot.com

Nitakueleza moja la Bi. Titi.

Abbas Sykes anasema wakati wa kupigania uhuru ilikuwa inafika mahali Mwalimu Nyerere akili imechoka hawezi kuhutubia.

Hapo wako chini ya jukwaa na uwanja umefurika watu.

Basi Nyerere akamwambia Bi. Titi apande jukwaani kuhutubia.

Bi. Titi atafanya hivyo.

Abbas Sykes anasema kutokana na hotuba ya Bi. Titi Mwalimu atapata "cue," na atazumgumza kutokana na yale aliyosema Bi. Titi.

Bi. Titi aliombwa na KANU aende Kenya kusaidia Kenyatta afunguliwe kutoka Kapenguria.

Alifanya mkutano mkubwa sana Tononoka, Mombasa akishirikiana na TANU Club iliyokuwa ikiongozwa na Ismail Bayuni kijana kutoka Moshi.

Kenyatta alipofunguliwa alikuja Tanganyika kumshukuru Bi. Titi na TANU kwa msaada wao.
Alikuwa nyumba ndogo yake
 
Mkuu, Mohamed Said!

Hao viongozi wa TANU kwa wanawake ukanda huo, Yaani wakina mama wa Bukoba walikuwa ni ndugu wa damu?!

Nimeona majina yao kufanana fanana karibu wote.

Na hapo walipokutana na Bibi Titi ulikuwa mwaka gani?
 
Makafiri wanapata taabu wanapoona majina ya kiislamu. Lakini huu ni ukweli usiyopingika, waislamu wana mchango mkubwa sana katika ukombozi wa nchi hii kutoka ktk mikono dhalimu ya wakoloni. Wengi wetu tumeathiriwa na historia aliyoiandika mzungu. Bila kutambua kwmb kuna uwongo mwingi ktk hiyo historia. Mfano mmoja wapo wa uwongo wa mzungu ktk historia, ni pale anapotufundisha kwmb "binaadamu hapo kabla alikuwa sokwe"
Majina ya kiislam au ya kiarabu? Kaijage nalo la kiislam au kihaya?
 
Mohamed Said, salaam.

Ama baada ya salamu Mimi ni buheri wa siha muruwa kabisa.

Dhumuni ya waraka huu ni kuomba kupata wasaa wa kuivinjari maktaba yako adhimu iliyojaa makablasha yenye makala, picha, maandiko, na kumbukumbu za namna kwa namna.

Natanguliza shukrani zangu za dhati.

Wako mtiifu, Bujibuji
"Buheri wa siha", "Buheri wa afya", "dhumuni la waraka", "Natanguliza shukrani zangu za dhati", "wako mtiifu".

Maneno hayo yananikumbusha miaka kadhaa ilopita, Ulikuwa ni uandishi safi kabisa na maridhawa ulotukuka kabla ya leo kuvamiwa kizazi cha "xaxa", xtaki, "xoma" n.k

Nakumbuka wakati huo niliandika barua mbili, Moja ikiwa ya kumwombea kazi jamaa yangu katika kampuni fulani ambapo alikubaliwa kazi moja kwa moja japo vigezo vingine havikuwa toshelezi.

Na waraka wa pili niliuandika kwa umaridadi kabisa ili kumtongoza binti, Na baada ya kuusoma alinielewa sana.
 
Mkuu, Mohamed Said!

Hao viongozi wa TANU kwa wanawake ukanda huo, Yaani wakina mama wa Bukoba walikuwa ni ndugu wa damu?!

Nimeona majina yao kufanana fanana karibu wote.

Na hapo walipokutana na Bibi Titi ulikuwa mwaka gani?
Regi...
Hiyo picha kanirushia mtu sina taarifa zaidi.
 
Back
Top Bottom