Bibi Titi Mohammed: Historia, harakati na wasifu wake

Bibi Titi Mohammed: Historia, harakati na wasifu wake

BIBI TITI MOHAMMED; MWANAMKE SHUJAA WA HARAKATI ZA UHURU WA TANGANYIKA ALIYEONJA JELA.

Na. Comred Mbwana Allyamtu


Kila binadamu hupitia magumu tena mara nyingine magumu hayo ambayo mimi huyaita ‘kipimo cha uimara wa mtu’ hupelekea kutoka kwa roho.
Leo nimeona si vibaya kuwakumbusha juu ya mwanamke aliyepata kujitoa kwa moyo wote ili nchi yetu ya Tanzania iwe huru lakini inaelezwa kuwa maisha yake ya mwisho hapa duniani yalijawa na huzuni, upweke, kubaguliwa na ufukara mkubwa.
Huyu ni Bibi Titi Mohammed, bila shaka vijana wengi wa sasa hawamjui kabisa mama huyu shupavu na wamekuwa wakisikia au kuiona tu barabara ya Bibi Titi. Kati ya miaka ya 1970 mwanamke mwenye wajihi wa ushupavu Bibi Titi Mohammed alihusishwa katika tukio la kujaribu kutaka kuipindua serikali ya wakati huo, Alihukumiwa kifungo cha maisha jela. Haikuwa rahisi kulipokea hilo kwani baadae alitolewa lakini ameendelea kukana kabisa mpaka umauti ulipomfika mwaka 2000.
Bibi Titi Mohammed aliingia TANU kwa kushawishiwa Schneider Plantan(Wanahistoria wengi huandika Nyerere-Baba wa Taifa ndo alimuingiza kwenye Chama si jambo la kweli) akapata kadi namba 16 na mumewe ndugu Boi Selemani alipewa kadi 15. Bibi Titi alikuwa mwasisi wa Umoja wa Wanawake Tanganyika (UWT) uliokuja kuundwa rasmi mwaka 1962.


Wakati wa harakati za kupigania uhuru alisimamia vikundi vya muziki kama vile lelemama’ na mara zote alitangulia kuongea na umati mkubwa kabla hata Nyerere hajaongea na watanganyika. Alikuwa na maneno makali dhidi ya ukoloni na alikuwa ana nguvu kubwa ya ushawishi. Akiwa na miaka 26 tu alikuwa ni mmoja kati ya wanawake wachache walioaminiwa katika kuongoza mapambano dhidi ya udhalimu waliokuwa wakifanyiwa Watanganyika.


Mwaka 1955, Nyerere na Bibi Titi Mohammed walifanya mkutano mkubwa huko Tabora. Hii ni kutokana na mualiko walioupata toka kwa watu wa huko, Ikumbukwe kuwa Tabora ya wakati huo ilikuwa na hamasa kubwa katika kudai uhuru. Hivyo mualiko ulitoka kwenye kamati ya wazee kama Hassan Mohamed Ikunji, Hamis Khalfan, Swedi Mambosasa, Germano Pacha, Juma Mrisho, Shaaban Mohamed Silabu, Bilali Rehani Waikela, Mohamed Mataka wakati ule akiwa muadhin wa Masjid Nur - msikiti wa Wamanyema pale Tabora.


Kuna mikutano mingi tu ya harakati za uhuru aliyoongoza Bibi Titi mfano ule wa Mombasa akishirikiana na Tom Mboya katika Ukumbi wa Tononoka. Kiujumala mkutano mkuu wa kwanza tabora ulifungua njia kukubalika kwa TanU baadaye kulifanyika Azimio La Tabora’. Azimio hilo liliongozwa na Nyerere na wengine kama Sheikh Suleiman Takadir,Mzee Jumbe Tambaza, Juma Selemani na Bibi Titi.
Baada ya uhuru 1961 alichaguliwa kuwa mbunge na waziri pia. Halikuwa jambo la kushtua kwani alistahili. Mwaka 1963 inaelezwa kulitokea kutokuelewana kati ya Bibi Titi na Mwalimu Nyerere wakati wa mkutano wa Halmashauri Kuu ya TANU uliofanyika Ukumbi wa Karimjee.

Hapo walitupiana maneno makali kabisa. Inaelezwa kuwa kati ya mambo mengine mengi sababu zilikuwa ni Halmashauri Kuu ya TANU kulivunja Baraza la Wazee wa TANU ambao kwa hakika walisaidia wakati wa harakati za uhuru, Hilo lilipingwa na Bibi Titi.


Jambo jingine linaelezwa na mwandishi Said Mohammed katika maandishi yake kuwa ni uamuzi wa Bibi Titi kuitetea jumuia ya EAMWS ambapo Mwalimu Nyerere alipinga hilo kwani aliona ni hatari kuchanganya ‘Dini na Siasa’. Bado kumekuwa na ugumu kupata taarifa hasa chanza cha mtifuano huo kwani wengi wanaelezea mkutano huo ulikuwa ni nafasi ya kuonesha tofauti zao wazi wazi.
Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1965 Bibi Titi na Tewa(Tewa Said Tewa alikuwa rais wa jumuia ya EAMWS) wakapoteza viti vyao ndani ya TANU na serikalini. Mwaka 1968, Bibi Titi alikamatwa na kuhusishwa na tukio la uhaini’ Mahakama ilimkuta na hatia ,alihukumiwa kwenda jela maisha. Mwaka 1972 aliachiwa huru kwa msamaha wa rais. Bado aliendelea kukana kuhusika kabisa na tukio hilo. Alirudi na kuendelea na maisha yake ya kawaida huko maeneo ya Temeke.

Inaelezwa kuwa kuwa alipoteza kumbukumbu za harakati za uhuru kama vile picha na taarifa nyingi za vikao.
Aliporudi walikuwa na urafiki kama zamani na Mwalimu Nyerere kama zamani, Aliumwa na kupelekwa na serikali ya Tanzania katika hospitali ya Net Care huko Afrika ya Kusini. Alifariki dunia akiwa hapo hospitalini akipata matibabu tarehe 5 Novemba 2000. Hakika ni ‘mama wa nguvu’ na shujaa mwanamke wa Tanzania yetu.

Ndimi

Comred Mbwana Allyamtu

+255679555526
+255765026057
Mbwanaallyamtu990@gmail. Com
d49a78211fe07afd114634c426c54a1c.jpg
 
BIBI TITI MOHAMMED; MWANAMKE SHUJAA WA HARAKATI ZA UHURU WA TANGANYIKA ALIYEONJA JELA.

Na. Comred Mbwana Allyamtu


Kila binadamu hupitia magumu tena mara nyingine magumu hayo ambayo mimi huyaita ‘kipimo cha uimara wa mtu’ hupelekea kutoka kwa roho.
Leo nimeona si vibaya kuwakumbusha juu ya mwanamke aliyepata kujitoa kwa moyo wote ili nchi yetu ya Tanzania iwe huru lakini inaelezwa kuwa maisha yake ya mwisho hapa duniani yalijawa na huzuni, upweke, kubaguliwa na ufukara mkubwa.
Huyu ni Bibi Titi Mohammed, bila shaka vijana wengi wa sasa hawamjui kabisa mama huyu shupavu na wamekuwa wakisikia au kuiona tu barabara ya Bibi Titi. Kati ya miaka ya 1970 mwanamke mwenye wajihi wa ushupavu Bibi Titi Mohammed alihusishwa katika tukio la kujaribu kutaka kuipindua serikali ya wakati huo, Alihukumiwa kifungo cha maisha jela. Haikuwa rahisi kulipokea hilo kwani baadae alitolewa lakini ameendelea kukana kabisa mpaka umauti ulipomfika mwaka 2000.
Bibi Titi Mohammed aliingia TANU kwa kushawishiwa Schneider Plantan(Wanahistoria wengi huandika Nyerere-Baba wa Taifa ndo alimuingiza kwenye Chama si jambo la kweli) akapata kadi namba 16 na mumewe ndugu Boi Selemani alipewa kadi 15. Bibi Titi alikuwa mwasisi wa Umoja wa Wanawake Tanganyika (UWT) uliokuja kuundwa rasmi mwaka 1962.


Wakati wa harakati za kupigania uhuru alisimamia vikundi vya muziki kama vile lelemama’ na mara zote alitangulia kuongea na umati mkubwa kabla hata Nyerere hajaongea na watanganyika. Alikuwa na maneno makali dhidi ya ukoloni na alikuwa ana nguvu kubwa ya ushawishi. Akiwa na miaka 26 tu alikuwa ni mmoja kati ya wanawake wachache walioaminiwa katika kuongoza mapambano dhidi ya udhalimu waliokuwa wakifanyiwa Watanganyika.


Mwaka 1955, Nyerere na Bibi Titi Mohammed walifanya mkutano mkubwa huko Tabora. Hii ni kutokana na mualiko walioupata toka kwa watu wa huko, Ikumbukwe kuwa Tabora ya wakati huo ilikuwa na hamasa kubwa katika kudai uhuru. Hivyo mualiko ulitoka kwenye kamati ya wazee kama Hassan Mohamed Ikunji, Hamis Khalfan, Swedi Mambosasa, Germano Pacha, Juma Mrisho, Shaaban Mohamed Silabu, Bilali Rehani Waikela, Mohamed Mataka wakati ule akiwa muadhin wa Masjid Nur - msikiti wa Wamanyema pale Tabora.


Kuna mikutano mingi tu ya harakati za uhuru aliyoongoza Bibi Titi mfano ule wa Mombasa akishirikiana na Tom Mboya katika Ukumbi wa Tononoka. Kiujumala mkutano mkuu wa kwanza tabora ulifungua njia kukubalika kwa TanU baadaye kulifanyika Azimio La Tabora’. Azimio hilo liliongozwa na Nyerere na wengine kama Sheikh Suleiman Takadir,Mzee Jumbe Tambaza, Juma Selemani na Bibi Titi.
Baada ya uhuru 1961 alichaguliwa kuwa mbunge na waziri pia. Halikuwa jambo la kushtua kwani alistahili. Mwaka 1963 inaelezwa kulitokea kutokuelewana kati ya Bibi Titi na Mwalimu Nyerere wakati wa mkutano wa Halmashauri Kuu ya TANU uliofanyika Ukumbi wa Karimjee.

Hapo walitupiana maneno makali kabisa. Inaelezwa kuwa kati ya mambo mengine mengi sababu zilikuwa ni Halmashauri Kuu ya TANU kulivunja Baraza la Wazee wa TANU ambao kwa hakika walisaidia wakati wa harakati za uhuru, Hilo lilipingwa na Bibi Titi.


Jambo jingine linaelezwa na mwandishi Said Mohammed katika maandishi yake kuwa ni uamuzi wa Bibi Titi kuitetea jumuia ya EAMWS ambapo Mwalimu Nyerere alipinga hilo kwani aliona ni hatari kuchanganya ‘Dini na Siasa’. Bado kumekuwa na ugumu kupata taarifa hasa chanza cha mtifuano huo kwani wengi wanaelezea mkutano huo ulikuwa ni nafasi ya kuonesha tofauti zao wazi wazi.
Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1965 Bibi Titi na Tewa(Tewa Said Tewa alikuwa rais wa jumuia ya EAMWS) wakapoteza viti vyao ndani ya TANU na serikalini. Mwaka 1968, Bibi Titi alikamatwa na kuhusishwa na tukio la uhaini’ Mahakama ilimkuta na hatia ,alihukumiwa kwenda jela maisha. Mwaka 1972 aliachiwa huru kwa msamaha wa rais. Bado aliendelea kukana kuhusika kabisa na tukio hilo. Alirudi na kuendelea na maisha yake ya kawaida huko maeneo ya Temeke.

Inaelezwa kuwa kuwa alipoteza kumbukumbu za harakati za uhuru kama vile picha na taarifa nyingi za vikao.
Aliporudi walikuwa na urafiki kama zamani na Mwalimu Nyerere kama zamani, Aliumwa na kupelekwa na serikali ya Tanzania katika hospitali ya Net Care huko Afrika ya Kusini. Alifariki dunia akiwa hapo hospitalini akipata matibabu tarehe 5 Novemba 2000. Hakika ni ‘mama wa nguvu’ na shujaa mwanamke wa Tanzania yetu.

Ndimi

Comred Mbwana Allyamtu

+255679555526
+255765026057
Mbwanaallyamtu990@gmail. Com
0d21db391083990895771d18edcde156.jpg
 
Bariadi,
Ahsante kwa link ya Bibi Titi.

Nimeisoma lakini kwa kweli hamna kitu mle ndani.

Hivi ndivyo nilivyoanza utangulizi kwa kitabu changu kuhusu Bibi Titi Mohamed (1926-2000):

''Ni vigumu kusema ni lini nimekuja kumfahamu Bi. Titi Mohamed. Nimefumbua macho nikikuwa
katika mitaa ya Dar es Salaam ya miaka ya 1950 na 1960 nikimuona na kumfahamu kuwa huyu
ndiye Bi. Titi. Mwanamke shupavu na kiongozi wa TANU.

Haikunipitikia kwa wakati ule nikiwa bado kijana mdogo wakati mwingine nikimuona katika mikutano
ya TANU pale Mnazi Mmoja au Jangwani kuwa ipo siku nitakaa nitafiti historia ya mashujaa wa uhuru
wa Tanganyika na Bi. Titi awe mmoja wa mashujaa wangu ambao nilataka sana kuandika maisha yao.

Siku moja tu kabla ya kifo cha Bi. Titi nilikuwa nikihojiwa na mwanafunzi wa kike wa Kitaliana kutoka
Chuo Kikuu cha Napoli, Italia ambae alikuwa akifanya utafiti kuhusu nafasi ya wanawake katika harakati
za kudai uhuru wa Tanganyika.

Binti huyu alikuwa alinihoji kuhusu Bi. Titi na akataka kujua kwa nini hatajiki katika historia ya TANU na
kwa nini wanawake wenzake aliokuwa nao katika harakati za kudai uhuru wanaonekana kutopenda
kueleza habari za Bi. Titi.

Nilimfahamisha binti yule kuwa sisi Watanzania tuna historia rasmi ya uhuru wa Tanzania ambayo
tunatakiwa kuienzi. Historia hiyo inaanza na Mwalimu Nyerere na kuishia na Mwalimu Nyerere.

Historia hiyo imewatoa wazalendo wengi katika historia pamoja na Bi. Titi. Binti huyo alikuwa na
masikitikokuwa wakati alipofanya mipango ya kutaka kwenda kumuhoji Bi. Titi akamkuta mgonjwa
kwa hiyo hakuweza kufanya mahojiano.

Nilimfahamisha mtafiti huyu yale niliyokuwa nayajua kuhusu Bi. Titi kisha tukaagana. Siku ya pili
nikapata habari kuwa Bi. Titi amefariki.

Kama alivyokuwa akisema mwenyewe marehemu, ‘Yote kuhusu mimi yameshaandikwa nyie waandishi
wa leo mtaandika nini ?'

Ni kweli Bi. Titi kaandikwa sana lakini waliomuandika hawakummaliza, kwa kuwa hawakummaliza ndiyo
maana na mimi nimepata nguvu ya kuweza kumuandika lau kama kwa muhtasari. Kwa hakika wengi wa
waandishi hao walikuwa wageni ; na wale waandishi wazalendo walipomwandika Bi. Titi walimwandika
kwa mtazamo wa agenda zao na vilevile bila kuwa na ujuzi wa historia ya Dar es Salaam katika miaka
ya 1950.

Wageni walimtazama Bi. Titi kwa jicho la ugeni mimi nataka kumwandika Bi. Titi kama alivyokwenda na
historia ya kudai uhuru. Nataka kumueleza Bi. Titi tokea mwanzo alipokuwa na Mwalimu Nyerere.
Nyerere akibandua hatua yake unyayo wa Bi. Titi unafuatia.

Nataka kumuandika Bi. Titi jinsi alivyopanda kutoka msichana mdogo wa Ki-Dar es Salaam akiwa na
miaka 26 hadi kufikia umaarufu mkubwa kabisa. Kisha ghafla nyota yake ikachujuka akaanguka na
akaishia kufungwa kifungo cha maisha kwa kosa la uhaini ambalo hadi kufa kwake alikana kuhusika.

Nataka kumuandika Bi. Titi jinsi alivyotoka kifungoni akiwa fukara mali yake yote imepotea na jinsi
alivyoyakabili maisha ya upweke na kutengwa. Nataka kumuandika Bi. Titi jinsi kwa ufundi mkubwa
na subra ya hali ya juu alivyomtegemea Mungu kama nilivyopata kumsikia akisema na Mungu akaitika
dua zake na kamrudishia siyo mali zake tu bali hata na hadhi yake.

Mtaa aliopewa kwa heshima yake ambao alinyang'anywa ukaja kurudishwa jina lake. Na wale waliomfanyia
khiyana ile wakiwa wa hai na hawana uwezo wa kufanya lolote.

Vipi Bi. Titi akaja kuuguzwa na kuzikwa na walewale watu waliolitangazia taifa kuwa alikuwa msaliti na
ta'azia zao baada ya kifo chake zikajaa maneno ya kumsifu. Ilikuwaje ikawa hivyo?

Nikiwa mtu mzima nilifanyiwa mihadi ya kuzungumza na Bi. Titi katika ya miaka ya 1990 nyumbani kwake
Upanga. Baada ya kusalimiana na kuniuliza nilikotoka nilimfahamisha wazazi wangu. Nilishangaa kuwa
alikuwa anamfahamu baba yangu vizuri sana hata akanieleza wajihi na umbo lake.

Nilimfahamisha kuwa nilikuwa nataka kuandika maisha yake. Bi. Titi akanikatalia kwa njia ya kistaarabu
kabisa. Kwa hekima kubwa sana aliweza kunitoa katika mazungumzo ya harakati za siasa za kudai uhuru
na akaelekeza fikra zangu katika senema ya watoto Cinderella niliyokuta akitizama pamoja na wajukuu
zake.

Kwa wale ambao walikuwa karibu na Bi. Titi watakuwa wanajua jinsi alivyokuwa fasaha wa kuzungumza
na jinsi alivyokuwa hodari wa kushinikiza hoja zake. Niliishia kunywa soda na kutazama ile senema katika
TV kisha tukaagana.

Lakini kwangu mimi nilikuwa nimefarajika sana. Miaka michache iliyopita rafiki yangu mmoja alikuwa anamuoa
binti ya ndugu yake Bi. Titi na harusi hii ilifanyika nyumbani kwa Bi. Titi Temeke. Hali niliyomkutanayo pale
Upanga ilikuwa tofauti sana na nilivyomuona Upanga mara tu alivyotoka kifungoni.

Kabla sijaondola Bi. Titi alinifahamisha kuwa hazina yake ya nyaraka za wakati wa kudai uhuru pamoja na picha
zake nyingi za kihistoria zilichukuliwa na askari wapelelezi wakati walipokuja kufanya upekuzi katika nyumba yake
kwa ajili ya tuhuma za kupindua serikali zilizokuwa zimemkabili katika miaka ya 1970.

Nilisikitishwa na hili kwa kuwa nilijua yeyote atakaekuja kuandika habari za Bi. Titi atakuwa amekosa zana za
kumsaidia kumwandika mama huyu kwa usahihi.''
roho imeniuma sana napo mkumbuka nyamadwanga marufu kama bibi titi shujaa Wa kindengereko
 
roho imeniuma sana napo mkumbuka nyamadwanga marufu kama bibi titi shujaa Wa kindengereko
Mndengereko One,
Allah amweke mahali pema peponi mama yetu huyu Bi. Titi biti Mohamed.

Nakuwekea picha yake ya mwaka 1955 wakati anaijenga TANU bega kwa bega
na Mwalimu Nyerere.

Hapo ni Magomeni Mapipa Mtaa wa Jaribu mahali Ali Msham alipofungua tawi
la TANU:

Ze66-NrvArZ16oI8DuSwtahV87kXO_7RnL4c5V-kNMae-zjFvIuJRZr7raM60GoNyObCOhg7-4B-L5mtZXREml7ii5TFd9O3aAr1dPnNKYq6JDfeP3rLt7mLu3iOIhCC-d46XgPgNrqrTA6yLQBbWx0bOp00wGARe7F0VkQqhALnBHj1394MLjkvHocnE1v-3B6Q2OAcXYNnl5oeQ7Dv-jbc_J866KbjdJoNRbl9DVOvVhs6buKIKsiVPPkNjOgv9_0qpVzUrkpLPajlNgViujtZKXSIQh0RRFHXAPgzD0lKG4tSO86o_xOwQRMqjqEBWODAJcAtm7c32empNCFjSRokMmSW5VkC83hPN8JYBhD6A1oNASTeWOHCMB8Sf4o2tKH423dJg4jyzFf46wu4PfeDJ2TJ1678bMrTj3EEHNgWfNygHsvwjHXWoWK35eKLHpey-92DFEeugmZA0VOUbmVH-0bmA92MYFzCR0HIixO_OqxiuehlxFFjD-bIi1Wf1Gx4hdYfYOQ3T_aItavC1IsJxGGDtdrC8WCVEbU2ivtD4oa5A1a0cjKh69fSR0UbC8Yr6trBzu71FDS0BHkNVOuui4-qU8Wa=w429-h297-no


Bi. Titi Mohamed wa tatu kushoto waliokaa
 
Mndengereko One,
Allah amweke mahali pema peponi mama yetu huyu Bi. Titi biti Mohamed.

Nakuwekea picha yake ya mwaka 1955 wakati anaijenga TANU bega kwa bega
na Mwalimu Nyerere.

Hapo ni Magomeni Mapipa Mtaa wa Jaribu mahali Ali Msham alipofungua tawi
la TANU:

Ze66-NrvArZ16oI8DuSwtahV87kXO_7RnL4c5V-kNMae-zjFvIuJRZr7raM60GoNyObCOhg7-4B-L5mtZXREml7ii5TFd9O3aAr1dPnNKYq6JDfeP3rLt7mLu3iOIhCC-d46XgPgNrqrTA6yLQBbWx0bOp00wGARe7F0VkQqhALnBHj1394MLjkvHocnE1v-3B6Q2OAcXYNnl5oeQ7Dv-jbc_J866KbjdJoNRbl9DVOvVhs6buKIKsiVPPkNjOgv9_0qpVzUrkpLPajlNgViujtZKXSIQh0RRFHXAPgzD0lKG4tSO86o_xOwQRMqjqEBWODAJcAtm7c32empNCFjSRokMmSW5VkC83hPN8JYBhD6A1oNASTeWOHCMB8Sf4o2tKH423dJg4jyzFf46wu4PfeDJ2TJ1678bMrTj3EEHNgWfNygHsvwjHXWoWK35eKLHpey-92DFEeugmZA0VOUbmVH-0bmA92MYFzCR0HIixO_OqxiuehlxFFjD-bIi1Wf1Gx4hdYfYOQ3T_aItavC1IsJxGGDtdrC8WCVEbU2ivtD4oa5A1a0cjKh69fSR0UbC8Yr6trBzu71FDS0BHkNVOuui4-qU8Wa=w429-h297-no


Bi. Titi Mohamed wa tatu kushoto waliokaa
mm huyu nyamadwanga naudugu nae wa damu
 
Habari Wana JF !

Naomba kama kuna Mtu Yoyote anajua Historia ya Bibi Titi anijuvye.

Huyu Mama anaonekana kutajwa sana hapa Tanzania Mpaka kuna Barabara inaitwa Bibi Titi Street, Je Huyu alikua ni Mwanasiasa au ?

Umaarufu wake unatokana na Nini ?

Wadau Naomba Majibu yatakanifunua Macho na Kujua Historia ya Taifa Letu.

----------------------------------------------------------------------------------------------------






Kwa habari zaidi zinazo Mhusu Soma Hapa
Bikra,
Nikikupa link haitoshi wewe kumjua Bi. Titi Mohamed.
Nakushauri soma kitabu cha Abdul Sykes.

Kila alipoweka mguu Mwalimu Nyerere nyayo iliyofuata
ilikuwa ya Bi. Titi.

Bi. Titi kahutubia mkutano wa TANU Mnazi Mmoja 1954
hajaona sura ya Mwalimu Nyerere.

Kaletwa kwenye chama na Schneider Abdullah Plantan.

Kitabu kinauzwa Ibn Hazm Media Centre Bookshop Msikiti
wa Mtoro na Manyema, Elite Bookshop Mbezi Samaki,
Soma Bookshop Mikocheni na Rubawa Investment Amana.

Nakuwekea hapo chini picha ya Bi. Titi na Nyerere siku ya
kusheherekea uhuru wa Tanganyika katiba ''Ball,'' iliyotumbuizwa
na band Royal Marine Band, Diamond Jubilee Hall:

y8zReMD0hArK2d8rM_b2b7HxOJV4ki9BnnVUplT9_wqa3qyoBMNKscqHjdzWlC0SxGtJkPqaDA20hj401LnhMXW6Qo3Y3ahuhkTh0mfnN1H8onB4Mlals9KUdR3m4MqxWP8X7Z-64-g6Z1YiiEraYwK26Ob3HlXu5DzqFQn65cdaIb24IY_B7SVG-pPVOhaxkwk99g4c9cF3Zp44EVPyFOSheijtemEql3IMDBCf_qsozRylHqJvDtw7Kqy9scpC000WG9tFc9MJDSjZmDba_Yk4aUmnUjuAqsdBJRygvo4LqACQlNVxwfertXEeMYmLsikUVH14TGP-SH-w05NY3_2eXP5Z6p_-FBdtz6fjo0TLv71AlVJvQlERZJPsrb7gvJILvfz_0vzRO3NiDa78Bw_LkqhfHMO9J-91wEIQZD0nD1oXNCOIOgh6ucdtufKlYbs1J5W3benFZRFdb1W_SeX9ZRe8TeRMCbEQL7bMicTfdpO5caUe37Q4oye9SfMy-g2wieFWp1mDmW2FWRB8T3K4c9vHA7pNYVYcNwrlgxHb0jY-9ByiDASqj1n-3XZUA0gH8qw3ZruNJ38vSRWxtq1NaXwponlM=w493-h657-no
 
Kama sitakosea niliwahi simuliwa na mzee wangu kuwa bibi huyo aliwekwa kizuizini ktk kijiji cha gumbiro barazani songea vijijini karibu na madaba akiwa kama bibi maendeleo.watu wa gumbiro ya zamani wanamfahamu sana bibi huyo
 
Bariadi,
Ahsante kwa link ya Bibi Titi.

Nimeisoma lakini kwa kweli hamna kitu mle ndani.

Hivi ndivyo nilivyoanza utangulizi kwa kitabu changu kuhusu Bibi Titi Mohamed (1926-2000):

''Ni vigumu kusema ni lini nimekuja kumfahamu Bi. Titi Mohamed. Nimefumbua macho nikikuwa
katika mitaa ya Dar es Salaam ya miaka ya 1950 na 1960 nikimuona na kumfahamu kuwa huyu
ndiye Bi. Titi. Mwanamke shupavu na kiongozi wa TANU.

Haikunipitikia kwa wakati ule nikiwa bado kijana mdogo wakati mwingine nikimuona katika mikutano
ya TANU pale Mnazi Mmoja au Jangwani kuwa ipo siku nitakaa nitafiti historia ya mashujaa wa uhuru
wa Tanganyika na Bi. Titi awe mmoja wa mashujaa wangu ambao nilataka sana kuandika maisha yao.

Siku moja tu kabla ya kifo cha Bi. Titi nilikuwa nikihojiwa na mwanafunzi wa kike wa Kitaliana kutoka
Chuo Kikuu cha Napoli, Italia ambae alikuwa akifanya utafiti kuhusu nafasi ya wanawake katika harakati
za kudai uhuru wa Tanganyika.

Binti huyu alikuwa alinihoji kuhusu Bi. Titi na akataka kujua kwa nini hatajiki katika historia ya TANU na
kwa nini wanawake wenzake aliokuwa nao katika harakati za kudai uhuru wanaonekana kutopenda
kueleza habari za Bi. Titi.

Nilimfahamisha binti yule kuwa sisi Watanzania tuna historia rasmi ya uhuru wa Tanzania ambayo
tunatakiwa kuienzi. Historia hiyo inaanza na Mwalimu Nyerere na kuishia na Mwalimu Nyerere.

Historia hiyo imewatoa wazalendo wengi katika historia pamoja na Bi. Titi. Binti huyo alikuwa na
masikitikokuwa wakati alipofanya mipango ya kutaka kwenda kumuhoji Bi. Titi akamkuta mgonjwa
kwa hiyo hakuweza kufanya mahojiano.

Nilimfahamisha mtafiti huyu yale niliyokuwa nayajua kuhusu Bi. Titi kisha tukaagana. Siku ya pili
nikapata habari kuwa Bi. Titi amefariki.

Kama alivyokuwa akisema mwenyewe marehemu, &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];Yote kuhusu mimi yameshaandikwa nyie waandishi
wa leo mtaandika nini ?'

Ni kweli Bi. Titi kaandikwa sana lakini waliomuandika hawakummaliza, kwa kuwa hawakummaliza ndiyo
maana na mimi nimepata nguvu ya kuweza kumuandika lau kama kwa muhtasari. Kwa hakika wengi wa
waandishi hao walikuwa wageni ; na wale waandishi wazalendo walipomwandika Bi. Titi walimwandika
kwa mtazamo wa agenda zao na vilevile bila kuwa na ujuzi wa historia ya Dar es Salaam katika miaka
ya 1950.

Wageni walimtazama Bi. Titi kwa jicho la ugeni mimi nataka kumwandika Bi. Titi kama alivyokwenda na
historia ya kudai uhuru. Nataka kumueleza Bi. Titi tokea mwanzo alipokuwa na Mwalimu Nyerere.
Nyerere akibandua hatua yake unyayo wa Bi. Titi unafuatia.

Nataka kumuandika Bi. Titi jinsi alivyopanda kutoka msichana mdogo wa Ki-Dar es Salaam akiwa na
miaka 26 hadi kufikia umaarufu mkubwa kabisa. Kisha ghafla nyota yake ikachujuka akaanguka na
akaishia kufungwa kifungo cha maisha kwa kosa la uhaini ambalo hadi kufa kwake alikana kuhusika.

Nataka kumuandika Bi. Titi jinsi alivyotoka kifungoni akiwa fukara mali yake yote imepotea na jinsi
alivyoyakabili maisha ya upweke na kutengwa. Nataka kumuandika Bi. Titi jinsi kwa ufundi mkubwa
na subra ya hali ya juu alivyomtegemea Mungu kama nilivyopata kumsikia akisema na Mungu akaitika
dua zake na kamrudishia siyo mali zake tu bali hata na hadhi yake.

Mtaa aliopewa kwa heshima yake ambao alinyang'anywa ukaja kurudishwa jina lake. Na wale waliomfanyia
khiyana ile wakiwa wa hai na hawana uwezo wa kufanya lolote.

Vipi Bi. Titi akaja kuuguzwa na kuzikwa na walewale watu waliolitangazia taifa kuwa alikuwa msaliti na
ta'azia zao baada ya kifo chake zikajaa maneno ya kumsifu. Ilikuwaje ikawa hivyo?

Nikiwa mtu mzima nilifanyiwa mihadi ya kuzungumza na Bi. Titi katika ya miaka ya 1990 nyumbani kwake
Upanga. Baada ya kusalimiana na kuniuliza nilikotoka nilimfahamisha wazazi wangu. Nilishangaa kuwa
alikuwa anamfahamu baba yangu vizuri sana hata akanieleza wajihi na umbo lake.

Nilimfahamisha kuwa nilikuwa nataka kuandika maisha yake. Bi. Titi akanikatalia kwa njia ya kistaarabu
kabisa. Kwa hekima kubwa sana aliweza kunitoa katika mazungumzo ya harakati za siasa za kudai uhuru
na akaelekeza fikra zangu katika senema ya watoto Cinderella niliyokuta akitizama pamoja na wajukuu
zake.

Kwa wale ambao walikuwa karibu na Bi. Titi watakuwa wanajua jinsi alivyokuwa fasaha wa kuzungumza
na jinsi alivyokuwa hodari wa kushinikiza hoja zake. Niliishia kunywa soda na kutazama ile senema katika
TV kisha tukaagana.

Lakini kwangu mimi nilikuwa nimefarajika sana. Miaka michache iliyopita rafiki yangu mmoja alikuwa anamuoa
binti ya ndugu yake Bi. Titi na harusi hii ilifanyika nyumbani kwa Bi. Titi Temeke. Hali niliyomkutanayo pale
Upanga ilikuwa tofauti sana na nilivyomuona Upanga mara tu alivyotoka kifungoni.

Kabla sijaondola Bi. Titi alinifahamisha kuwa hazina yake ya nyaraka za wakati wa kudai uhuru pamoja na picha
zake nyingi za kihistoria zilichukuliwa na askari wapelelezi wakati walipokuja kufanya upekuzi katika nyumba yake
kwa ajili ya tuhuma za kupindua serikali zilizokuwa zimemkabili katika miaka ya 1970.

Nilisikitishwa na hili kwa kuwa nilijua yeyote atakaekuja kuandika habari za Bi. Titi atakuwa amekosa zana za
kumsaidia kumwandika mama huyu kwa usahihi.''
Naomba kitabu chako
 
Baada ya kufahamiana na Mwalimu alipewa uongozi katika Women Wing ya TANU ambapo alishiriki katika kuhamasisha wanawake kuunga mkono harakati za TANU za kudai uhuru. Hata hivyo kwa mujibu wa Bibi Titi mwenyewe, (Kwa jinsi alivyowahi kuniambia) ni kwamba tofauti za msingi kati yake na Mwalimu zilianza mwaka 1958 ambapo Mwl. alimpeleka, kwa maelezo ya Bibi Titi, Demu wake masomoni Ulaya kwa kutumia Fedha za Umoja wa Wanawake badala ya mwanamke aliyekuwa amendekezwa na Umoja huo. Mwanamke huyo wakati huo alikuwa ni Nesi katika Hopitali mojawapo iliyokuwa mikoa ya kusini.

Japokuwa hakueleza, bayana kwa nini alichukizwa na kitendo kile cha Mwalimu, wadadisi wa mambo wanadai kuwa, chuki hiyo ilitokana na wivu wa kimapenzi kwani inadaiwa kuwa hata Mwalimu na Bibi Titi walikuwa................
cc; Elli BAK MANI tpaul zumbemkuu
Sina hakika kama historia hii mumewahi kuisoma maana thread hii ni ya zamani ila leo mie ndio nimeiona. Nimewashirikisha ili muwaze kama niwazavyo mimi hapa nilipo. Tufanye habari hii ni ya kweli, halafu tuchukulie maisha ya wakati huo (almost 60 years ago) na ya wakati huu tulionao. Kumbe duniani hakuna jipya kabisa! Haya mambo yetu haya kumbe yalikuwepo sana na hayata tuzuia kufikiriwa utakatifu hapo baadae kama tutayaenzi. Ni mtizamo tuu
 
Mie Mkuu nilipata bahati ya kuhadithiwa na watu waliomfahamu Bibi Titi kwa karibu kabisa. Walifahamiana naye hata kuweza kualikana majumbani mwao. Waliniambia kuhusu umaarufu mkubwa aliokuwa na Bibi Titi ndani ya TANU na pia ukaribu wake na Baba wa Taifa. Baba wa Taifa inasemekana alimpenda huyu kwa kujituma kwake katika kuhamasisha Watanganyika kujiunga na TANU na pia kwenye harakati za kutaka uhuru toka kwa Mkoloni. Hili la kuwa mpenzi wa Mwalimu sikuwahi kulisikia, labda hawakuona umuhimu wa mimi kulijua (kama ni kweli)

cc; Elli BAK MANI tpaul zumbemkuu
Sina hakika kama historia hii mumewahi kuisoma maana thread hii ni ya zamani ila leo mie ndio nimeiona. Nimewashirikisha ili muwaze kama niwazavyo mimi hapa nilipo. Tufanye habari hii ni ya kweli, halafu tuchukulie maisha ya wakati huo (almost 60 years ago) na ya wakati huu tulionao. Kumbe duniani hakuna jipya kabisa! Haya mambo yetu haya kumbe yalikuwepo sana na hayata tuzuia kufikiriwa utakatifu hapo baadae kama tutayaenzi. Ni mtizamo tuu
 
Bi Titi ni miongoni mwa watu ambao hawakutendewa haki na Nyerere,walijitolea maisha yao kudai uhuru lakini wakaishia jela
 
Jaman cc wengine tunafurahia kuongeza maarifa ktk ubongo wetu maana tulikua hatujui hii hustoria ya bibi titi na mwalimu
 
Sheikh Mohamed Said tupe kidogo juu ya Kambona na Bibi Titi ukaribu wao ulikuweje
 
Sheikh Mohamed Said tupe kidogo juu ya Kambona na Bibi Titi ukaribu wao ulikuweje
Kiatu...
Katika TANU kulikuwa na wasemaji kwa maana ya wahutubuaji wakubwa
wawili nao walikuwa ni Nyerere na Bi. Titi Mohamed.

Hawa wawili ndiyo walikuwa vinara wa harakati.

Kambona alikuja baadae katika TANU na yeye alikuwa na uwezo mkubwa
pia lakini hakumzidi Bi. Titi katika kukibeba chama.

Kwa kipindi kile cha kudai uhuru Bi. Titi alikuwa juu zaidi aking'ara zaidi ya
Kambona.

Kambona
alikuja kuwa juu baada ya uhuru kwani haukupita muda Bi. Titi
na Nyerere wakakuruzana mwaka wa 1963 Nyerere alipoonysha dalili za
kutaka kuifungia East African Muslim Welfare Society (EAMWS).
 
Back
Top Bottom