Victor Mlaki
JF-Expert Member
- May 1, 2016
- 4,151
- 4,277
Katika mambo yanayoshangaza ni namna Biblia inavyoonesha kurejea vitabu vingi ambavyo havipo ndani yake. Swali la kujiuliza ni je vitabu hivyo vimetajwa tu havipo au vimeondolewa? Na kama vimeondolewa ni kwa nini? Ni nani anafaidika na kutokuwepo kwa vitabu hivyo?
Angalia namna maandiko haya yafuatayo yanayoonesha uwepo wa vitabu vingine zaidi ya vilivyozoeleka:
2 Mambo ya nyakakati 12:14&15 " Naye akatenda yaliyo maovu, Kwa kuwa hakuutunza moyo wake amtafute BWANA. 15 Basi mambo yake Rehoboamu ya kwanza na ya mwisho je hayakuandikwa katika tarehe za Shemaya nabii na Ido mwonaji kwa jinsi ya kuandika nasaba?....Hapa inaonesha mambo ya Yeroboamu aliandikwa na kama yaliandikwa na yalipaswa kuwa katika makundi mawili ,Yeroboamu wa kwanza na Yeroboamu wa pili. Yaliandikwa katika tarehe za Shemaya. Je kitabu cha Shemaya kipo wapi? Nabii Ido mwonaji Je?...( Hapa kuna maarifa yamefichwa mahali).
Joshua 10:13 Ndipo jua likasimama na mwezi ukatulia, Hata Hilo Taifa lilipokuwa limekwisha jipatiliza juu ya adui zao. Hayo je hayakuandikwa ndani ya kitabu cha Yashari?...Tujiulize je yaliyoandikwa yalikuwa yapi? Na tungeyajua yangetusaidia kujifunza nini? Je kitabu cha Yashari kilichorejelewa kipo wapi? Hapa kuna maarifa tuliyopaswa kuyafahamu ila yamefichwa kwa maslahi fulani ya wachache wenye lengo fulani.
1Wafalme 14:19 Na mambo yake Yeroboamu yaliyosalia, ya kupigana na ya kutawala, tazama yameandikwa katika kitabu cha tarehe cha wafalme wa Israeli. Jiulize na wewe hiki kitabu cha tarehe cha wafalme wa Israeli linaonekana kuwa na siri za kupigana (vita) na kutawala lakini kwa nini hakipo katika Biblia zetu? Kuna kitu watu wachache wanakifahamu kwa faida yao ila wengi wetu tunapapasa tu " exoteric knowledge"
1 Wafalme 14: 29 Na mambo yake Rehoboamu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! hayakuandikwa katika kitabu cha tarehe cha wafalme wa Yuda? (Hiki kitabu cha tarehe cha wafalme wa Yuda kipo wapi). Kwa nini kisiwekwe wazi tukajifunza mambo ya Yeroboamu?
Najiuuliza tu ni kwa nini Biblia ambayo ni kitabu kitakatifu kinatutajia vitabu ambavyo havipo ndani yake?.Swali hili ni zito sana kwangu ila nina hakika kuwa haya yote yapo Kwa kusudi fulani na kuna watu wanafadika na hali ilivyo.
1 Wafalme 16:20 Na mambo yote ya Zimri yaliyosalia na fitina yake aliyoifanya, je! hayakuandikwa katika kitabu cha tarehe cha wafalme wa Israeli?. Huyu Zimri ni nani? alifanya fitina gani? Hiki kitabu cha wafalme wa Israeli kinaonekana kuwa na mambo muhimu sana ila ndiyo hivyo kimefichwa.
1Wafalme 11:41 Nayo yaliyosalia ya Sulemani mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je! hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani? .Je kuna kitabu kinachoeleza mambo yote aliyoyafanya Sulemani? Kama yapo ni kitabu kipi? Je Mithali na Muhubiri vinatosha kuwa vitabu vya mambo yote na hekima yote ya Sulemani?. Kuna kitabu cha Sulemani hapo kimefichwa mahali.
2 Wafalme 16:11 Na tazama mambo yake Asa ya kwanza na ya mwisho, angalia yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli. Hiki kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli kipo wapi?.
Kupitia maandiko hayo machache niliyoyarejelea Biblia inaonesha wazi kuwa ilikuwa na vitabu vingi zaidi na walioviondoa kwa kujua au kutojua waliacha kufuta maandiko yaliyorejelea vitabu walivyoviondoa kwa maslahi yao.
Siyo ajabu leo kutokana na kufichwa kwa maarifa jamii kubwa ya wanadamu ikafanywa vyovyote na watu wachache sana wanaoelewa maarifa halisi na yasiyoeleweka kwa wengi. Na hapa niaiona safari ndefu gizani.
Angalia namna maandiko haya yafuatayo yanayoonesha uwepo wa vitabu vingine zaidi ya vilivyozoeleka:
2 Mambo ya nyakakati 12:14&15 " Naye akatenda yaliyo maovu, Kwa kuwa hakuutunza moyo wake amtafute BWANA. 15 Basi mambo yake Rehoboamu ya kwanza na ya mwisho je hayakuandikwa katika tarehe za Shemaya nabii na Ido mwonaji kwa jinsi ya kuandika nasaba?....Hapa inaonesha mambo ya Yeroboamu aliandikwa na kama yaliandikwa na yalipaswa kuwa katika makundi mawili ,Yeroboamu wa kwanza na Yeroboamu wa pili. Yaliandikwa katika tarehe za Shemaya. Je kitabu cha Shemaya kipo wapi? Nabii Ido mwonaji Je?...( Hapa kuna maarifa yamefichwa mahali).
Joshua 10:13 Ndipo jua likasimama na mwezi ukatulia, Hata Hilo Taifa lilipokuwa limekwisha jipatiliza juu ya adui zao. Hayo je hayakuandikwa ndani ya kitabu cha Yashari?...Tujiulize je yaliyoandikwa yalikuwa yapi? Na tungeyajua yangetusaidia kujifunza nini? Je kitabu cha Yashari kilichorejelewa kipo wapi? Hapa kuna maarifa tuliyopaswa kuyafahamu ila yamefichwa kwa maslahi fulani ya wachache wenye lengo fulani.
1Wafalme 14:19 Na mambo yake Yeroboamu yaliyosalia, ya kupigana na ya kutawala, tazama yameandikwa katika kitabu cha tarehe cha wafalme wa Israeli. Jiulize na wewe hiki kitabu cha tarehe cha wafalme wa Israeli linaonekana kuwa na siri za kupigana (vita) na kutawala lakini kwa nini hakipo katika Biblia zetu? Kuna kitu watu wachache wanakifahamu kwa faida yao ila wengi wetu tunapapasa tu " exoteric knowledge"
1 Wafalme 14: 29 Na mambo yake Rehoboamu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! hayakuandikwa katika kitabu cha tarehe cha wafalme wa Yuda? (Hiki kitabu cha tarehe cha wafalme wa Yuda kipo wapi). Kwa nini kisiwekwe wazi tukajifunza mambo ya Yeroboamu?
Najiuuliza tu ni kwa nini Biblia ambayo ni kitabu kitakatifu kinatutajia vitabu ambavyo havipo ndani yake?.Swali hili ni zito sana kwangu ila nina hakika kuwa haya yote yapo Kwa kusudi fulani na kuna watu wanafadika na hali ilivyo.
1 Wafalme 16:20 Na mambo yote ya Zimri yaliyosalia na fitina yake aliyoifanya, je! hayakuandikwa katika kitabu cha tarehe cha wafalme wa Israeli?. Huyu Zimri ni nani? alifanya fitina gani? Hiki kitabu cha wafalme wa Israeli kinaonekana kuwa na mambo muhimu sana ila ndiyo hivyo kimefichwa.
1Wafalme 11:41 Nayo yaliyosalia ya Sulemani mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je! hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani? .Je kuna kitabu kinachoeleza mambo yote aliyoyafanya Sulemani? Kama yapo ni kitabu kipi? Je Mithali na Muhubiri vinatosha kuwa vitabu vya mambo yote na hekima yote ya Sulemani?. Kuna kitabu cha Sulemani hapo kimefichwa mahali.
2 Wafalme 16:11 Na tazama mambo yake Asa ya kwanza na ya mwisho, angalia yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli. Hiki kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli kipo wapi?.
Kupitia maandiko hayo machache niliyoyarejelea Biblia inaonesha wazi kuwa ilikuwa na vitabu vingi zaidi na walioviondoa kwa kujua au kutojua waliacha kufuta maandiko yaliyorejelea vitabu walivyoviondoa kwa maslahi yao.
Siyo ajabu leo kutokana na kufichwa kwa maarifa jamii kubwa ya wanadamu ikafanywa vyovyote na watu wachache sana wanaoelewa maarifa halisi na yasiyoeleweka kwa wengi. Na hapa niaiona safari ndefu gizani.