Biblia inasema fungu la kumi litolewe mara moja tu kwa mwaka, hawa wanaodai fungu la kumi kila wiki ni wezi. Fungu la 10 waweza kulinywea hata pombe

Kumbukumbu la Torati 14:22,24-26
[22]Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka.
Thou shalt truly tithe all the increase of thy seed, that the field bringeth forth year by year.

Fungu la kumi la kutoa kila wiki au hata kila mwezi, Lina tofauti gani na Fungu la kumi la kutoa mara moja kwa Mwaka????
 
Hizo pesa na Mali zilizokua zikitolewa zilikua zinaliwa na nani?

Au watu wa hilo hekalu walikua na uwezo wakumtumia huyo Mungu!!
 
Kutoa kila wiki/ kila mwezi ni Wiki na utapeli

Utapeli upo wapi hapo?

Na unaona waumini wangefanikiwa kutoa mara moja kwa Mwaka, kama wangefata ya Biblia?

Hiyo si itakuwa ni mwisho wa Mwaka.. Mwisho wa mwezi Disemba? Au lini?

Bado nauliza utofauti wa kiasi utakuwa wapi?
 
Aisee,sikujua hili..
Ila ch kushangaza Wakristo wanatawala Dunia katika kila nyanja!
Sasa kama Wapumbavu wasio na akili wanaitawala Dunia..

Sasa hapo wanaotawaliwa wakoje!
 
Wayahudi wengi walikuwa ni wakulima na wafugaji kama tunavyojua shughuli hizi mazao yao yanapatikana baada mwaka mzima ila sasa Dunia ya sasa imebadilika watu kila mwezi wanaingiza pesa
 
Utapeli upo wapi hapo?

Na unaona waumini wangefanikiwa kutoa mara moja kwa Mwaka, kama wangefata ya Biblia?

Hiyo si itakuwa ni mwisho wa Mwaka.. Mwisho wa mwezi Disemba? Au lini?

Bado nauliza utofauti wa kiasi utakuwa wapi?
Biblia imesema zaka itolewe mara moja tu kwa mwaka.
Anayekwambia utoe kila mwezi, maana yake utatoa zaka mara 12 kwa mwaka, kitu ambacho si agizo la Mungu.
Anayekwambia utoe kila wiki, huyo anataka utoe zaka mara 52 kwa mwaka, ni shetani kabisa huyo
 
Wayahudi wengi walikuwa ni wakulima na wafugaji kama tunavyojua shughuli hizi mazao yao yanapatikana baada mwaka mzima ila sasa Dunia ya sasa imebadilika watu kila mwezi wanaingiza pesa
Wafanyabiashara, na wafanyakazi (vibarua na watumwa) walikuwepo
 
Kiukweli uzi huu
Nimeona wengi u GT
Na uwezo wa nje ya BOKSI
Kuanzia mleta mada

Bado low low na nasikitika ni kupitia Dini, mmeonyesha mkoje.

Duh!!!!!!!!

Na subscribe nijege niwasome mlivyo mbeleni, nikiwa nataka kusoma pa kusongesha muda.
 
Kiukweli uzi huu
Nimeona wengi u GT
Na uwezo wa nje ya BOKSI
Kuanzia mleta mada

Bado low low na nasikitika ni kupitia Dini, mmeonyesha mkoje.

Duh!!!!!!!!

Na subscribe nijege niwasome mlivyo mbeleni, nikiwa nataka kusoma pa kusongesha muda.
Na wewe uko sawa tu na sisi, ndege wafananao huruka pamoja
 
Biblia imesema zaka itolewe mara moja tu kwa mwaka.
Anayekwambia utoe kila mwezi, maana yake utatoa zaka mara 12 kwa mwaka, kitu ambacho si agizo la Mungu.
Anayekwambia utoe kila wiki, huyo anataka utoe zaka mara 52 kwa mwaka, ni shetani kabisa huyo

Hata ukifafanua kitu najua utofauti huu.

Swali utofauti wake upo wapi hadi uwaite matapeli?

Utapeli huo hapo ukoje?

Si unaongelea fedha?

Ingekuwa siku, wiki, mwezi ndio shida.. Ungeandika wanakosea si ndio? Ukweli umekubali though bado utabisha..

Utofauti upoje mtu akitoa kwa wiki, kwa mwezi na kwa mwaka hilo Fungu la kumi?

Na urahisi wa mtaka kutoa kutimiza lengo upo au haupo? Hapa lazima uende nje ya BOKSI ukiweza.
 
Aisee,sikujua hili..
Ila ch kushangaza Wakristo wanatawala Dunia katika kila nyanja!
Sasa kama Wapumbavu wasio na akili wanaitawala Dunia..

Sasa hapo wanaotawaliwa wakoje!
Hatari sana sheikh
 
Dr shoo hii mistari haijui, pamoja na elimu yake
 
Fungu la kumi la kipato cha wiki ndilo hilo hilo fungu la kumi la kipato cha mwaka. Tafuta calculator, sasa hivi zinapatikana japo za mtumba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…