Biblia, kitabu cha ajabu maishani mwangu

Biblia, kitabu cha ajabu maishani mwangu

Jackwillpower

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2017
Posts
2,467
Reaction score
3,687
“Mimi ni BWANA; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu. Tazama, mambo ya kwanza yamekuwa, nami nayahubiri mambo mapya; kabla hayajatokea nawapasheni habari zake.” Isa. 42:8,9.

“Kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi; nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yango.” Isa. 46:9,10.

Utabiri wa Biblia juu ya mambo ambayo yangetokea baadaye, unathibitisha uvuvio wa Biblia, mambo hayo yanapotokea.

Angalia mifano ifuatayo:​

A. Kuinuka na kuanguka kwa falme nne zilizotawala dunia:
Babeli, Umedi na Uajemi, Uyunani na Rumi. (Danieli 2,7,8.)

B. Koreshi kuwa Mpiganaji ambaye angeiteka Babeli. “Haya ndiyo BWANA amwambiayo Koreshi, masihi (mtiwa mafuta) wake, ambaye nimemshika mkono wake wa kuume, ili kutiisha mataifa mbele yake, nami nitalegeza viuno vya wafalme; ili kufungua milango mbele yake, hata malango hayatafungwa. Nitakwenda mbele yako, na kupasawazisha mahali palipoparuza; nitavunja vipande vipande milango ya shaba, na kukata kata mapingo ya chuma; nami nitakupa hazina za gizani, na mali zilizofchwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni BWANA, nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli.” Isa. 45:1-3.

C. Baada ya kuangamizwa, Babeli isingekaliwa tena. “Na Babeli, huo utukufu wa falme, uzuri wa kiburi cha Wakaldayo, utakuwa kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.” “Haya! juu ya mlima usio na miti inueni bendera, wapazieni sauti zenu, wapungieni mkono, kwamba waingie katika malango ya wakuu.” (Isa. 13:19,2). “Na Babeli utakuwa magofu, makao ya mbwa-mwitu, ajabu, na mazomeo, pasipo mtu wa kukaa huko.” Yer. 51:37.

D. Misri kutokuwa na amri tena kati ya Mataifa. “Nami nitawarejeza Wamisri walio katika hali ya kufungwa, nami nitawarudisha hata nchi ya Pathrosi, hata nchi ya kuzaliwa kwao; na huko watakuwa ufalme duni. Utakuwa duni kuliko falme zote, wala hautajifunua tena juu ya Mataifa; nami nitawapunguza, ili wasitawale tena juu ya Mataifa.” Eze. 29:14,15. “Nami nitaikausha mito, na kuiuza nchi, na kuitia katika mikono ya watu wabaya; nami nitaifanya nchi kuwa ukiwa, na watu wote walio ndani yake, kwa mkono wa wageni; mimi, BWANA, nimenena neno hili.” Eze. 30:12,13.

E. Majanga ya kushtua dunia na hofu kadiri tunavyoelekea siku za mwisho. “Tena, kutakuwa na ishara katika jua, na mwezi, na nyota; na katika nchi dhiki ya Mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake; watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika.” Lk. 21:25,26.

F. Kuporomoka kwa maadili katika siku za mwisho. “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako na nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio saf, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.” 2 Tim. 3:1-5.

G. Unabii juu ya matukio katika maisha ya Yesu. “Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika Maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.” Lk. 24:27. “Kwa maana aliwashinda Wayahudi kabisa kabisa mbele ya watu wote, akionyesha kwa maneno ya Maandiko ya kuwa Yesu ni Kristo.” Mdo. 18:28. Kwa kuwa wakati huo Agano Jipya lilikuwa halijaandikwa, ni wazi kuwa Maandiko yanayozungumziwa hapa ni Agano la Kale. Utabiri wa Agano la Kale juu ya Masihi ulikuwa dhahiri na ulitimizwa na Yesu wa Nazareti kiasi cha kumfanya Yesu mwenyewe na Apolo kuutumia kuwathibitishia Wayahudi kuwa Yesu alikuwa ndiye Masihi.

1642851703389.png

1642851745110.png


Moja kati ya uthibitisho mkuu kwamba Biblia si kitabu cha kawaida tu kilichoandikwa na watu wema, ni uwezo wake wa kubadili maisha ya watu. Inaweza kumbadilisha mtu mwovu kabisa na kumfanya kuwa Mkristo mwaminifu. Inaweza kumfanya mtu asiye mwaminifu, kutaka kurejesha alichochukua, au kusahihisha uongo aliosema. Ni uwezo gani wa ajabu ulio katika kitabu hiki unaobadilisha kiajabu matamanio na makusudi ya watu? Ni uwezo wa kufanya miujiza wa Roho wa Mungu anayefanya kazi kupitia kitabu hiki kutuonyesha Mwana–Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu.

Je, ungependa kuielewa Biblia vizuri zaidi?​

Je, utatenga muda maalum kila juma kwa ajili ya kujifunza Biblia? Kwa kutambua kwamba Biblia ni barua ya Mungu inayokueleza mapenzi yake, je, unakusudia kuishi sawasawa na neno lake kama asemavyo katika Biblia?
 
Hakika sio cha mchezo kwani mpaka shetani anahukumu kwa hilo neno la mungu kwani usipo lifuata umepoteza
 
Baada ya Rumi wakafuata England/Anglo Saxons (?) Kisha USA naona zamu ya China inawadia. Tanzania tusubiri zamu yetu maybe 3500 huko tutatawala dunia
 
Baada ya Rumi wakafuata England/Anglo Saxons (?) Kisha USA naona zamu ya China inawadia. Tanzania tusubiri zamu yetu maybe 3500 huko tutatawala dunia
Kwani hiyo 3500 wazambia nao watatawala dunia.
 
Je, ungependa kuielewa Biblia vizuri zaidi?


Je, utatenga muda maalum kila juma kwa ajili ya kujifunza Biblia? Kwa kutambua kwamba Biblia ni barua ya Mungu inayokueleza mapenzi yake, je, unakusudia kuishi sawasawa na neno lake kama asemavyo katika Biblia?
NDIVYO NITAKAVYOFANYA KWA MSAADA WA BWANA
 
Mbona misri wanawasaidia Tanzagiza kujenga bwawa la kuzalisha umeme??? AU ITAKUWA SISIEMU WANAENDA KINYUME NA MATAKWA YA BIBILIA????
 
Mtoa mada najua unaijua vizuri biblia kuniliko naomba nitafutie andiko la kusema kuwa mchungaji akiwa na uhitaji achangiwe "harambee" lakini muumini akiwa na uhitaji aombewee
 
Biblia ni kitabu Cha ajabu sana, kinasomwa kuliko kitabu chochote, kimeuzwa kuliko kitabu chochote, kimetafsiriwa katika lugha nyingi kuliko kitabu chochote, kimepigwa vita kuliko kitabu chochote hata hivyo maadui wa biblia katika vizazi vyote hufa lakini biblia ipo, ni kitabu Cha zamani kisichopitwa na wakati, hili ni Neno la Mungu lisilo na mashaka.
 
Unawapataje hao kwenye zoom?
Unajua zoom meeting?
Wao wanaunda group tuseme watu watano wanapanga kila siku jumamosi saa 2 tunakutana online kudiscuss bible lessons kwa dakika 30 - 45. Hivyo haiihitaji kukutana physically ila wanaonana kwa video conferencing.
 
Mtoa mada najua unaijua vizuri biblia kuniliko naomba nitafutie andiko la kusema kuwa mchungaji akiwa na uhitaji achangiwe "harambee" lakini muumini akiwa na uhitaji aombewee
hakuna
 
“Mimi ni BWANA; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu. Tazama, mambo ya kwanza yamekuwa, nami nayahubiri mambo mapya; kabla hayajatokea nawapaskale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi; nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yango.” Isa. 46:9,10.

Utabiri wa Biblia juu ya mambo ambayo yangetokea baadaye, unathibitisha uvuvio wa Biblia, mambo hayo yanapotokea.

Angalia mifano ifuatayo:​

A. Kuinuka na kuanguka kwa falme nne zilizotawala dunia:
Babeli, Umedi na Uajemi, Uyunani na Rumi. (Danieli 2,7,8.)

B. Koreshi kuwa Mpiganaji ambaye angeiteka Babeli. “Haya ndiyo BWANA amwambiayo Koreshi, masihi (mtiwa mafuta) wake, ambaye nimemshika mkono wake wa kuume, ili kutiisha mataifa mbele yake, nami nitalegeza viuno vya wafalme; ili kufungua milango mbele yake, hata malango hayatafungwa. Nitakwenda mbele yako, na kupasawazisha mahali palipoparuza; nitavunja vipande vipande milango ya shaba, na kukata kata mapingo ya chuma; nami nitakupa hazina za gizani, na mali zilizofchwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni BWANA, nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli.” Isa. 45:1-3.

C. Baada ya kuangamizwa, Babeli isingekaliwa tena. “Na Babeli, huo utukufu wa falme, uzuri wa kiburi cha Wakaldayo, utakuwa kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.” “Haya! juu ya mlima usio na miti inueni bendera, wapazieni sauti zenu, wapungieni mkono, kwamba waingie katika malango ya wakuu.” (Isa. 13:19,2). “Na Babeli utakuwa magofu, makao ya mbwa-mwitu, ajabu, na mazomeo, pasipo mtu wa kukaa huko.” Yer. 51:37.

D. Misri kutokuwa na amri tena kati ya Mataifa. “Nami nitawarejeza Wamisri walio katika hali ya kufungwa, nami nitawarudisha hata nchi ya Pathrosi, hata nchi ya kuzaliwa kwao; na huko watakuwa ufalme duni. Utakuwa duni kuliko falme zote, wala hautajifunua tena juu ya Mataifa; nami nitawapunguza, ili wasitawale tena juu ya Mataifa.” Eze. 29:14,15. “Nami nitaikausha mito, na kuiuza nchi, na kuitia katika mikono ya watu wabaya; nami nitaifanya nchi kuwa ukiwa, na watu wote walio ndani yake, kwa mkono wa wageni; mimi, BWANA, nimenena neno hili.” Eze. 30:12,13.

E. Majanga ya kushtua dunia na hofu kadiri tunavyoelekea siku za mwisho. “Tena, kutakuwa na ishara katika jua, na mwezi, na nyota; na katika nchi dhiki ya Mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake; watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika.” Lk. 21:25,26.

F. Kuporomoka kwa maadili katika siku za mwisho. “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako na nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio saf, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.” 2 Tim. 3:1-5.

G. Unabii juu ya matukio katika maisha ya Yesu. “Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika Maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.” Lk. 24:27. “Kwa maana aliwashinda Wayahudi kabisa kabisa mbele ya watu wote, akionyesha kwa maneno ya Maandiko ya kuwa Yesu ni Kristo.” Mdo. 18:28. Kwa kuwa wakati huo Agano Jipya lilikuwa halijaandikwa, ni wazi kuwa Maandiko yanayozungumziwa hapa ni Agano la Kale. Utabiri wa Agano la Kale juu ya Masihi ulikuwa dhahiri na ulitimizwa na Yesu wa Nazareti kiasi cha kumfanya Yesu mwenyewe na Apolo kuutumia kuwathibitishia Wayahudi kuwa Yesu alikuwa ndiye Masihi.

View attachment 2091663
View attachment 2091665

Moja kati ya uthibitisho mkuu kwamba Biblia si kitabu cha kawaida tu kilichoandikwa na watu wema, ni uwezo wake wa kubadili maisha ya watu. Inaweza kumbadilisha mtu mwovu kabisa na kumfanya kuwa Mkristo mwaminifu. Inaweza kumfanya mtu asiye mwaminifu, kutaka kurejesha alichochukua, au kusahihisha uongo aliosema. Ni uwezo gani wa ajabu ulio katika kitabu hiki unaobadilisha kiajabu matamanio na makusudi ya watu? Ni uwezo wa kufanya miujiza wa Roho wa

Je, ungependa kuielewa Biblia vizuri zaidi?​

Je, utatenga muda maalum kila juma kwa ajili ya kujifunza Biblia? Kwa kutambua kwa

mba Biblia ni barua ya Mungu inayokueleza mapenzi yake, je, unakusudia kuishi sawasawa na neno lake kama asemavyo katika Biblia?

Unajua zoom meeting?
Wao wanaunda group tuseme watu watano wanapanga kila siku jumamosi saa 2 tunakutana online kudiscuss bible lessons kwa dakika 30 - 45. Hivyo haiihitaji kukutana physically ila wanaonana kwa video conferencing.
Hongera mtumishi kwa andiko zuri.
Ndiyo mimi ningependa kuielewa biblia vizuri zaidi
 
Mtoa mada najua unaijua vizuri biblia kuniliko naomba nitafutie andiko la kusema kuwa mchungaji akiwa na uhitaji achangiwe "harambee" lakini muumini akiwa na uhitaji aombewee
[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
 
Back
Top Bottom