Biblia Takatifu: Mathayo 7:22-23 ni angalizo linalohitaji maarifa (Wakristo tupo kwenye mtego mkali sana)

Biblia Takatifu: Mathayo 7:22-23 ni angalizo linalohitaji maarifa (Wakristo tupo kwenye mtego mkali sana)

Oya Tusepe

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2016
Posts
265
Reaction score
870
Matt 7:22-23

"Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako? na kwa jina lako kutoa pepo?, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?. Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."

Andiko tajwa hapo juu ni zito sana, na litawapeleka wakristo wengi kwenye maangamizi mabaya sana. sio jambo jepesi na kwa mtazamo wangu naona kama linahitaji ufunuo mzito.

BWANA ANASEMA watakuja kwake (baadhi ya wakristo) na kumwambia kwamba walilitumia jina lake na wakatenda miujiza mingi,

Msingi wa kwanza hapa ni kwamba watu hawa walidhani mioyoni mwao kwamba walikuwa wanamtegemea Mungu na YESU na si vinginevyo,

Watakuwa wanajiamini kwamba wapo sahihi na watamuendea YESU kifua mbele lakini YESU atawakataa na atasema hakuwahi kuwafahamu kamwe katika kipindi chote.

SWALI

Hawa mabwana wanatenda miujiza kwa nguvu za nani ikiwa ni kweli walidhani wanamtegemea Yesu kumbe sivyo na pia kwa shetani hawapo maana mpaka wanapata Jeuri ya kumuendea YESU ni kwamba wanaamini pasi na shaka mioyoni mwao kwamba YESU atawapokea lakini sasa anawakana.

Je miujiza hii watu wanafanya kwa nguvu za nani? Je mwanadamu ana Nguvu za kutenda miujiza bila kumtegemea Mungu au Ibilis?

Hapa kuna kitu cha kujifunza.
 
Kuna watu wanatumia jina la Yesu lakini nyuma yake Wana nguvu za giza au Imani za Siri Kama Freemason n.k, baya zaidi wanawawekea mikono viongozi wa chini yao ili nao waombee kwa jina la Yesu na miujiza inatendeka, wanatabiri n. k
Sasa hili kundi la pili halijui Siri ya ile miujiza, kwa hio wanaujasiri wa kusema tumeponya kwa jina la Yesu.

Kumbuka jibu la Yesu kuwa sikuwajua kamwe, yaani sijawahi kuwafahamu au kushirikiana na nyie

Zipo Imani ambazo wale top layer ndio Wana makubaliano na shetani, sisi waumini hatujui chochote. Chunguza vizuri Imani yako, usijifariji
 
Kuna watu wanatumia jina la Yesu lakini nyuma yake Wana nguvu za giza au Imani za Siri Kama Freemason n.k, baya zaidi wanawawekea mikono viongozi wa chini yao ili nao waombee kwa jina la Yesu na miujiza inatendeka, wanatabiri n. k
Sasa hili kundi la pili halijui Siri ya ile miujiza, kwa hio wanaujasiri wa kusema tumeponya kwa jina la Yesu.

Kumbuka jibu la Yesu kuwa sikuwajua kamwe, yaani sijawahi kuwafahamu au kushirikiana na nyie

Zipo Imani ambazo wale top layer ndio Wana makubaliano na shetani, sisi waumini hatujui chochote. Chunguza vizuri Imani yako, usijifariji
Hapa utamuibua yule mshindi wa BSS 2009 Pascal Kasiani nae aje kuelezea yaliyomsibu kwamba hao watu hata yeye walimfuata wakam-turn in bila yeye kuelewa kumbe ndio vile
 
Ukirejea sura hiyo ya 7 :18,19
Mti mwema hauwezi kuzaa Matunda mabaya wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri

Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni,

Kwa hiyo sura 7:21,23
Ni maelezo kuhusu hiyo mistari ya juu 18,19
Naona hapa dhumuni kubwa ni kutusisitiza kama wakristo yakupasa kuzaa matunda

Kwa hyo kutoa pepo kufanya unabii kufanya miujiza si zaidi sana ya kufanya matendo mema Kuwaleta wengi kwa Kristo huko ndiko kuzaa matunda hayo ndio mapenzi ya Mungu
Matendo mema /Kuwaleta wengi kwa kristo ni vitu vimpendezavyo Mungu

Maoni yangu ni hayo tuendelee. Kujifunza
 
Mleta maada hapo hawazungumziwi akina mwamposa nop

Hapo tunazungumziwa akina sisi ambao ni wa kristo pure, ambao tukitaka kupeleka watoto wetu shule hutumia jina la YESU KRISTO, ambao tukitaka kufungua maduka yetu na biashara zetu hutumia jina la YESU KRISTO, ambao tukitaka kuoa na kuolewa hutumia jina la YESU KRISTO kupata wachumba, ambao tukitaka kusafiri hutumia jina la YESU KRISTO safarini, ambao tukitaka kulala hutumia jina la YESU KRISTO


Lakini unapokuja kwenye matendo yetu tuna matendo machafu kuliko hata shetani

Ndo maana hapo YESU KRISTO anatoa tahadhar kuwa atatukataa licha ya kwamba utajiri wetu, elimu zetu, wachumba wetu na watoto wetu tuliwapata kwa msaada wa jina la YESU KRISTO lenye miujuza


Kumbe jifunze kuwa MWEMA
 
Kuna watu wanatumia jina la Yesu lakini nyuma yake Wana nguvu za giza au Imani za Siri Kama Freemason n.k, baya zaidi wanawawekea mikono viongozi wa chini yao ili nao waombee kwa jina la Yesu na miujiza inatendeka, wanatabiri n. k
Sasa hili kundi la pili halijui Siri ya ile miujiza, kwa hio wanaujasiri wa kusema tumeponya kwa jina la Yesu.

Kumbuka jibu la Yesu kuwa sikuwajua kamwe, yaani sijawahi kuwafahamu au kushirikiana na nyie

Zipo Imani ambazo wale top layer ndio Wana makubaliano na shetani, sisi waumini hatujui chochote. Chunguza vizuri Imani yako, usijifariji
exactly, umeelewa kama mimi nilivyokua nimeelewa
 
Back
Top Bottom