Biden hakukosea ndio mpango uliokuwepo, ila ametoa Siri kizembe. USA walimshindwa Castro, watamuweza Putin?

Biden hakukosea ndio mpango uliokuwepo, ila ametoa Siri kizembe. USA walimshindwa Castro, watamuweza Putin?

lee Vladimir cleef

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
9,571
Reaction score
35,475
Kwa kifupi Biden hajaropoka TU,Bali amejikuta akitoa Siri kwa kukosa kifua.

Ni kama yule Rais alosema wanajeshi wakiwa vitani halafu akatokea msaliti wanajeshi humshughulikia.mda mfupi baadae Kuna mtu mmoja akamimimniwa vipande vya vyuma mwilini. Rais huyo alijikuta anakosa kifua na hatimae kutoa Siri ya mpanga uliokuwepo nyuma ya pazia.

Joe Biden nae hajajiongelea TU,alichosema ndio kinachopangwa nyuma ya pazia,kwamba kwa namna yoyote Putin lazima atoke madarakani,atoke akiwa hai ama atoke akiwa mfu.

Haya maneno Biden kayatamka kwa kukosa uvumilivu TU,na kwa mawazo yangu ni kuwa Kuna mpango nyuma ya pazia kwa ama nchi za NATO ama USA peke Yao kumtoa Putin.

Kumtoa kwenyewe Ni kutokana na vita hii,wameprovoke vita,wakamwekea vikwazo vya kufa mtu,wakiwasaidia wa Ukraine kwa silaha,ili vita iwe ngumu kwa Urusi.

Kwa vikwazo na vita hii watu wa Urusi wateseke waichukie Serikali ya Putin waandamane na wampondue Putin. Ama matajiri na wafanyabiashara wakubwa waone Kua kua. Uwezekano wa kufilisika na wakuu wa vyombo vya usalama waone hakuna sababu ya vita,na waone ugumu wa vita Kisha kwa Siri waandae mapinduzi ya wazi ama ya kificho. Kumpiga risasi,Sumu au namna yoyote Ile.

LAKINI.
Baada ya vita hii kuanza wananchi wa Urusi wameoneka watulivu na wanafatilia vita hii kwa umakini mkubwa. Njia za kudhibiti ama kupunguza makali ya vikwazo zinachukuliwa kwa umakini mkubwa.

Urusi imesema inafatia kwa umakini mkubwa sana kauli ya Biden. Urusi Ina majasusi Bora kabisa hapa duniani.kwa kauli hiyo majasusi hao kwao hii ni operation mpaya. Ingawa tayari walikua wanajua Kila mipango inayofanyika nje na ndani ya Urusi dhidi ya taifa lao ama Rais wao.

Marekani kwa takrinan miaka 30 walikua wana mpango wa kutaka kumuua Fidel Castro wa Cuba,nchi ndogo na ilio jirani kabisa na USA lakini walimshindwa.na Hadi Fidel alistaafu urais na kumuachia mdogo wake Raul. Na baadae alikuja kufa kifo Cha kawaida kabisa akiwa mstaafu.

Nadhani USA wanatamani sana kumuua Rais wa Korea Kaskazini huyu aliyepo na nadhani walitamani sana kumuua Rais aloepita yaani baba yake na Kim jong UN huyu Rais wa Sasa.

Nadhani USA wanatamani sana kuuangusha utawala wa Sasa wa Iran.

Nadhani Iko wazi kuwa USA wakitaka kumtoa madarakani ama kwa kumuua ama kumpindua na kukimbia nchi raia Assad wa Syria.
Lakini alikingiwa kifua na Urusi.

Nadhani USA wakitaka kumuua ama kumpindua Nikolas Maduro lakini alikingiwa kifua na Urusi.

Sasa Leo mkingia kifua wenzie ndi Biden anataka kumtoa.

Je Leo USA anaweza kumuua Rais Wa Urusi?

Nchi kubwa na yenye majasusi mahili kabisa hapa duniani?

Je wananchi wa Urusi wako tayari kumtoa Putin kwa maandamano?

Ikumbukwe kwamba USA iliwahi kupoteza Rais wake mmoja kwa kupigwa Risasi na watu wasiojulikana.

Haya ni maoni yangu TU jamani.

Mimi nimejaribu kufikiria TU kuwa huenda Biden karopoka Siri iliyokuwepo.
 
Screenshot_20220328-230953.jpg
 
Kwa kifupi Biden hajaropoka TU,Bali amejikuta akitoa Siri kwa kukosa kifua.
Ni kama yule Rais alosema wanajeshi wakiwa vitani halafu akatokea msaliti wanajeshi humshughulikia.mda mfupi baadae Kuna mtu mmoja akamimimniwa vipande vya vyuma mwilini...
Tena jamaa aliyempiga risasi Jf kennedy miezi 3 nyuma alikuwa anaonana kwa siri na sniper mbobezi wa russi,[emoji88]
 
Yes, japo marekani walisema hayo yalikuwa maoni ya Biden na mwenyewe Biden amesema siyo kwamba karopoka it's real kuwa that Russia president lazima atoke.


Tuseme sasa Marekani inajipanga kivita na Urusi.

Naona vita kuu ingine ya dunia ikija.

Naungana na Biden, wamtoe huyu gentleman maana wamama na watoto wanateseka huko Ukraine.
 
Kwa kifupi Biden hajaropoka TU,Bali amejikuta akitoa Siri kwa kukosa kifua.
Ni kama yule Rais alosema wanajeshi wakiwa vitani halafu akatokea msaliti wanajeshi humshughulikia.mda mfupi baadae Kuna mtu mmoja akamimimniwa vipande vya vyuma mwilini...

Niliona Kwenye mtandao sijui Kweli au propaganda kwamba mtu atakaye muua Putin ni binti yake!
 
Marekani na nato wameuwa zaidi ya wanawake na watoto milion 11 Libya, Sirya Afaghanistan Iraq na Yemen
Huwa nashangaa Sana watu wanaomuona marekani mtakatifu,

Maaafa mengi ya kivita yanayoendelea Dunia hii ni fitina za marekani, hataki kuona umoja wowote wenye nguvu, taifa lenye nguvu.

Hivi tushasahau Iraq, Afghanistan,Libya na sehemu zingine marekani ametembeza kichapo kwa interest zake na hakuna kikwazo chochote Wala lawama aliyopokea kutoka mataifa mengine isipokuwa Russia na uchina tu.....!

Russia anapambania usalama wake ambao anaona dhahili marekani anauhatarisha kupitia NATO.
 
Interviewer :”The first motive of assassination is to get inside the security of the president Putin: “I know” “Only God knows our destinies yours & mine” He seems a good guy sema west wanamchafua tu
 
Huwa nashangaa Sana watu wanaomuona marekani mtakatifu,

Maaafa mengi ya kivita yanayoendelea Dunia hii ni fitina za marekani, hataki kuona umoja wowote wenye nguvu, taifa lenye nguvu.

Hivi tushasahau Iraq, Afghanistan,Libya na sehemu zingine marekani ametembeza kichapo kwa interest zake na hakuna kikwazo chochote Wala lawama aliyopokea kutoka mataifa mengine isipokuwa Russia na uchina tu.....!

Russia anapambania usalama wake ambao anaona dhahili marekani anauhatarisha kupitia NATO.

Sio makosa yao bbc cnn sky newz ni sumu na ndio zishawalevya
 
Yes, japo marekani walisema hayo yalikuwa maoni ya Biden na mwenyewe Biden amesema siyo kwamba karopoka it's real kuwa that Russia president lazima atoke.


Tuseme sasa Marekani inajipanga kivita na Urusi.

Naona vita kuu ingine ya dunia ikija.

Naungana na Biden, wamtoe huyu gentleman maana wamama na watoto wanateseka huko Ukraine.
Mbona haushauri Obama na bush wauwawe kwa sabbu walichangia kuua mamilion ya watu katk falme za kiarabu
 
Yes, japo marekani walisema hayo yalikuwa maoni ya Biden na mwenyewe Biden amesema siyo kwamba karopoka it's real kuwa that Russia president lazima atoke.


Tuseme sasa Marekani inajipanga kivita na Urusi.

Naona vita kuu ingine ya dunia ikija.

Naungana na Biden, wamtoe huyu gentleman maana wamama na watoto wanateseka huko Ukraine.

Kwny Hizo nchi hapo chini(Syria,Libya, Afghanistan,Iraq) wamama na watoto walikua wanaenjoy saaana namna USA/NATO walivyokua wakizifanyia nchi zao.
FN-NfsLX0AIzOqJ.jpg
 
Back
Top Bottom