Bidhaa zinazoingiza mapato makubwa zaidi ya kikodi Tanzania 2023/24: Pombe yachangia bilioni 929

Matumizi ya Pombe kwa Busara

1. Pombe kama baraka na furaha: Biblia inataja mvinyo kama sehemu ya sherehe na baraka kutoka kwa Mungu.

Zaburi 104:14-15: "Hukotesha majani kwa ajili ya wanyama... na divai imfurahishe moyo wa mwanadamu."

Mhubiri 9:7: "Enenda, ule chakula chako kwa furaha, na unywe divai yako kwa moyo wa kushangilia."



2. Yesu alibadilisha maji kuwa divai: Katika harusi ya Kana, Yesu alibadilisha maji kuwa divai, tukio lililokuwa ishara ya furaha na uhai.
 
Hakuna Qur'an inayosema hivyo labda hio Qur'an imetungwa US au Israel. We huwezi badilisha Qur'an hata siku moja, Qur'an imehifadhiwa hata na mtoto mdogo wa KISLAM.

Nini maana ya Qur'an 4 129
Al Nisaa(Wanawake)Na haitakuwa katika uwezo wenu kuwafanyia wake zenu uadilifu hata mnavyotamani. Na kwa hiyo, msijiruhusu kuelekea upande mmoja kwa kutomtenga mwingine, na kumwacha katika hali ya kuwa na kutokuwa na mume.
 
Aisee namba 2, 3, na 5 kwa hizi dini za kimagumashi za maboti si wanasema ni haram au dhambi.....sasa je, watahama nchi na kwenda kuishi jehanam watuachie taifa letu tukufu.
 
Hahaha, kwanini tusi hamasishe wapunguze umri wa kuanza kulewa ili kuongeza asilimia ya wajenga nchi. Kundi kubwa la vijana chini ya umri wa miaka 18 wanaweza kusaidia kuongeza hiii idadi kufikia Trilioni kwa mwaka.
 
Hahaha, kwanini tusi hamasishe wapunguze umri wa kuanza kulewa ili kuongeza asilimia ya wajenga nchi. Kundi kubwa la vijana chini ya umri wa miaka 18 wanaweza kusaidia kuongeza hiii idadi kufikia Trilioni kwa mwaka.
Tanzania hakuna umri wa kulewa, kule njombe vichanga vinapigishwa ulanzi vilale wakubwa wafanyekazi. Vikifika miaka 2 vinajitegemeà kulewa.
 
Duuuh watu hawajengi aiseee ,sigara kumbe ina watumiaji wengi sana.
 
Nafaka????
 
Sijaiona bidhaa za Kilimo hapo
 
Yaani pamoja na kupingwa sana na akina Janabi, walokole etc bado bia imeshika nafasi ya pili..!! Sema nini, inasaidiwa sana na kitimoto..!!
 
zinachangia chini ya 50%ya bajeti?
 
Nadhani kuna haja zaidi ya kuwekeza katika unywaji wa pombe maana imeonesha jitihada za dhati katika kuboresha uchumi na hali ya kifedha nchini, nadhani ni muda muafaka sasa waondolewe vikwazo vya kibiashara ikibidi kuruhusu bar zifanye biashara saa 24 ili kukuza pato la Taifa.
Hebu vuta taswira bar zinaruhusiwa kufunguliwa saa kumi jioni na kufungwa saa tano usiku lakini zimeupiga mwingi kiasi hicho, sasa pata picha ndiyo zingepiga kazi 24 hrs.
Pia hapo kwenye mafuta nashauri Serikali ipunguze ama iondoe kabisa kodi kandamizi za uagizaji wa magari kutoka nje ya nchi ili ikibidi angalau kila familia nchini iwe na uwezo wa kumiliki mkweche wake na Serikali ijizatiti katika biashara ya uagizaji na uuzaji wa mafuta nchini, huwezi amini hayo mapato yatakayopatikana tunaweza tukajenga hospital za rufaa zenye hadhi sawa na MNH kwa kila Wilaya nchini.
Tuachane na dhana kuwa eti tukishusha kodi ya uagizaji wa magari tutageuka kuwa dumping state au miundombinu haitaweza kumudu kuhimili ongezeko hilo maana ni akili mgando pekee ndiyo inayoweza kuwaza hivyo wakati return itakayopatikana katika biashara ya mafuta na vipuri inaweza kutufanya tukapaa kiuchumi kuliko tunavyodhania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…