Biharamulo: Kampeni, kura na matokeo!

Hivi hawa FFU huwa wanaonekana tu wakati wa kampeni na kuchukulia hatua upinzani peke yake?
 
CHADEMA MATATANI BIHARAMULO -
Kwa mujibu wa mfanyabiashara maarufu mjini hapo, John Rwegasira ambaye pia ni mhamasishaji wa Kampeni wa CCM, .

Oscar Mukasa aka Rwegasira and John Rwegasira - incidence, coincidence or maneouver ?
 

CCM yafanya kampeni kwa mbwembwe Biharamulo
Frederick Katulanda, Biharamulo
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) juzi jioni kilifanya kampeni zake huku Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama hicho, Mfaume Kizigo akitangaza kuwa vijana wake wako tayari kuwashughulikia watu watakaoleta vurugu kwenye jimbo hilo.

Mkutano huo wa kampeni za CCM ni wa kwanza kufanyika katika mji wa Biharamulo mjini tangu Juni 10 mwaka huu, kampeni zilipoanza ambapo Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ndicho kilikuwa cha kwanza kufungua kampeni zake katika mji huo, wakati CCM ilizindulia katika mji wa Nyakanazi.

CCM ilifanya mkutano huo siku moja baada ya Chadema kuitisha mkutano wa wandishi wa habari katika ofisi yake ambapo ilikilalamikia Chama Cha Mapinduzi na polisi kwa tuhuma za kuuhujumu uchaguzi huo.

Hata hivyo juzi hiyo, vijana wa CCM walianza hamasa saa 12: 15 aubuhi , baada ya kundi la vijana wapatao 35 kupita katika kona za mji huo wakikimbia mchakamchaka na kuimba nyimbo za mafunzo ya mgambo huku wakiwa wamevalia sare za CCM.

Ilipotimu saa 6:20 mchana, kundi lingine la vijana 20 likiwa na bendera ya Chama hicho, lilianza kupita tena, likikimbia mchakamchaka, huku likiimba nyimbo zenye maneno mengi ya kuchekesha yakiwemo ya "Tutawashughulikia wapinzani mpaka wakione cha moto na mgombea wake apandwe presha ama aharishe’.

Wakati kundi hilo likiendelea, mkuu wa kitengo cha propaganda Tambwe Hiza yeye alikuwa akisaidiana na baadhi ya vijana wengine wa chama hicho kugawa Magazeti ya 'Sauti huru na Nyundo' ambayo yalichapishwa habari nyingi za kuviponda vyama vya upinzani.

Mkutano wa CCM ulianza saa 9:30 ambapo wa kwanza kupanda jukwaani alikuwa Kizigo ambaye alisimama na kusema kuwa yeye kama mkuu wa vijana wa chama hicho hayuko tayari kuiacha Tanzania huru na Biharamulo ikichafuliwa amani na vijana wa Chadema na hivyo kusema vijana wa chama chake wamejipanga kikamilifu.

Alisema “Jana Chadema wamefanya mkutano hapa wakasema kuwa tunawamwagia tindikali, tuna mapanga na tunatembea na magobole, sasa nataka kuwaeleza kuwa CCM ni chama cha amani lakini hatuko tayari kuona vurugu na vijana wangu watawashughulikia wakianza vurugu”, alifafanua.

Naye mbunge wa Bukoba Mjini Balozi Hamisi Kagasheki ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, alisema CCM imekuja kwa heri kugombea katika jimbo la Biharamulo na kuwataka wananchi kuepuka vurugu na matusi ambayo alidai kuwa yamekuwa yakitolewa na vyama vya upinzani kwa kumchagua mgombea wa CCM.

“Mkiona watu wanakuja kwa shari na matusi mjue kuwa hao wameishiwa sera na wamefilisika, mimi nimekuja kwa niaba ya wabunge wote wa CCM mkoa wa Kagera kuwaomba mtuchagulie mgombea Oscar ili tuweze kuwaletea maendeleo,” alieleza.

Kagasheki alisema yeye alimfahamu mgombea huyo tokea akiwa nchini Holland alikokuwa akisoma na kwamba ndiye aliyemshauri kurudi Biharamulo kugombea na kumwelezea kuwa ni kijana makini na msikivu ambaye anapaswa kuwa mbunge.

Akizungumza kumnadi mgombea wa chama chake Naibu Katibu Mkuu wa CCM George Mkuchika, alisema mgombea wake amekuwa tishio kwa Chadema, jambo ambalo liliwafanya kumsingizia kuwa siyo raia ya Tanzania ili aenguliwe uwanja wa uchaguzi kwa kumhofia kuwa atawashinda.

Naye mgombea wa CCM, Oscar Rwegasira Mukasa akijinadi kwa wapiga kura alieleza kuwa jimbo la biharamulo kwa sasa linahitaji mbunge kutoka CCM kwa vile kwa muda limekuwa nyuma kimaendeleo kutokana na kuwa na mbunge wa upinzani na hivyo kuwaomba wananchi wamchague yeye kwa vile amedhamiria kuwaletea maendeleo kwa kushirikiana na wabunge wenzake wa CCM mkoani Kagera.

Alisema iwapo watamchagua yeye ataanza kushughulikia suala la maendeleo kwa kusimamia mpango wa maendeleo wa Halmashauri ya wilaya ikiwa ni pamoja na kukutana na walimu wa shule ambao alidai kuwa wamekuwa wakifundisha katika mazingira magumu..

Alisema mbali na suala la walimu atahakikisha kuwa vijana wanapata fursa ya kukopa katika taasisi za mikopo kwa kushirikiana na wizara husika na kuwasihi wananchi kuhakikisha wanamchagua yeye kwa vile ni mgombea wa CCM yenye ilani ya uchaguzi inayotekelezeka.

Mkutano huo wa CCM ulihitimishwa kwa maandamano ambapo viongozi wa CCM waliwatangazia wananchi kuwa baada ya mkutano huo wananchi wamsindikize mgombea wao ambaye atatembea kwa mguu kuelekea ofisi za chama.


Source: Mwananchi Read News
 
Taarifa tulizo nazo ni kwamba
Mhe. Yusuphuh Makamba na Pius Msekwa wameondoka Biharamulo kimya kimya. Vyanzo vyetu havijapata sababu haswa za kuondoka kwa wakuu hao wa CCM katika kipindi hiki kigumu cha kampeni.

.

Ukweli wa wao kuondoka na sababu za kuondoka vimepatikana?
 

Matanzania wewe ni ccm bendela kama sauti ya umeme. Sijawahi kuona hata siku moja umeweka kitu ambacho ni positive kwa chadema. HJili swalai ni kwa nia njema kabisa nataka kujua
 
lyatonga kweli shushushu haachi kazi mpaka kiama leo anaikampenia ccm.
 
huyo mrema anafaidi matunda ya waislam waliomkalia itikafu baada yeye kujiona mUngu Mtu wa Tz alipopewa uwaziri wa Mambo ya Ndani sasa anaanguka tu kisiasa na sasa anaanza kuanguka bafuni
 
Huyu Mzee wa Kiraracha -- nilimsapoti sana 1995. Katu siningefanya hivyo kama ningekuwa na uwezo wa kutabiri ya mbele. Angefanikiwa kuula urais, hadi leo hii angekuwa rais, wengi wangekufa au kutupwa jela, na katiba angebadilisha kuondoa ukomo wa vipindi au kuweka sheria ya yeye kuwa rais wa maisha.

Na hawa viongozi wa TLP -- hawawezi kuzinduka na kumwondoa? anawahonga nini, iwapo hali yake no hohehahe?
 
Ukweli wa wao kuondoka na sababu za kuondoka vimepatikana?

Uhakika kwa sasa tunao. Alitoa maelekezo kadhaa kwa watendaji wa serikali akiwepo Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Biharamulo Magh. kwamba ni lazima mgombea wa CCM ashinde la siyo ajijue kuwa hana kazi. Hayo hayo katoa kwa OCD. Pia walimu wakuu wa mashule yenye vituo vya kupigia kura wamepigwa mkwala kwamba kama CCM itashindwa kwenye vituo vya shule zao wataona cha moto.

Jana Diwani wa Viti Maalum ambaye ni mke wa diwani pia alitoa agizo kwa genge maalum la kutesa wapinzani kwamba mhamasishaji wa CHADEMA atekwe nyara na akapelekwa porini ambako alipigwa kwa muda wa nusu saa. Mhamasishaji huyo alituhumiwa kwa kosa la kuwashawishi wafuasi wengi wa CCM wakajiunga na CHADEMA.

Mhamasishaji huyo ameletwa leo mjini Biharamulo na kukimbizwa Hospitali Teule ya hapa mjini ambako anapata matibabu.

Polisi walipopelekewa malalamiko hayo na viongozi wa CHADEMA ili wakamkamate huyo diwani, wamewataka viongozi wa CHADEMA wakamtafute Mhe. Diwani ili walimalize jambo hilo eti KIDIPLOMASIA.
 
Kujenga demokrasia ni safari ndefu.inahitaji patiency ya hali juu kama walivyofanya waimbambwe.Naomba sana wanaharakati wafanye sensitisation ya hali juu kwa wananchi wa Tanzania.Hii stage tulipofikia haina tofauti yeyote ya nchi inayopitia transistional democracies.Hivi tumeanza kupata machungu, ambayo hatimaye tutavuka kipindi hiki kigumu cha manyanyaso kama walivyofanya Zimbabwe.
Makamanda wetu Mh.Mbowe,Zitto,John Mrema,Tundu Lissu,John Mnyika,Kiwanga n.k.Dalili za mafanikio zimeanza kuchomoza ndio tafsiri ya kuweweseka kwa hawa wakiritimba CCM.
Wameshaatamia mzoga hawawezi kuachia kirahisi bila kupitia machungu!
 
Leo asubuhi kuanzia saa 4.00 hadi saa 4.50 kikosi cha askari wa polisi wakiwa na silaha za aina mbali mbali walishiriki zoezi la kufanya upekuzi mkali kwenye gari moja linalotumiwa na John Mnyika katika kampeni hapa jimboni Biharamulo.

John Mnyika anaratibu kampeni katika kata ya Rusahunga ambayo ni ya pili kwa ukubwa (ina wapiga kura zaidi ya 16,200) Katika kata hiyo, CCM wana hali mbaya sana

Polisi walianza mtafaruku na Mnyika baada ya kutuhumu kuwa vijana wa CHADEMA katika kata hiyo wakiwa pamoja na dereva wa gari husika waliwafanyia vijana wa CCM fujo na kuwapa kipigo kikali.

Gari iliyokuwa ikitumika huko Rusahunga ililala katika Hotel ya Roberts hapa mjini Biharamulo. Polisi wa Kikosi cha kutuliza ghasia walilinda gari hilo hadi asubuhi. Polisi hao na makada wa CCM walieneza uvumi kuwa gari hilo la CHADEMA lina mabomu, mapanga na visu ndani yake.

Asubuhi hiyo mkuu wa kamandi ya FFU Tanzania na RPC Kagera wakaamuru gari hiyo ya CHADEMA ikafanyiwe upekuzi.

Wakati huo viongozi wa CCM akiwepo Dr. Deodarus Kamala walikuwa katika Hotel iliyoko karibu kabisa (mita 50 hivi) iitwayo White House ili kupokea kwa shangwe taarifa za CHADEMA kupatikana na silaha katika gari yao.

Upekuzi ulisimamiwa na Inspector Omary kutoka makao Makuu ya Jeshi la Polisi na kushuhudiwa na Mashinda na Basil Lema kutoka CHADEMA na kijana mmoja Hamisi wa Roberts Hotel. Kilikuwepo kikosi cha askari wenye silaha na kuvalia kofia za kutuliza fujo wapatao 20 pamoja na wananchi wengi waliokuja kushanga kuna nini?

Hatimaye upekuzi umehitimishwa kwa kukuta kuwa gari hilo halikuwa na kitu chochote cha hatari.

Ama kweli CCM wameamua kufanya kila hila kuwapachika CHADEMA tuhuma za ujasusi.
Lakini Mungu Mkuu: ukweli umeonekana!!!!
 
they are days are numbered ..no suprise to see they are doing all that
 
Huyo Kamala anafanya nini badala ya kuwa Bungeni? Upepo wa Kisiasa ukoje lakini ? CCM watarejesha jimbo?
 
Last edited by a moderator:

huo ni mwanzo tu, kama kweli ccm imeamua kuwafanyia hila wasishangae siku moja wanaamka na kujikuta wamebebeshwa mabomu kwenye magari yao.tena hapo biharamulo ni jirani na rwanda na burundi kwahiyo mabomu na silaha zinauzwa tu kama nyanya pale buguruni.
 
Sasa mlitaka polisi wasifanye kazi yao? Sioni ubaya wowote wa walichofanya polisi. Wabaya ni hao waliotoa hizo taarifa. In fact ningewalaumu polisi kama wasingelikagua ipasavyo hilo gari.

Huku wenzetu wanafunga mitaa kwasababu tu kuna mtu amesema kuna kifurushi kisicho na mwenye nancho ndio iwe habari za silaha kama mapanga?

Polisi wakifanya kazi zao mnalaumu, wasipofanya pia mnalaumu. Ni bora watu kupata usumbufu wa saa moja kuliko kuacha madhara yatokee.
 
Hapana shaka kuwa kuna kila dalili za CCM kuleta vurugu kama zile za Busanda..!! Hivyo baada ya Kujua kuwa maji yamefika shingoni, hivyo Huyu Kamala huko anafanya nini?? Mbona Hajakaguliwa hawa watu wa CCM. Siku zao zinahesabika bwana,
 
Hapana shaka kuwa kuna kila dalili za CCM kuleta vurugu kama zile za Busanda..!! Hivyo baada ya Kujua kuwa maji yamefika shingoni, hivyo Huyu Kamala huko anafanya nini?? Mbona Hajakaguliwa hawa watu wa CCM. Siku zao zinahesabika bwana,

Huruma yangu huwa ni kwa polisi walivo pigika lakini wanazidi kusaidia watu wanao wafanya wapigike.

Anyway, Mungu yupo kuna siku haya yataisha, itafikia mahali hata vitisho hujuma na hila zote zitashindikana na haki itachukua mkondo wake.
 

Tatizo la Jeshi la Polisi ni kwamba huwa wanafuatilia tuhuma za upande mmoja tu. Wangekuwa wanafuatilia tuhuma za pande zote basi hakuna mtu ambaye angelalamika wala kupiga kelele.

Hivi majuzi huko Busanda kuna wana CCM walishikwa na polisi na walikiri kwamba walikuwa wakinunua shahada za kupigia kura, leo hii ukienda Busanda hakuna hata kesi moja iliyo mahakamani.

Je, bado tuendelee kuliamini jeshi la polisi ambalo limekuwa likishiriki kulinda "amani na raia ambao ni wana CCM" kwa kuangalia maslahi ya CCM?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…