Biharamulo: Kampeni, kura na matokeo!

Kwa sasa vituo ni tupu na hakuna kinachoendelea. Wakati tukiisubiri hiyo saa 10 ifike zoezi la kuhesabu kura lianze, sio vibaya nikawamwagia data chache kuhusu Biharamulo.
Ina eneo la kilomita za mraba zaidi ya elfu 5 na wakazi wanaokadiriwa kufikia zaidi ya laki 2. Kati yao Wasubi ndio wengi zaidi ya 35%, Waha 25%, Sukuma 20% na Wahaya 10%.
Profile ya Biharamulo inaonyesha wana utajiri mkubwa wa kilimo, mifugo na uvuvi mpaka wameweka data za mavuno, cha ajabu wametaja tuu kuhusu mgodi wa dhahabu wa Tulawaka lakini hakuna data zozote zinazoonyesha kunapatikana nini, inawezekana hata mrahaba unaishia kwenye matumbo ya watu.

Pia kunaonekana kuna shule 16 za sekondari ila haijaelezwa kama zinafika form six au zote zinaishia form four.
Yaani Biharamulo ina kila dalili za neema, ardhi nzuri yenye rutuba, madini, maeneo ya malisho, bado sipati picha huu umasikini wa Biharamulo unaletwa na nini!?.
 
Nikutana na mtaalam wa siasa za Biharamulo amenieleza WanaBimulo zao ni kufanya mambo kimya kimya, Chadema kama kawaida yake ndie mtawala wa maeneo ya mijini kwa wajanja na watu waliochangamka, CCM nayo kama kawa, wamewakumbatia wajumbe wa nyumba kumikumi. Kuna nyepesi nyepesi ambazo hazijathibitishwa na hakuna namna ya kuzithibitisha ni kuwa jana baada ya kufungwa kwa kampeni, misimbazi ilitawanywa kwa wajumbe wa nyumba kumikumi na 20,000 ya chenji chenji noti za 2,000 zikielezwa ni nauli ya kujia kwenye vituo vya kupigia kura leo asubuhi, kabla ya hapo kulitolewa madai kuwa kiongozi mmoja wa chama fulani alikwenda benki Biharamulo akiwa na Shilingi milioni 60 alizotaka chenji ya buku mbili mbili, benki wakawa hawana, wakaagiza chenji toka Bokoba!.
Huyo mtaalamu wa siasa za Bi'mulo anasisitiza wana Bi'Mulo sio WanaBusanda, fulana watavaa, kofia watajikingia jua na vumbi, fungu likimwaga watapokea, ila kura watampigia yule waliyeshamchagua.
Hawa jamaa ni wakimya cha ajabu, hata hamasa kuwa kunafanyika uchaguzi hakuna, vituo vya uchaguzi viko tupu, jamaa hawazungumzii siasa zozote mitaani ni kimya kimya.Saa kumi ndio hii, naanza kutembelea tena vituo kushuhudia zoezi la kuhesabu kura.
 

Mkuu Pasco asante sana kwa updates, tunategemea utaendelea tumwagia matokeo kadri utakavo kuwa unayapata!
 

Wakitimiza huo msimamo wao(ktk bold line) basi watakuwa wametufundisha sisi wa mjini bonge la shule.
 


they are capitalizing in ignorance and poverty of majority of the populations in general......ndio maana mkuchika huwa anawaambia ..wapinzani ni mahodari mijini na kwenye magazeti.....kwani huko vijijini hata magazeti yakifika wadanganyika kwa umaskini wao hawawezi kumudu shilingi 400 kununua gazeti!!.....siasa za kwenye televisheni ..vijijii hawana umeme...hiyo RTD yenye national coverage ndio hiyo.....tunayo safari ndefu...ndio maana ccm hawataweza fanya "kosa" kuondoa ufukara vijijini au kupeleka elimu ya uraia kwani siku raia wakiwa na uwezo hawataichagua..

naona safari hii CHADEMA wamefanya mabadiliko makubwa kwenye aina ya kampeni wanazofanya....crown pulling campagne ni ngumu kwa sababu wengi wa vijana wanaokuja kushangilia aidha hawakjajiandikisha au wameshauza shahada...kazi ipo !!
 
Inaonyesha safari hii hakuna kelele nyingi kama Busanda kwanini? au CCM wanauhakika zaidi au ni aina ya watu wanao deal nao?
 
kwanini mnagawa watu kwa makabila kama wamerakani wakiwa vitani? mimi niko-against ya kucategorize watu kwenye makabila kwa asilimia huo ni ujinga ambao tutakiwa kuepukana nao!
 

Wakimbizi na mamluki kibao huko. Huwezi kuongea ukiwa nchi nyingine kama huna uhakika na uraia wako.
 
Wakimbizi na mamluki kibao huko. Huwezi kuongea ukiwa nchi nyingine kama huna uhakika na uraia wako.

Uraia sio tataizo as long as wewe ni mwanachama wa chama cha wenye nchi, hata uwaziri mkuu unaweza kupewa tu! Only in Tanzania.

Yes, ukitaka mambo yako yakunyokee wewe kuwa mmoja wao!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…