Biharamulo: Kampeni, kura na matokeo!

Wananchi wa Biharamulo watakuwa wamepoteza mweleko iwapo watajaribu kukichagua chama chenye sera ya kunyanyapa wananchi.

Chama hiki ni aibu ya mwaka kwa kujaribu kuwarubuni wakinamama kwa chupi na sidiria!
 
Swali kubwa ni jee -- CUF wataingia kwenye kinyang'snyiro? Wako kimya au labda wanangojea mapesa kutoka CCM -- yaani kwa kuzingatia Profesa-Jussa-RA clique? Si mnaielewa lugha ya Profesa siku hizi kuhusu masuala ya ufisadi?

Waliingia Busanda kujaribu kuiharibia Chadema -- lakini haikuwa haja -- kwani kuzoa kura 900 tu huwezi kusema kamharibia mtu yoyote.

Lakini pamoja na kwamba CCM itashinda kule kutokana na incumbency na pia kuwa na strong candidate (inavyodaiwa) lakini ni lazima Chadema watoe upinzani mkali ili kujipima hasa kwa kujaribu kukosoa utendaji wa CCM na hasa kuwaelimisha wananchi jinsi ufisadi ulivyokithiri -- kuonyesha kuwa hiyo issue ndiyo sababu kubwa inayochangia umasikini wao.

Ndiyo tutaihitaji Chadema kufanya kazi hiyo kwani CUF, TLP na CMM hawaiwezi hiyo kazi.

Tuliona jinsi Mama Kilango alivyokuwa akipata taabu jukwaani huko Busanda alipokuwa anajaribu kukiosoa chama chake kuhusu ufisadi -- hadi masikini wakamzomea -- kwani wananchi waliona vita dhidi ya ufisadi haiwezi ikawa agernda ya CCM -- agenda ya chama hichio ni kinyume chake.
 
 
1.- Heshima mbele mkuu, hivi huko Biharamulo si hakuna mbunge toka Mh. Kabuye alifariki, na besides si alikuwa mbunge wa TLP, sasa incumbency ya CCM huko inatokea wapi mkuu?
***********
2.- After all this, hawa wananchi wakaichagua CCM anyways, something is not right hapo au?

_____________________________________

FM ES:

1. Incumbency hapa nilimaananisha serikali iliyopo ni ya CCM - incumbent party. samahani kama sikueleweka.

2. Mkulu, sikusema kama issue ya ufisadi ndiyo ili-play katika kutoa final results. Nilikuwa na-imply tu namna issue hiyo ilivyohamasisha wananchi hadi kuwazomea wapiga debe wa mgombea wa CCM.
*************

 

- Sawa sawa mkuu nimekusikia na umeeleweka sasa.

Respect.

FMEs!
 
Muhimu ni hilo swala la upinzani kusimamisha mgombea mmoja.

Hilo haliwezi kusaidia katika chaguzi ndogo labda Tarime na Karatu kwani ccm inahamishia raslimali zote za taifa kwenye jimbo moja. Mfano mzuri ni Busanda. 2010 inawezekana kwa sababu, Magufuli, Masha, Chiligatiwa, Malechela(japo ni mbunge wa maisha wa jimbo la Mtera na wengineo watakuwa majimboni mwao wakihangaika.
 

- Yaani kutokuungana kwa upinzani ni kosa la CCM?

FMEs!
 
Muhimu ni hilo swala la upinzani kusimamisha mgombea mmoja.

Hilo ndilo million dollar question watu wana jiuliza kila siku. Kuungana kina taka wahusika wawe na nia moja na wakubali lazima kuwepo viongozi na wanao ongzwa. Na hata hao wanaoongozwa kuna mwenye cheo cha juu zaidi na mwenye cha chini zaidi. Wapinzani wasimamishe mgombea mmoja na wakati kila mmoja wao ana taka kuongoza? Sehemu uta kayo ona upinzani wameungana kum simamisha mgombea mmoja hapo ujue vyama vingine vime kubali kwa sababu wana jua hawana nafasi yoyote ya kushinda. Tukija kwenye kuungana kitaifa hilo ndiyo kabisa litakua kazi. Nani aongoze huo muungano na nani awe mgombea uraisi wao? kila mmoja ata taka kuwa kiongozi. Kabla ya vyama vya upinzani kuungana kwa upinzani kwanza wana bidi wajue nani ana nguvu wapi na nani anafaa katika nafasi ipi. Kama fulani ndiyo ana uwezo wa kuwa mwenyekiti bora basi apewe yeye bila wengine kuleta vizingiti. kama mwingine ndiyo ana uzika kwa wananchi basi huyo ndiyo apewe nafasi ya kugombea iwe udiwani, ubunge au urahisi. Kwa sasa upinzani kuna tamaa mno ya uongozi kitu ambacho kita zuia muungano wowote wa maana.
 

Asante Pasco kwa kuwa mstari wa mbele kutuhabarisha kuhusu hizi chaguzi ndogo. Natumaini mchango wako utakuwa mkubwa kama Busanda.

Kwenye nukuu hapo juu sikubaliani na hitimisho na utabiri unaofikia kutokana na hitimosho hilo. Nakubali umoja ni nguvu, ila inategemea kama vinavyoungana vinafanana au vinalingana walau kidogo. Mfano Busanda, hata ukichukua kura 900 na kitu za CUF ukachanganya na za UDP bado CCM wanashinda. Pili hakukuwa na kugawana kura nyingi. CHADEMA elfu ishirini na zaidi, CUF na UDP hata elfu moja hawakufikia, sasa huko kugawana kura nyingi kuko wapi?

Kuna mifano mingi kuonyesha swala sio kuungana tu. Mfano mwaka 2005 Jimbo la Ulanga magharibi alisimama Prof. Mlambiti (TLP) peke yake na Prof. Ngasongwa (CCM). lakini CCM walishinda sio kwamba Prof. Mlambiti alikuwa hakubaliki ila kona za CCM ni nyingi.

Swala sasa ni vyama vya upinzani kupitia upya sera zao, kujijenga katika ngazi za chini na kupigana zaidi. Siamini katika kuunganisha nguvu bila walua kuwa na uwezo, mwelekeo na nia zinazoshabiihana.

Tatizo sio vyama kuungana, tatizo ni bado mwamko wa mageuzi haujawagusa wengi. Hili linakuja. Njaa zetu zinavyozidi tutaanza kujiuliza kama kweli huyu baba ni wetu au wa wengine.
 
Kwa mtazamo wangu, naamini wengi ambao hawakupiga kura ni wafuasi wa CUF na UDP ambao walisoma dalili za nyakati kuhusu uwezekano wa vyama vyao kushinda, walipoona hawawezi kushinda, wengine wakasusa na wengine wakaichagua CCM katika ule mtindo wa adui wa adui wako ni rafiki yako. CCM na Chadema ndio maadui, kwa CUF waliokubali kushindwa kuna waliiona kuwa badala ya kuwaacha Chadema washinde, bora waipigie kura CCM.
Hoja ya mwamko wa mageuzi ni hoja nyeti sana ndio maananasisitiza civic education, Wanabusanda wa interior wasiojua Kiswahili, kusoma wala kuandika, njaa kali, hakuna umeme wala maji, barabara usiseme, wataelewa nini kati ya wimbo wa Chadama wa vita dhidi ya ufisadi na aliyepitisha kilo ya sukari usiku kabla ya uchaguzi?
 
Hizi politik za wapi jamani? kwa nini kuungana vyama wakati kila mmoja ana sera na maono yake? Kila mmoja aingie kivyake. Wananchi kama wanadhani watapata maisha bora chini ya wezi hawa wa chama chao wawape na waendelee kuumia
 
Kuna watu walinotisi mara moja mabadiliko ya kutoka kutumia jina la "Mukasa" kwenda kwa "Rwegasira"... well

Na Frederick Katulanda, Mwanza (Mwananchi)

WAKATI kampezi za uchaguzi mdogo wa kiti cha ubunge katika Jimbo la Biharamulo Magharibi zikiwa zimeanza, mgombea wa CCM katika kinyang’anyiro hicho, Oscar Rwegasira, amewekewa pingamizi kwa madai kuwa si raia wa Tanzania .

Habari kutoka Biharamulo na ambazo zimethibitishwa na Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, Zuberi Mbyana, zilisema pingamizi hilo limewekwa na mgombea wa Chadema Dk. Anthony Mbassa.

Mgombea huyo wa CCM, aliteuliwa baada ya kuwashinda wapinzani wake katika kura za maoni kwa kupata kura 309.

Walioshindwa katika hatua hiyo ni na kura zao katika mabano ni, Agricola Magotto (120), Mwajemi Mustapha (23), Hassan Rwabudongo (15), Mussa Matata (10) na Nitibihora Burchard (5).

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Mbyana alikiri kupokea pingamizi hilo na kwamba tayari ofisi yake imekwishamwandikia mgombea wa CCM, kumtaka kujibu pingamizi hilo.

Alisema katika pingamizi hilo, mgombea wa Chadema anadai kuwa mgombea wa CCM, hana sifa za kuwania nafasi hiyo kwa sababu si raia wa Tanzania.

Alisema kwa mujibu wa mweka pingamizi, mgombea wa CCM ni raia wa Uganda na kwamba wazazi wake wote wa wawili walitoka Uganda.

Msimamizi huyo alisema mgombea huyo wa Chadema anadai kuwa wazazi wa mgombea mwenzake, hawajawahi kuomba uraia hapa nchini.

“Barua tuliyomwandikia mgombea wa CCM ni yenye kumbukumbu namba BBC/30/3/Vol. X/114 ya Juni 10, 2009 ambayo nimemtaka ajibu tuhuma za pingamizi alilowekewa na Chadema” alisema msimamizi huyo.

Mkuu wa operesheni ya uchaguzi wa Chadema, John Mrema, alisema katika pingamizi hilo, Chadema wamebaini kuwa mgombea wa CCM, ameshindwa kueleza mahali alikozaliwa.

“Baada ya kubaini hilo na kufuatilia uhamiaji na kwingineko, wamebaini kwamba wazazi wake mgombea huyo walingia nchini mwaka 1971 wakitokea Bunyoro nchini Uganda na kuishi eneo la Misenyi,” alidai Mrema.

Alidai kuwa mgombea huyo wa CCM, alizaliwa Uganda mwaka 1970 na si katika kijiji cha Rukalagata Biharamulo kama anavyodai.
 
Harufu ya Mbeya vijijini hiyoooooooooooo! kama hii habari itathibitika kuwa kweli, lakini je CCM watakuwa tayari kukubali yaishe??? Maana akina Tambwe Hiza, Makamba hizo kampeni ni sehemu ya ulaji!
 
Chama makini kama CCM kinaweza vipi kumteua mtu ambaye si raia? So nadhani hili haliendi mbali. CCM haiwezi kumpendekeza mtu awe Mbunge wakati si Raia
 
CCM cyo chama makini hata kidogo. kingekuwa makini kama mafisadidi wote wangefukuzwa uanachama na wawepo segerea au keko.
 
Ile kutoka Mukasa kuja Rwegasira ilikuwa ni ishara tosha, lakini mbona Matayo david Msuya alivyobadili kuwa Matayo David Matayo hakukuwa na angalizi ama kwa kuwa yote ni majina ya kitanzania? Mukasa aje na vielelezo vya uraia wake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…