Biharamulo: Kampeni, kura na matokeo!

Biharamulo: Kampeni, kura na matokeo!

Masanilo
FMES huwa ananifurahisha sana CCM ikiwekwa angle mbaya.This time wanalo,Mukasa hebu tueleze,kulikoni gafla bin vuu ukawa Rwegasira?

Ni kweli naona ni vizuri mamba tukimuita mamba. Tusimuite Kenge. Lakini tukumbuke kuwa inapofika swala la CCM, maslahi yake yanakuwa mbele zaidi kuliko maslahi ya Taifa. Kuna mifano mingi tu ya watu wenye utanzania wenye utata, lakini kwa kuwa wanaCCM au kwa kuimba nyimbo za CCM wanakuwa WATANZANIA, wakibadilika kidogo tu basi wanakuwa siwatanzania. Hii tutake tusitake ni mbegu iliyopandwa na CCM kwa watanzania, si ajabu kama ikiota kama ilivyopandwa.
 
Kwani Katiba inasemaje? Kama katiba imeonyesha dhahili nani anae qualify kuwa Mtanzania kwa nini tuipinge?

Kwani ni mbunge tu ndiye anayestahili kuwa mtanzania? Mbona huu uzalendo hatunao kwenye nafasi nyingine? Mbona hatusikii tarishi kwenye ofisi ya serikali akisakamwa kuhusu uraia? Ni unafik kumuachia mtu asome, atumikie taifa hili kwa nguvu zake zote halafu vup bin vuu mara tunataka kujua uraia wake!

Amandla..........
 
- Sasa baba yake alifikiaje kufanya kazi kwenye serikali yetu mpaka kuwa ofisa wa juu huko wilayani na mkoani bila kua raia wetu? It does not add up!

Respect.

FMEs!

wakati wa nyerere nadhani hakuwa akifuata sana hayo mambo ya uraia, akiona wewe ni potential na uko tayari kulitumikia taifa basi unaishi na kuwa kama raia wako wengi tu hasa Wamalawi, Zambia, Warundi na Waganda
 
JAMANI nadhani swala la uraia watu tumeshaliongelea hapa mpaka sheria na misahafu ikatundikwa humu. Kikubwa hapa naomba tujue kwamba..kila mtu anayo haki ya kubadilisha jina lake na kuitwa anavyotaka. Hata kama angeamua kuitwa Chungwa au embe...its him! Unless proved otherwise.

Nategemea watu humu JF tulijadili swala hili objectively. Kwanza, lazima tujue kabisa watu wengi wa Tanzania especially wa mikoa iliyo pembezoni mwa nchi kama Kagera, Kigoma, Mara nk..wengi wa wananchi wana connection na nchi jirani either kwa lugha au undugu. NA HILI ni purely geographical accident halikwepeki. Mtu wa Kigoma au Ngara definitely yuko closer na mtu wa Burundi kuliko mtu wa Rukwa kwa sababu ambazo ziko wazi kabisa. Wanaongea lugha moja! So is mtu wa Mara na mtu wa Kenya. But kasumba ambayo tunaiendekeza especially wabongo wengi..ni kuwaona raia wa hizi sehemu kama warwanda au warundi..simply because they speak similar language..same ukija Msoma..Mkurya ataambiwa..wewe kwanza ni mkenya..and on and on.. Hili lazima tulikubali kama legacy ya mipaka iliyowekwa blindly na mkoloni na kuhalalishwa na nchi zetu baada ya uhuru. Na hawa watu wameingiliana maana ndo wanasaidiana katika shida na raha..Its purely geographical accident.

Pili, lazima tujue kwamba Tanzania yetu sheria nyingi ziko kwenye mashelf wananchi waliowengi hawazijui na viongozi ambao wanapaswa kuzitekeleza wanafumba macho..zinaibuliwa pale kunapokuwa na maslahi ya watu fulani. Kwa hiyo usishangae kuona kuna warwanda, wakenya, waganda..name them..wameishi tanzania wakaoa watanzania..watoto wao wamezaliwa Tanzania..wamekulia tanzania kifupi they have known no other homeland than Tanzania. Na wamefanya yote haya bila kuulizwa na mtu. Sasa inapofika watoto kama hawa waliohangaika kama watanzania, ingawa wazazi wao either hawakuwa raia au hawakuhalalisha uraia wao.. wengine wanataka ku-participate kwenye shughuli pevu kama hizi za kisiasa..ndo sheria zinaibuliwa. Sasa huyu mtu aende wapi? mtu kazaliwa kijijini hata hiyo birth certificate hana! Yes, ni rahisi kusema kwamba watu wahalalishe uraia wao..lakini do you think..hii fursa ni wangapi wanaijua? Na swali langu kubwa..why should we punish a child kwa sababu ya makosa ya wazazi wake? Huyu hata ungemrudisha Uganda kwanza atajulikana kama Mtanzania..na at the end of the day..atakuwa Stateless. Maana hata huko hatakubalika!

Kama alivyouliza FMES..iweje kama baba siyo raia afikie level kubwa ya utumishi katika jamhuri yetu? Jibu wote tunalijua..swala la uraia ni kadi ya maslahi especially siasa. na si Tanzania tuu..its all over Africa.

Mi nadhani issue kama hizi za uraia..ni vema ku-raise legitimate questions, lakini tusiwahukumu watoto ambao wamepigana kama sisi..simply because their parents did this or that. Ni kuwanyima fursa...simply because baba au mama hakufanya kitu fulani..ni kama kumuita mtoto wa nje ya ndoa..illegitimate..its damn unfair..maana mtoto hakuhusika na maelewano ya wazazi wake..sasa kwa nini leo anyimwe haki sawa..simply because alizaliwa kwa baba aliyekimbia mimba? Think about it. NA KUNA SHERIA KAMA HIZI ARCHAIC NYINGI..BADO ZIMO KWENYE VITABU VYETU!

Ndo maana governance inatushinda, maana jiulize..ni lini hawa wanaomuwekea pingamizi walijua kwamba jamaa siyo raia? mbona hawakusema hilo mapema? Ofcourse Chadema wana haki ya kuuliza maswali kama haya..lakini..sisi kama wasomi humu JF..we should go beyond these cheap talk..tupeane ideas namna ya kuli-address hili tatizo maana kuna silent majorities wengi sana kwenye hii dilemma. Yaani baba ni wa kuja lakini mtu kazaliwa Tanzania na ameishi TZ miaka yote..leo amemaliza Chuo kikuu..amepata scholarship ya kwenda PHD nje..ananyimwa passport kwamba siyo raia..it doesnt add up..mtu kama huyo..anakuwa frustrated sana...yuko radhi kutoa rushwa yoyote apate hiyo passport.

My suggestion: Tufanye kama USA with some modifications kiasi..kila mtu ahukumiwe kama yeye! Kama umezaliwa ndani ya mipaka yetu basi wewe ni raia (with few exceptions kama wakimbizi walio chini ya uangalizi wa sheria za kimataifa..etc).... Hii itawasaidia watoto wengi..especially wanaozaliwa vijijini. Otherwise hii ni political witch hunt..ambayo inamuumiza kijana wa watu kwa kosa ambalo hakulifanya. Angalia hata CV yake..kijana ni mpiganaji..leo anaambiwa eti siyo raia..duh!

Masanja,

Mwanawane,

Mneno mingi but Sheria ni msumemo.
 
CCM waliwahi kumchagua Premji kule Kigoma akasimama akashinda uchaguzi mahakama ikatangua kwa kuwa hakuwa raia kwa mujibu wa sheria za nchi kwa hiyo hata huko Biharamulo wanaweza kumsimamisha mtu asiye raia
 
Hivi kwa Mfano mimi naitwa Ndumilakuili Kipepe na katika Documents zangu zote za shule, za kuzaliwa na Hata Passport ina hizo info, sasa naamua kugombea Ubunge naiambia tume ya Uchaguzi jina langu ni Ndumilakuili Pimbi Betina, Je kuna kosa la kisheria kwamba nimetoa taarifa za Uongo? Je ni kosa watu kunihoji imekuaje nikadanganya Majina? Wajuvi wa Sheria tuambie legal implication ya hiyo Scenario.

Asanteni
Kulingana na mfano wako, Ndumilakuili Kipepe ni mtu tofauti na Ndumilakuili Pimbi Betiba. Hivyo utatiwa hatiani kwa kutoa taarifa za uwongo. lakini si kosa watu kukuhoji kwa nini umedanganya majina. In fact wasipokuhoji ndio watakuwa wanafanya kosa
 
Kulingana na mfano wako, Ndumilakuili Kipepe ni mtu tofauti na Ndumilakuili Pimbi Betiba. Hivyo utatiwa hatiani kwa kutoa taarifa za uwongo. lakini si kosa watu kukuhoji kwa nini umedanganya majina. In fact wasipokuhoji ndio watakuwa wanafanya kosa

Sasa cha msingi ni kuangalia document zote kama bwana Mukasa alidanganya majina basi sheria ichukue mkondo wake, anyway sheria huwa inakuwa mbaya inapowahusu baadhi ya watu.
This is animal farm principalkwambat all animals are equal but others are more equal than other
 
Ile kutoka Mukasa kuja Rwegasira ilikuwa ni ishara tosha, lakini mbona Matayo david Msuya alivyobadili kuwa Matayo David Matayo hakukuwa na angalizi ama kwa kuwa yote ni majina ya kitanzania? Mukasa aje na vielelezo vya uraia wake!


Huyu matayo haileti maswali sababu kaondoa tu ubini wa kipare kwa sababu anazojua mwenyewe. Historia yake inafahamika na waliompakata akiwa mdogo wanashuhudia
 
Kulingana na mfano wako, Ndumilakuili Kipepe ni mtu tofauti na Ndumilakuili Pimbi Betiba. Hivyo utatiwa hatiani kwa kutoa taarifa za uwongo. lakini si kosa watu kukuhoji kwa nini umedanganya majina. In fact wasipokuhoji ndio watakuwa wanafanya kosa


Mpitanjia, Mfano wa ndege ya uchumi inatupeleka kule kule kwa ROSTUM, RUSTUM, ROSTAM, Sakary n.k. Hivyo sasa hivi mtu akileta majina tofauti tu tunashtuka!
 
tunasubiri kwa hamu!

POLENI Kwa kusubiria ni kweli pingamizi limetupiliwa mbali sababu msimamzi ameeleza lakini chadema wameamua kukata rufaa tume ya taifa ya uchaguzi na wamedai kuwa wanao ushahidi, mmoja wapo ya ushahidi huo ni mkanda wa video wa maelezo ya mgombea huyo ambayo yanatofautiana na yake aliyojaza katika fomu na yake aliyosema katika kikao cha CCM
 
CCM ni noma. Hilo pingamizi lazima walikatae (kwa kutumia wasimamizi wa uchaguzi). Halafu CHADEMA wakikata rufaa tume ya uchaguzi, nayo itakataa. Wakienda mahakamani hakuna uchaguzi hadi mwakani, wanapitisha mgombea mwingine!

Kule mbeya mtu alitolewa kwa kusign kwa wakili badala ya hakimu. Ni wagombea wangapi wa CCM wengine wako madarakani waliokwisha sainisha fomu zao kwa mawakili? Wapo wengi. Ila uamuzi ilikuwa wa mara moja usio na mjadala. Sasa hili wako tayari kusiwe na uchaguzi B'muro. They will do it!
 
POLENI Kwa kusubiria ni kweli pingamizi limetupiliwa mbali sababu msimamzi ameeleza lakini chadema wameamua kukata rufaa tume ya taifa ya uchaguzi na wamedai kuwa wanao ushahidi, mmoja wapo ya ushahidi huo ni mkanda wa video wa maelezo ya mgombea huyo ambayo yanatofautiana na yake aliyojaza katika fomu na yake aliyosema katika kikao cha CCM

Kwa nini hawaendi mahakamani moja kwa moja?
Kabla msimamizi wa uchaguzi hajatupilia mbali malalamiko yao ni lazima amewasiliana na tume, kwa hiyo CHADEMA wasitegemee muujiza toka tume. Kama wako serious waende mahakamani moja kwa moja.
 
Msemo wa "Sheria ni msumeno" nadhani kwa sasa ufutwe na uwe "sheria ni kisu" kinachokata upande mmoja aupendao mkataji.
 
Dah dogo wajanja ndo washakuharibi, kwa kifupi kitumbia kishaingia mchanga, no deal tena, rudi Ifakara health uendeleze fani yako ya IT
 
Nikisema Uwiano ni Mkenya, huna jukumu kuthibisha we si Mkenya. Mzigo wa kuthibisha tuhuma ni wa mtuhumu.
Lakini kwa Immigration mambo huwa tofauti. Ukiambiwa wewe si raia basi unatakiwa uondoke, otherwise uthibitishe kwamba wewe ni raia wa Tz. Na ndio maana Immigration wakikuambia uondoke Tz, huwa hawasemi ni nchi gani uende, kwa maana wanachukulia kwamba hilo si jukumu lao, ila sasa ni jukumu lako wewe mtuhumiwa kuthibitisha kwamba wewe ni Mtanzania so unatakiwa kuwapo Tanzania kama raia. Umeshawahi kusikia Immigration wanamtajia mtu nchi yake? No, ila wanakupa tu masaa machache unayoweza kuwepo Tz.
 
Binafsi nilijua Chadema hawafiki mbali - kwani Jaji Lewis Makame akale wapi ? mzee wa watu na umri ndio huo tena. Kisheria Oscar Mukasa hawezi kuwa Oscar Rwegasira - labda akale kiapo mahakamani. Kuna ushahidi wa tangu awali kuwa Oscar Mukasa ndiye alijitokeza kuwania ubunge kwa tiketi ya CCM. Hili jina ndilo lililowasilishwa CC na ndio maana wadakuzi wakatutangazia kuwa aliyeteuliwa ni Oscar Mukasa

Hata hivyo baada ya vuta nikuvute ndani ya kikao cha CC kuhusiana na jina Mukasa, kikao kinachojulikana zaidi kwa kuhalalisha ufisadi, jina Rwegasira likawa "invented". Shughuli kubwa iliyofanyika baada ya hapo ni kulihalalisha hili jina na kikao kilimalizika tu baada ya kuhakikisha kuwa mamlaka zote husika zimehamasishwa. Ndio maana tunasikia habari za CCM chama makini, hakiwezi kufanya kosa kama hilo.
search_redirect.php

s891520514_6312.jpg
search_redirect.php

Oscar Mukasa - Rwegasira katoka wapi ?

CCM wameweza kumhalalisha Abdulrasul Chakaar
watashindwaje Oscar Rwegasira ?
 
..nimezungumza na jamaa wanaomfahamu mgombea wa CCM. wanadai siku zote amekuwa akijulikana kama Oscar Mukasa.

..labda ana matatizo ya uraia kama wengi wanavyohisi hapa.

..uwezekano mwingine alirudia shule[darasa la saba] na kulazimika kubadilisha jina.
 
Bofya HAPA kunogesha mjadala. Jamaa wanaua noma kwa kutoweka jina la baba ya mgombea, vinginevyo yangekuwa manne na kuongeza maswali. Nadhani la Mukasa wameliweka katikati ili lionekane ni la baba yake, na si la ukoo.
 
Back
Top Bottom