BIKO inapiga goli la mkono, ni mchezo wa kamari na utapeli tupu

Ukiangalia kwenye ile mashine yao inavozungusha namba utaona namba inaanza moja moja had kutimia namba kumi zote

Kwa mfano inaanza
0 zen inafata 6 or 7 halafu znaendelea namba nyingine hadi zinatimia zote

Swali la kujiuliza ni je hizo bahat nasibu zinachezwa na watanzania wote? Kama sio kwanini mchakato wa namba huanza moja moja?

Kama ishu n program swali linakuja mbona hiyo droo huzungushwa kwa sekunde chache had kupelekea mshindi apatikane?

Conclusion...
Kwakua huu mchezo ni bahati nasibu basi endeleeni kucheza one day yes mtakuja kuwa nasibu kamili
 
Changa la macho ukifuatilia ni kama wanaofanya zamu zamu ya mikoa umri fani na jinsia hawana lolote wanasikia watu eti number imezungushwa hata hajatulia kujua ni number gani tayari wameahampigia alie shinda hahahaha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuh mm nimewahi kushinda laki moja toka biko 5000 *3
10000*2
20000*1
100000*1

Na nikishinda tu wa nanitumia ndani ya dk na Nina wiki 2 toka nianze kucheza


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi hawajanishawishi hata kidogo yani. Ni heri football betting everybody has an equal chance to win provided ubashiri ni sahihi.
Umenikumbusha kitambo sana hiyo ya viringi mkuu
 
Inwezekana uyasemayo. Ila mimi jana nimeshibda elfu 20 ingawa lengo langu siyo elfu 20 bali hiyo milioni 50.
Hilo la simu za washindi kupatikana hamna hata moja inayopigwa kisha isipatikane nami napata mashaka...

Sent using Jamii Forums mobile app
Biko hairushwi live ni recorded so suala la hakun anayepigiwa hapokei is not more issue mayb kutokan n sabab za airtime wanabajeti. Ila hiyo , mil 50 kuipata
Utaipata lkn , jasho ltakutoka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Trust me huyu jamaa aliyeshinda Mil 50 nimesoma naye chuo Mbeya ni mshkaji kiufipi pia ni mdogo wa 94 so kanambia hata yy anashangaa kashinda so sidhani kama ni uongo kivile.

Sent using Iphone 7+
Agent at work.....acha kudanganya watu
 
speaking from experience ...
hii michezo musijaribu kabisa kwani madhara yake ni makubwa mno, kwanza huleta umaskini, huchangia umaskini, na pia huweza kupelekea watu kupoteza hata maisha...na nk..

hio biko, au tatu mzuka etc kuna wizi mkubwa mnoo ambao wanao faidika ni wachache mno...

kwa ushauri wangu kama kweli hii inchi ni ya uadilifu na wapo kwa ajili ya maslahi ya umma washuke pale chini kwenye ile board ya bahat nasibu ichunguzwe kitaalamu uone jinsi formula kandamizi zinavyowa dhulumu wananchi kwa maslahi ya wachache...

wafute tu hio michezo, tutafute njia nyingine za kuwekeza...sasa hivi 80% ya wasio na ajira na wale wenye vijimishahara wanateteza fedha zao huko.

serikali adilifu ifanye ya fuatayo.

kwanza wa review software inatumika kwa tatu mzuka..na hizo biko..hapa sitaandika mno kuna mlolongo ambao najua kwa siasa zetu wakifuatilia watazifunga..

wachezeshaji wachunguzwe kwa kila kitu kuanzia mawasiliano yao maisha yao etc...

washindi wale wakuchaguliwa pia wachunguzwe..na kufuatiliwa...

kingine na cha mwisho... kwa wale wadadisi wapenda ku penetrate na kupiga huku ndo kwenye fursa..
 
Kuna mshikaji wangu yupo MTO wa mbu huko Manyara anafanya tour guard ,week mbili zilizopita nilishangaa ametangazwa channel 10 ameshinda mil 30,na akahojiwa ila kama ni utapeli mbona sometimes ukicheza unaweza kujishindia buku 5 au 10 papo kwa papo
Wanachezaje hiyo biko
 
BIKO punda hao nimecheza mara kadhaa sijawahi pata hata mia, ila kuna watu wa karibu walipewa buku 5-5

mara ya mwisho naambiwa bado nafasi moja udake m1 nkasema hawa punda hawanipati tena. wameishia kuntumia meseji kila siku kunihamasisha tu
 
Ni kweli kabisa. Mimi nilimsikia yule mtangazaji/mchezeshaji anasema kwamba mtu akishinda atapigiwa simu lakini asipopokea ile simu ushindi unakwenda kwa mtu mwingine.
Mpaka hapo tu, mchezo unaonekana kama ni wa kihuni kwani mimi sioni sababu yoyote ya msingi eti mtu akishinda ni lazima apigiwe kwanza simu na aipokee ili aweze kupata ushindi wake.
Ebu tujiulize, kwa nini mtu anapocheza mchezo huu hasubiri kupigiwa kwanza simu lakini anaposhinda ndiyo asubiri kwanza apigiwe simu?
Kama namba ya simu ya mtu aliyeshinda inafahamika, ni kwa nini basi akishinda asitumiwe tu kiasi cha fedha alichoshinda pamoja na sms kumjulisha kuwa ameshinda?
Mimi nashauri, huu ni mchezo wenye mizengwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bodi ya michezo ya kubahatisha ipo na huwa wanakagua hizo system
Bahati Ansibu maana yake mshindi anaibuka 1 tu kati ya wote waliocheza hata muwe 1000
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…