Bila huruma ya Algeria Taifa Stars isingefuzu, tuipongeze Algeria sio Taifa Stars

MKWEAMINAZI

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2023
Posts
930
Reaction score
1,304

Hakika Watanzania hawana shukrani kabisa, badala ya kuimiminia pongezi za dhati nchi ya Algeria kwa kutubeba katika mchezo wa jana bila aibu tunaipongeza Taifa Stars kwa kufuzu baada ya kutoka sare na timu ngumu iliyoamua kutoifunga Taifa Stars, kwani ilikuwa na uwezo kwa kuifunga Taifa Stars hata magoli 10.

Binafsi naipongeza sana Algeria kwa moyo wa huruma wa kutubeba.
 
Nidhamu, juhudi, nguvu, umoja, uthubutu, na mshikamano, maamuzi sahihi yenye busara ndani yake, ndivyo ilifanya timu ya Tanzania Taifa stars, kufanya vyema dhidi ya mchezo wa Jana na Algeria.

pongezi kubwa kwa nchini yangu ya Tanzania. Kwa pamoja hatushindwi jambo.
 
Unatesea ukiwa wapi we kolo,ahaaaaa
 
Siku hizi upangaji wa matokeo unapingwa sana kwa hiyo mechi za upangaji matokeo zinachezwa kwa mbinu kali sana na inabidi uwe na jicho la ziada kuziona. Ukitaka kujifunza upangaji wa matokeo wa siku hizi ulivyo angalia mechi za Yanga vs Singida au hata Yanga vs Azam hata za msimu ulioisha tu.
 
hilo liko wazi,kocha wa taifa star ni m algeria,wamembeba ndugu yao,kibarua kisiote nyasi..
 
Naendelea kutofaitisha ushabiki halisi na uhuni. Huu hapa ni uhuni mchundo. Jana Taifa stars imeshambuliwa zaidi ya mara 10 na Algeria na mashambulizi manne Kati ya hayo yalikuwa ya hatari. Lakini anajitokeza Mbumbumbu mmoja anasema Algeria hawakuwa serious.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…