Bila Tsh. Milioni 4.5 haurekodi ngoma kwa Producer S2Kizzy a.k.a Zombie

Kuna msanii anadai kashamlipa hela ya nyimbo 10 .Milioni arobaini na tano.Nikasema tu hiiii.
 
Kwanza hagongi beat kali kumshinda Franken na Duke

Hata kumfikia Owe bado

Wakina Uno wanakunyongea beat nzito unaweza kudhani kama ndio proffesional yao kumbe ni rappers tu
Ila sisi waswahili ni hatari sana.halafu kesho muanze kumcheka??heshimuni watu kutokana na ubora wa kazi wanazofanya na walipwe stahili zao kabisa.Kama nafikiri muziki wake una thamani hiyo na akaidai mlipe au nenda kwa kina Uno.
huu mtazamo umefanya mpaka leo kina Marlon wanaunga unga tu maisha ,hayafanani na ujuzi na hela walizowaingizia watu kwa kazi zao za ubunifu.
S2kizzy ni miongoni mwa wazalishaji wakali sana hapa Africa,mnataka fanyeni nae,hamtaki nendeni kwa mnaowezana bei.ila msivunjane moyo namna hii,sio afya kwa muziki wetu
 
Wao ndiyo wajitahidi waohitaji masoko, the end is what justifies the means.
Kabisa.Eti vitu "conscious" 🀣 .Muziki ni biashara na kila biashara ina soko lake.Sasa kama hao aliowataja bwana mkubwa hapo wanafanya tu "conscious" na majority wanao stream na kukomba hizi nyimbo ni watu wa kidimbwi na watoto wa kike anategemea hao prodyuzaz watajulikana kama kina S2kizzy ambao wanafanya kila kitu??
hii ni biashara,na BIASHARA HAITAKI HISIA!
 
Huyu Ammywave nae ni shida nyingine mjini, jamaa ana kazi nzuri ila sijui kwanini amepoa sana.

Sikiliza ile beat kwenye nyimbo ya CountryWizy - YOU.

Usipokuwa makini unaweza hisi ni goma la ulaya huko[emoji1].
Kwa ground hii Industry ni ngumu mkuu,
 
Basi msanii aimbe akapela
 
Ifike mahali kazi ya uproducer iheshimiwe

Inasikitisha unaskia ngoma kali sn afu kumbe producer alietengeneza alilipwa laki 5

Na msanii nyimbo hiyo hiyo anaipigia show moja kwa dola 10,000
 
Huyo ndo alie imba ile nyimbo ya buga basi ni bora aseme kumbe ndo alijitengenezea ile beat
 
Mnaolalamika mil 4.5 pesa nyingi naona mnaongea kimihemko sana, muziki una hela wakuu.

Wasanii wanatemgeneza pesa nyingi sana

Haiingii akilini audio na mixing ya wimbo ukatengeneze kwa laki 5 kwa s2kizzy afu video ukatengeneze kwa mil 10-15 kwa hanscana au kenny.

Huu ni unyonyaji kwa producer anaeiumizia kichwa nyimbo nzima from the scratch[emoji3525]
 
Ni haki yake

Bongo bado tuna safari ndefu,nilisomaga kitabu Kimoja alichoandika 50 cent ndo nikajua mziki marekani una pesa yani producer kulipwa 50m kwa ngoma ni kawaida sana

Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
Maproducer kibongo bongo wanadharaulika sn, ila ndo wameupaisha sana muziki wetu. Yafaa walipwe vizur
 
Mtoto anavimba sana huyu
 
Kimsingi hakuna kina Hanscana kama hakuna kina S2kizzy
 
Bei ya audio automatically haiwezi kuendana na video achilia mbali walau kufika nusu ya gharama zake...
Video inahitaji vitu vingi Sana location, video vixens, nauli, pamba, vibali, na mambo mengine mengi...
Sijasema maprodyusa wa audio walipwe kidogo mi nazani basata wangesimamia namna bora ya kuingia mikataba Kati ya producer na msanii....
Mfano production inaweza kubaki hiyo laki 5 lakini kuwepo na malipo ya ziada kulingana na Ngoma itakavoingiza hela kuanzia platform zinazolipa mfano YouTube, boomplay na kwenye shoo...
Hapa producer angekua anatengeneza pesa ndefu sana
 
Bora twende kwa Murda beatz.... anatengeneza beats kali za kina Quavo huncho na migos, lil yatch, lil baby... πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Hizi hits zote za muda huu zinatoka plutoo. Wacha atambe ndio muda wake nayeye....zombiiiee sikutajii humuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…