Bilionea Gautam Adani ambaye Kafulila anataka kumpa shirika la TANESCO ashitakiwa kwa utapeli huko Marekani

Mpigie Kafulila
 
Kwa wenye akili...hebi tujikumushe

On Friday, October 25, the High Court halted the government's KSh 95.68 billion Adani-KETRACO electricity transmission deal, citing constitutional concerns.

Justice Bahati Mwamuye issued a conservatory order suspending the deal’s implementation pending further legal examination.

The Law Society of Kenya (LSK) challenged the deal, claiming it lacked transparency, public participation, and accountability.

Azimio La Umoja One Kenya Coalition parties also filed a lawsuit to challenge Indian firm Adani Group's leasing of Jomo Kenyatta International Airport (JKIA).
 
Miaka ya nyuma nilimchukulia David Kafulila kama kijana smart sana kichwani! Ila tangu alipohamia CCM, tena baada ya kudhulumiwa ushindi wake wa ubunge! Ndiyo nikagundua kumbe na yeye yupo kwenye lile kundi maarufu la wachumia tumbo.
 

Kama mtu anathubutu kuhonga Marekani, aisee huyo Tanzania anafaa sana CCM, yani ni malaria, Ccm na rushwa ni sawa na ( ke na me )
 
Miaka ya nyuma nilimchukulia David Kafulila kama kijana smart sana kichwani! Ila tangu alipohamia CCM, tena baada ya kudhulumiwa ushindi wake wa ubunge! Ndiyo nikagundua kumbe na yeye yupo kwenye lile kundi maarufu la wachumia tumbo.

Bado ana akili sana maana anafanya vizuri kwenye sera za Ccm, kuleta mtu anayeweza jaribu kuhonga Marekani, tena NY sio mchezo!
 
Wahindi ni no. 1 Kwa kutoa Rushwa Duniani...!

Utasikia "Veve.... Nani lamba Kono tupu....!?"

Hatuhitaji kuumiza Sana kichwa kujua Kwa Nini Kafulila anawapigia Debe hao Wahindi.
 
Machawa walisema anafaa kuwa rais ajaye hapahapa tukasema tusubiri tutaona! Eti msafi alikataa mambo ya escrow, hahahaha! Wabongo tulivyo walafi hivi tukatae mpunga??
Wavivu wa kufikiri tunapenda mihemuko hatuna subira, yaani kujua kama yaliyomo yamo?, tuseme hatufikiri nje ya sanduku tunapenda matokeo makubwa sasa, (Big results now)
 
Utawala wa madalali wa rasilimali za nchi.
 
Red flags everywhere. Lakini bado watu wanampigia chapuo aje apige na hapa kwetu ili wao wapate % zao.

Tanzania inahitaji factory reset. CCM haitokuja kufanya reforms zitakazobadili mifumo ya hovyo inayokiweka madarakani.

Tofauti na majiri zetu hapo Kenya, hapa kwetu mahakama zetu na bunge letu hakuna wanachoweza kufanya kama kiongozi mkuu wa serikali hataki.
 
Wenzetu wako serious sana lakin hapa nyumbani they dont care, madhara huwa yanaonekana baadae sana halaf watakaa kimyankama hawajui kilichotokea
Sio tu they dont care,they dont have exposure to deal with unscrupulous, pathetic conmen.
Huyo gwiji la Kihindi Adani lina wajuzi wa mikataba kibao, ujanja mwingi,uzoefu wa kupambana na nchi za wajuaji,watoaji hongo kubwa kubwa kwa mpangilio.Waje eti wapambane na Bwana Mdogo Kafulila aliyevishwa Ukurugenzi kama kilemba cha ukoko?Nada!!
Huyo Adani sio mgeni ndio mmliki mpya wa TPA Berth no 8,9,10,11 zilizokuwa zinamilikuwa na akina Karamagi.
Bado anataka kujisogeza kwenye umeme wa TANESCO,Reli ya TRC.Bila kumungunya maneno serikali ya Tanzania haina uwezo wa kumdhibiti kigogo huyo wa kihindi,ni bora kiustaarabu kumwambia NO THANK YOU.
 
Hakuna Mradi Kampuni itapewa hapo PPP Kwa Bwana Kafulila bila kumpatia 10% yake

Ukimsikia anavyoongea utasema ni mtu smart sana, kumbe hamna kitu

Na hapo ana mpango mwakani akagombee Ubunge ili apewe Uwaziri wa Nishati kama alivyohaidiwa na watu walio karibu na Bi Mkubwa ili waje wapige zaidi 🙌
 
Tatizo hawa wakiamua wameamua, (wanajizima data), mambo makubwa kama haya yanahitaji mijadala ya wazi kwakutumia wabobezi tulionao
 
Lucas Mwashambwa njoo unyooshe maelezo hapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…