G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,795
- 36,704
Mambo ndiyo kama hivi wadau!
==========
Bilionea wa Kirusi, Igor Sosin amefariki kwenye mapumziko mjini Zanzibar akiwa na mwanae wa kike, Taisia pamoja na mwanamke ambae hajafahamika. Hii ni miaka mitano tangu mtoto wake wa kiume, Egor alipomnyonga mke wake wa pili na waya wa simu mwaka 2015.
Mwanae Egor hakupata kesi kwa kumuua mama yake baada ya kugundulika na ugonjwa ambao haukusemwa wa akili. Alikubali kumuua kwenye hoteli ya Kazan akidai alitaka kulitoa shetani ndani ya mama yake. Baadae aliachiliwa kwenye hospitali ya akili baada ya kufanikiwa kutibiwa ugonjwa huo.
Inasemwa kuwa amemtaliki mke wake wa tatu na chanzo cha kifo bado hakijajulikana. Miezi kadhaa iliyopita, bilionea huyo wa Kirusi alipona Covid19. Polisi mjini Zanzibar wamethibitisha kutokea kwa kifo hicho kwenye hoteli ya Park Hyatt na mwili wake ulipelekwa hospitali ya Mnazi mmoja kujua chanzo cha kifo chake.
RPC wa Mjini Magharib, Awadhi Juma Haji amesema ofisi yake bado haijapokea taarifa kutoka hospitali hivyo hawezi kusema nini hasa kilimuua bilionea huyo. Mwili wake utasafirishwa kwenda nchini kwake kwani taratibu zote zimekamilika.
==========
Bilionea wa Kirusi, Igor Sosin amefariki kwenye mapumziko mjini Zanzibar akiwa na mwanae wa kike, Taisia pamoja na mwanamke ambae hajafahamika. Hii ni miaka mitano tangu mtoto wake wa kiume, Egor alipomnyonga mke wake wa pili na waya wa simu mwaka 2015.
Mwanae Egor hakupata kesi kwa kumuua mama yake baada ya kugundulika na ugonjwa ambao haukusemwa wa akili. Alikubali kumuua kwenye hoteli ya Kazan akidai alitaka kulitoa shetani ndani ya mama yake. Baadae aliachiliwa kwenye hospitali ya akili baada ya kufanikiwa kutibiwa ugonjwa huo.
Inasemwa kuwa amemtaliki mke wake wa tatu na chanzo cha kifo bado hakijajulikana. Miezi kadhaa iliyopita, bilionea huyo wa Kirusi alipona Covid19. Polisi mjini Zanzibar wamethibitisha kutokea kwa kifo hicho kwenye hoteli ya Park Hyatt na mwili wake ulipelekwa hospitali ya Mnazi mmoja kujua chanzo cha kifo chake.
RPC wa Mjini Magharib, Awadhi Juma Haji amesema ofisi yake bado haijapokea taarifa kutoka hospitali hivyo hawezi kusema nini hasa kilimuua bilionea huyo. Mwili wake utasafirishwa kwenda nchini kwake kwani taratibu zote zimekamilika.