Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna kamsemo kanasemeka hivi 90% wanagombania 10% yapesa hapa duniani lakini 10% ndiyo wenye maamuzi ya 90% ya pesa zote hapa duniani.mmmhhhh hela hazina kazi jamani
Imeripotiwa kuwa baada ya mshiriki wa Nigeria kwenye shindano la Big Brother Afrika, Tayo kuzikosa dola laki tatu za Biggie zilizomwendea Idris wa Tanzania Jumapili iliyopita, mshiriki huyo wa Naija amezawadiwa $350,000 sawa na zaidi ya milioni 600 kutoka kwa shabiki wake bilionea.
Bilionea huyo aitwaye Ayiri Emami ameamua kuongeza dola 50,000 juu zaidi ya ile ambayo ilitolewa na Biggie ambayo ni $300,000 kutokana na kuwa shabiki mkubwa wa Tayo.
Staa wa Nigeria Davido ameshare picha ya story hiyo Instagram na kuandika "we do this easy, bar dey".
Inasemekana hii si mara ya kwanza kwa bilionea huyo kumwaga mkwanja mrefu kwa wasanii anaowapenda, aliwahi kufanya hivyo kwenye harusi ya 2Face 2010 ambapo inasemekana alitoa zaidi ya Naira milioni 20 (sawa na zaidi ya Tsh 189,000,000) na kumzawadia Range Rover mpya, na pia alimzawadia msanii mwingine aitwaye Durella gari aina ya Toyota Prado Jeep.
=======================
Chanzo: MillardAyo.com
Hiii si dharau jamani
​Hiyo hela si bora angenunua suruali avae, mkubwa mzima kuvaa diaper hivyo haoni usumbufu.
?Hiyo hela si bora angenunua suruali avae, mkubwa mzima kuvaa diaper hivyo haoni usumbufu.