Bilionea wa Nigeria amzawadia Tayo $350,000 baada ya kushindwa kuzinyakua $300,000 za BBA Hotshot

Bilionea wa Nigeria amzawadia Tayo $350,000 baada ya kushindwa kuzinyakua $300,000 za BBA Hotshot

Sijakuelewa hicho kiwango wametoa wamepeleka wapi? Tulia ueleze vizuri
 
Katika hali ya kustaajabisha na kutokubali kushindwa

billionea mmoja wa nigeria ameamua kumpa doller 350,000 mshindi wa pili

wa big br akiamini ndie alistahili kushinda ....

Pamoja na yooote hayo kama kuna mnigeria humu anasoma mshindi wa big br

anajulikana kama idriss na si shebedo lenu hilo hata apewe doller million

kukosea wakati wa kwenda kurudi twarudi wenyewe na sasa hivi kila bbr tunalamba sisi
 
Hii ilitokea yule Mzimbabwe aliposhinda $300000 aliongezewa $300000 zingine na mfanyabiashara m1
 
akitoa mnaija no problem, akitoa Rugemalira.....
 
Wanaijeria wanaweweseka sana... Hizo kelele zote hazihamishi fact that Idris/Tanzania won. Ukitaka kujua hiki ni kijembe kwetu, hebu jiulize, ni kwanini huyo billionea alitoa huo mkwanja 30 minutes after huyo tayo kushindwa?? hata kama alitaka kutoa kwanini asimngoje arudi kwao Nigeria ndio ampe cheque?? hata hivyo, tunaomba tuoneshwe hiyo cheque ili tuamini kwamba kapewa maana hawa mapapaa ndio zao, kelele mingi lakini hawatoi chochote zaidi ya sound
 
KUMBE NI UONGO JAMANI, HAKUNA BILLIONEA ALIYETOA PESA, COOKED STORIES TU WAJIPOOZE. Tayo mwenyewe ametweet huyo mtu anayetoa pesa ni nani na yuko wapi?? Na inaonekana hajui chochote kuhusu hiyo pesa..
 
Imeripotiwa kuwa baada ya mshiriki wa Nigeria kwenye shindano la Big Brother Afrika, Tayo kuzikosa dola laki tatu za Biggie zilizomwendea Idris wa Tanzania Jumapili iliyopita, mshiriki huyo wa Naija amezawadiwa $350,000 sawa na zaidi ya milioni 600 kutoka kwa shabiki wake bilionea.

Bilionea huyo aitwaye Ayiri Emami ameamua kuongeza dola 50,000 juu zaidi ya ile ambayo ilitolewa na Biggie ambayo ni $300,000 kutokana na kuwa shabiki mkubwa wa Tayo.

Staa wa Nigeria Davido ameshare picha ya story hiyo Instagram na kuandika "we do this easy, bar dey".

Inasemekana hii si mara ya kwanza kwa bilionea huyo kumwaga mkwanja mrefu kwa wasanii anaowapenda, aliwahi kufanya hivyo kwenye harusi ya 2Face 2010 ambapo inasemekana alitoa zaidi ya Naira milioni 20 (sawa na zaidi ya Tsh 189,000,000) na kumzawadia Range Rover mpya, na pia alimzawadia msanii mwingine aitwaye Durella gari aina ya Toyota Prado Jeep.

=======================

Chanzo: MillardAyo.com

Hiii si dharau jamani
 
​Hiyo hela si bora angenunua suruali avae, mkubwa mzima kuvaa diaper hivyo haoni usumbufu.
 
Back
Top Bottom