Bima kwa wote: Tanzania kuweka rekodi Barani Afrika katika Sekta ya Afya

Bima kwa wote: Tanzania kuweka rekodi Barani Afrika katika Sekta ya Afya

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
Baada ya kuwezesha suala la Elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha Sita na Mikopo ya Elimu ya Juu kwa wanaohitaji. Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inakwenda kuweka rekodi nyingine Barani Afrika.

Wananchi watakaotambuliwa kutokuwa na uwezo wataendelea kupatiwa huduma kwa utaratibu utakaowekwa na Serikali kwa kila mtu kuwa na kadi yake ya bima ya afya.

Suala hili la BIMA ya Afya kwa wote ni matokeo ya ushirikishwaji wa wadau wote. Ni mpango bora unaotekelezwa na serikali ya awamu ya sita ikiwa ni sehemu ya ahadi za Mhe. Rais kumuwezesha kila Mwananchi kupata huduma ya Afya.

Wenye uwezo wa kuchangia (Wasio na familia) watachangia TZS 84,000 kwa Mwaka, sawa na TZS 7000 Kwa Mwezi. Huku kaya ya watu 6 pendekezo likiwa ni TZS 340,000 kwa Mwaka. Mpaka sasa mapendekezo haya yanaonekana kuwa ya chini zaidi Barani Afrika.

Kupitia mfumo wa bima ya afya kwa wote, mfumo wa rufaa wa matibabu utatumika, ambapo wananchi watapata matibabu kuanzia ngazi ya zahanati hadi Taifa itakapohitajika bila shida au adha ya aina yoyote.

Rais Samia Suluhu anahakikisha kila mtanzania anapata huduma bora za afya zenye gharama nafuu.
 
Kama NHIF imeshindwa hii itawezekana vipi?Ikimbukwe kwamba mfuko wa NHIF ni kwa waajiriwa wa serikali(matajiri).Kama huu umezorata huo mwingine utaweza?
 
hivi hizi tafiti huwa mnafanyia wapi enyi vilaza chawa?
Kila kitu tz ni no.1 acheni uendawazimu wa kichawa!

Rwanda yenyewe ina hii kitu zaidi ya miaka 8 iliyopita!
 
Kama NHIF imeshindwa hii itawezekana vipi?Ikimbukwe kwamba mfuko wa NHIF ni kwa waajiriwa wa serikali(matajiri).Kama huu umezorata huo mwingine utaweza?
Hii ni bima ya afya kwa wote bila kujari mwajiriwa au jobless ndio maana ata gharama yake ni affodable
 
hivi hizi tafiti huwa mnafanyia wapi enyi vilaza chawa?
Kila kitu tz ni no.1 acheni uendawazimu wa kichawa!

Rwanda yenyewe ina hii kitu zaidi ya miaka 8 iliyopita!
Tanzania ni bei Rahisi zaidi haijawai tokea Rais Samia Suluhu anaendelea kuboresha sekta ya afya ili watanzania wote tupate huduma bora ya afya bila kikwazo
 
kaya yenye watu chini ya sita? na sisi wenye wake zaidi ya mmoja na kaya zetu ni kubwa kubwa?😀😀
Piga mahesabu hapo bro ni rahisi sana haijawai tokea Serikali ya Rais Samia Suluhu imeturahisishia sana katika masuala ya afya
 
Bima kwa watu wote ni kitu kimoja na huduma Bora za afya ni kitu kingine hivyo tusikimbilie kuweka historia ambayo haina uhalisia mbona NHIF imefeli?
Lemngo la Rais Samia Suluhu anahakikisha anapunguza gharama za afya pia kuhakikisha watanzania wote tunapata huduma bora za afya na za uhakika
 
Baada ya kuwezesha suala la Elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha Sita na Mikopo ya Elimu ya Juu kwa wanaohitaji. Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inakwenda kuweka rekodi nyingine Barani Afrika.

Wananchi watakaotambuliwa kutokuwa na uwezo wataendelea kupatiwa huduma kwa utaratibu utakaowekwa na Serikali kwa kila mtu kuwa na kadi yake ya bima ya afya.

Suala hili la BIMA ya Afya kwa wote ni matokeo ya ushirikishwaji wa wadau wote. Ni mpango bora unaotekelezwa na serikali ya awamu ya sita ikiwa ni sehemu ya ahadi za Mhe. Rais kumuwezesha kila Mwananchi kupata huduma ya Afya.

Wenye uwezo wa kuchangia (Wasio na familia) watachangia TZS 84,000 kwa Mwaka, sawa na TZS 7000 Kwa Mwezi. Huku kaya ya watu 6 pendekezo likiwa ni TZS 340,000 kwa Mwaka. Mpaka sasa mapendekezo haya yanaonekana kuwa ya chini zaidi Barani Afrika.

Kupitia mfumo wa bima ya afya kwa wote, mfumo wa rufaa wa matibabu utatumika, ambapo wananchi watapata matibabu kuanzia ngazi ya zahanati hadi Taifa itakapohitajika bila shida au adha ya aina yoyote.

Rais Samia Suluhu anahakikisha kila mtanzania anapata huduma bora za afya zenye gharama nafuu.
Likifanikiwa hili ,Samia atazidi kukumbukwa Sana mwaka 2035 akimaliza muda wake baada ya katiba mpya,afya ya watanzania Ni Jambo muhimu
 
Kama unafuatilia,hii Bima kwa wote lengo wala siyo kwa maslahi ya hao wote.

Ni sawa tu na kanuni mpya za kikokotoo cha pension kwa wastaafu.

Lengo limerudiwa mara nyingi tu na waziri wa Afya ni kuiongezea NHIF wachangiaji ili isife,How?

Pamoja na kuchangia lakini huduma nyingi tu hospital zitakuwa za kujilipia NHIF inapumlia ventilator.

Business as usual.
 
Likifanikiwa hili ,Samia atazidi kukumbukwa Sana mwaka 2035 akimaliza muda wake baada ya katiba mpya,afya ya watanzania Ni Jambo muhimu
Umenena vyema Rais Samia Suluhu atakumbukwa sana hasa na wananchi wa hali za chini wasio na uwezo wa kutoa elfu 30 au 50 kumuona dr
 
Kama unafuatilia,hii Bima kwa wote lengo wala siyo kwa maslahi ya hao wote.

Ni sawa tu na kanuni mpya za kikokotoo cha pension kwa wastaafu.

Lengo limerudiwa mara nyingi tu na waziri wa Afya ni kuiongezea NHIF wachangiaji ili isife,How?

Pamoja na kuchangia lakini huduma nyingi tu hospital zitakuwa za kujilipia.

Business as usual.
Sio kweli bima ya afya kwa wote itacover kila kitu tena habari nzuri zaidi ni kwamba wasio na uwezo kabisa watasaidiwa kupitia mfuko wa TASAF
 
Piga mahesabu hapo bro ni rahisi sana haijawai tokea Serikali ya Rais Samia Suluhu imeturahisishia sana katika masuala ya afya
kwani nimepinga au kuponda hata ulirushie jina la rais?
 
Msidanganyike watanganyika wezangu,hakuna hizo huduma,mpaka leo hii mmeshindwa kuwapa watanzania huduma ya maji safi na salama kwa wakati wote sembuse itakuwa afya!
 
Back
Top Bottom