Binadamu anaweza kuishi bila dini ikiwa anafahamu mwanzo na kusudi la mwisho la kuwepo kwake

Binadamu anaweza kuishi bila dini ikiwa anafahamu mwanzo na kusudi la mwisho la kuwepo kwake

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
16,464
Reaction score
35,629
Hii ni kwa Kiranga na mshamba_hachekwi , naomba maoni yenu 🤔

Dini lengo lake kuu ni kuwaunganisha watu kuwa katika udugu mmoja kwa ufunuo wa chanzo kimoja cha asili, lakini dini imekuwa tofauti imekuwa uwanja wa ubishani nani yupo sahihi?

Lengo la jumla la dini halipo ila lipo lengo la kumfanya binadamu kuwa bidhaa katika mafundisho yao. Anayo kheri binadamu asiye na dini lakini ndani upo upendo wenye utu kuliko binadamu aliye na dini lakini ndani upo upendo wa utengano na dhihaka.Upendo ulio na unyama ndani

Dini zimeruhusu Mungu kufa, kwakua kila dini imeunda Mungu wa kumtumikia mwenye sifa tofauti kabisa, ulimwengu wenye dini zaidi ya Elfu kumi umepoteza maana muhimu ya dini kwa kutojibu swali hili "Kwa nini ninaishi, na ni nini mtazamo wangu kwa ulimwengu usio na kikomo ambao unanizunguka?"

Dini zinaingia sana katika mijadala ya nje na kusahau ndani kwenye msingi halisi, hii huonesha jinsi dini zenyewe zisivyo jitambua katika "Upendo" unao enezwa

Binadamu mwenye hekima huutafuta ustaarabu nje ya dini, ustaarabu upatikanao katika dini huua asili ya binadamu na kumvisha asili bandia. Dini zimewekwa katika kumchachisha binadamu ufahamu wake

"Wale wanao jitambulisha katika ubinadamu wao wana upendo kuliko wale wajitambulishao katika dini zao. Wale wajitambulishao katika dini zao hujihesabia Kweli na haki na wale wajitambulishao katika ubinadamu wao huhesabiwa watu wa ulimwengu potevu"

Tujiulize binafsi, tujiulize tukiwa nafsi huru, tujiulize kabla ya kujazwa maarifa ya nje, tujiulize kwa maarifa ya ndani Je tunafanya jambo sahihi? Matendo yetu yanaendana
sawa na nguvu iliyotutuma ulimwenguni?

Kusudi la maisha halipatikani katika dini,ikiwa tutalitafuta katika dini maisha yatakuwa katili sana juu yetu,ila kusudi linapatika katika "Utambuzi"
 
Hii ni kwa Kiranga na mshamba_hachekwi , naomba maoni yenu 🤔

Dini lengo lake kuu ni kuwaunganisha watu kuwa katika udugu mmoja kwa ufunuo wa chanzo kimoja cha asili, lakini dini imekuwa tofauti imekuwa uwanja wa ubishani nani yupo sahihi?

Lengo la jumla la dini halipo ila lipo lengo la kumfanya binadamu kuwa bidhaa katika mafundisho yao. Anayo kheri binadamu asiye na dini lakini ndani upo upendo wenye utu kuliko binadamu aliye na dini lakini ndani upo upendo wa utengano na dhihaka.Upendo ulio na unyama ndani

Dini zimeruhusu Mungu kufa, kwakua kila dini imeunda Mungu wa kumtumikia mwenye sifa tofauti kabisa, ulimwengu wenye dini zaidi ya Elfu kumi umepoteza maana muhimu ya dini kwa kutojibu swali hili "Kwa nini ninaishi, na ni nini mtazamo wangu kwa ulimwengu usio na kikomo ambao unanizunguka?"

Dini zinaingia sana katika mijadala ya nje na kusahau ndani kwenye msingi halisi, hii huonesha jinsi dini zenyewe zisivyo jitambua katika "Upendo" unao enezwa

Binadamu mwenye hekima huutafuta ustaarabu nje ya dini, ustaarabu upatikanao katika dini huua asili ya binadamu na kumvisha asili bandia. Dini zimewekwa katika kumchachisha binadamu ufahamu wake

"Wale wanao jitambulisha katika ubinadamu wao wana upendo kuliko wale wajitambulishao katika dini zao. Wale wajitambulishao katika dini zao hujihesabia Kweli na haki na wale wajitambulishao katika ubinadamu wao huhesabiwa watu wa ulimwengu potevu"

Tujiulize binafsi, tujiulize tukiwa nafsi huru, tujiulize kabla ya kujazwa maarifa ya nje, tujiulize kwa maarifa ya ndani Je tunafanya jambo sahihi? Matendo yetu yanaendana
sawa na nguvu iliyotutuma ulimwenguni?

Kusudi la maisha halipatikani katika dini,ikiwa tutalitafuta katika dini maisha yatakuwa katili sana juu yetu,ila kusudi linapatika katika "Utambuzi"
Mkuu,

Asante kwa tag.

Umeandika mengi ya kufikirisha na kuchambua kwa matabaka kadhaa ya uchambuzi. Na sitataka kwenda deep sana kwa kuanzia, nitaanzia kwenye tabaka la juu tu.

Nitaanza kwa mfano wa habari ya ukweli iliyonitokea mimi.

Mimi familia yangu ni watu wa kanisani sana kutoka pande zote mbili. Kwa baba na mama ni familia za kichungaji. Watu ambao wamezaliwa kanisani. Kwa hivyo kuna walokole wengi sana.

Kuna siku, mama mmoja mtu mzima wa familia alikuwa anaongea na mimi. Akaniambia "Familia yetu ina walokole wengi, lakini nikiwaangalia naona wengi kama hawana upendo ule wa kweli kabisa. Wanapenda kujionesha utakatifu wao, kusema wengine, lakini pale panapotakiwa kuonesha upendo kabisa unawaona wanafeli mitihani. Lakini wewe Kiranga ni mtu mmoja ambaye sikuoni kabisa kwenye ulokole, wewe ni "Komredi" (hiyo ndiyo euphemism yake ya "atheist), lakini nikikuangalia kwenye mambo ya msingi kabisa ya kuonesha upendo katika familia, kutokubali makundi, kujitoa kwa wenzako, etc, naona umewazidi sana wale walokole wengi sana".

Huyo mama alinifikirisha sana. Kwa sababu siku zote kuna vitu nilikuwa navifanya navichukulia poa tu, kumbe kuna watu wanaangalia, wanarekodi.

Wanaangalia nani anasema sana "nampenda Yesu" halafu tukija kwenye vitendo haoneshi upendo, halafu nani hataki kujinadi kidini, lakini ukimuangalia matendo yake unamuona huyu mtu roho safi sana.

Sasa ulivyoandika mambo ya dini vs utubora usiofuata dini umenikumbusha sana hiki kisa.
 
Hii ni kwa Kiranga na mshamba_hachekwi , naomba maoni yenu 🤔

Dini lengo lake kuu ni kuwaunganisha watu kuwa katika udugu mmoja kwa ufunuo wa chanzo kimoja cha asili, lakini dini imekuwa tofauti imekuwa uwanja wa ubishani nani yupo sahihi?

Lengo la jumla la dini halipo ila lipo lengo la kumfanya binadamu kuwa bidhaa katika mafundisho yao. Anayo kheri binadamu asiye na dini lakini ndani upo upendo wenye utu kuliko binadamu aliye na dini lakini ndani upo upendo wa utengano na dhihaka.Upendo ulio na unyama ndani

Dini zimeruhusu Mungu kufa, kwakua kila dini imeunda Mungu wa kumtumikia mwenye sifa tofauti kabisa, ulimwengu wenye dini zaidi ya Elfu kumi umepoteza maana muhimu ya dini kwa kutojibu swali hili "Kwa nini ninaishi, na ni nini mtazamo wangu kwa ulimwengu usio na kikomo ambao unanizunguka?"

Dini zinaingia sana katika mijadala ya nje na kusahau ndani kwenye msingi halisi, hii huonesha jinsi dini zenyewe zisivyo jitambua katika "Upendo" unao enezwa

Binadamu mwenye hekima huutafuta ustaarabu nje ya dini, ustaarabu upatikanao katika dini huua asili ya binadamu na kumvisha asili bandia. Dini zimewekwa katika kumchachisha binadamu ufahamu wake

"Wale wanao jitambulisha katika ubinadamu wao wana upendo kuliko wale wajitambulishao katika dini zao. Wale wajitambulishao katika dini zao hujihesabia Kweli na haki na wale wajitambulishao katika ubinadamu wao huhesabiwa watu wa ulimwengu potevu"

Tujiulize binafsi, tujiulize tukiwa nafsi huru, tujiulize kabla ya kujazwa maarifa ya nje, tujiulize kwa maarifa ya ndani Je tunafanya jambo sahihi? Matendo yetu yanaendana
sawa na nguvu iliyotutuma ulimwenguni?

Kusudi la maisha halipatikani katika dini,ikiwa tutalitafuta katika dini maisha yatakuwa katili sana juu yetu,ila kusudi linapatika katika "Utambuzi"
Ndio!
 
Mimi ninaishi bila dini tangu 2000, baada ya kugundua kuwa dini ni mitego ya wazungu ili kuteka akili zetu. Nikiamka asubuhi kitu cha kwanza nawaomba mizimu yangu iniombee kwa Mungu wa kweli (hapa duniani ni Mungu wa mchongo) wao ni roho na Mungu ni roho, wanawasiliana. Ila naimba moyoni wimbo huu "usimtendee mtu kitu ambacho hutaki kutendewa" nafuata katiba ya nchi, kama msahafu wangu na maisha yanaendelea. Ukweli utajulikana baada ya roho kutengana na mwili.
 
Kwa mtazamo wangu upo sahihi,

Lakini hamna cha kufanya juu ya hilo.

Mimi najichanganya na watu wa dini kama kawaida, na ninajitahidi nisiwakosoe
Vita ya maneno ya kidini ni zaidi ya Russia na Ukraine, huwa kwa upande wangu nakosoa kwa njia ya kawaida tu
 
Nimetoka kijijini kwa wajomba zangu kwenye msiba na mjomba hakuwa anasali na hajui dini yoyote. Kafa na kuzikwa kimila kwa mara ya kwanza nimeshuhudia mazishi ya aina hiyo.
Maajabu niliyoona
Viongozi wa madhehebu tofauti huko kijijini kutaka kuzimka kwa kufuata dini ambazo marehemu hakujihusisha nazo lkn kaka yake alipinga.
 
Mimi ninaishi bila dini tangu 2000, baada ya kugundua kuwa dini ni mitego ya wazungu ili kuteka akili zetu. Nikiamka asubuhi kitu cha kwanza nawaomba mizimu yangu iniombee kwa Mungu wa kweli (hapa duniani ni Mungu wa mchongo) wao ni roho na Mungu ni roho, wanawasiliana. Ila naimba moyoni wimbo huu "usimtendee mtu kitu ambacho hutaki kutendewa" nafuata katiba ya nchi, kama msahafu wangu na maisha yanaendelea. Ukweli utajulikana baada ya roho kutengana na mwili.
Uliwezaje kutambua hili jambo ? Ulisoma vitabu au ? Nipe darasa mkuu
 
Back
Top Bottom