Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 49,390
- 152,301
Pamoja sana kamanda.Kaongea ukweli mtupu.Nakala ya uzi huu imfikie Salary Slip popote alipo .
Last edited by a moderator:
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pamoja sana kamanda.Kaongea ukweli mtupu.Nakala ya uzi huu imfikie Salary Slip popote alipo .
Kipigo nilichokipata tangu Kikwete aingie madarakani na 'declare' siku ya leo kama sikukuu kwangu, nasherehekea kwa sababu zifuatazo,
- Naachana na rais ambaye hakuwa serious kulingana na umuhimu wa ofisi yake,
- Rais aliyetumia zaidi ya nusu ya uongozi wake akiwa nje akitumia kodi yangu badala ya kuwatumikia wananchi wake,
- Rais asiyethamini taaluma za watu wakiwemo waalimu, wauguzi yeye ni siasa tu,
- Rais asiyejali mihimili mingine,
- Rais aliyetuhumiwa kwa kila dili EPA yumo, Richmond yumo, Merameta yumo, Escrow yumo, what type of a president,
- Hakuipenda nchi nchi yake kwa dhati, tangu aseme pesa zetu siyo za umma niliumia sana,
- Maliasili zinahamishwa yeye hakujali,
- Rais aliyekuza udini na ukanda "rais hawezi toka kaskazini" hakuonekana kukemea,
- Rais aliyetuambia anayo majina ya wauza unga hadi leo anaondoka nayo,
- Rais anayesamehe wezi wakubwa wa EPA wakati wadogo wakiozea jela,
- Rais aliyependa vijembe kwa wananchi wanaotofautiana naye,
- Rais aliyetumia ofisi kwa maslahi yake na familia yake.
Nikuyakumbuka haya na mengine mengi hakika leo nasherehekea kuondoka kwake na wala siyo kuapishwa kwa Magufuli.
Mungu yehova asante kutuondolea mtu huyu...twakuomba kama huyu aliyeapishwa leo kama ni aina yake please, LORD MAY YOU STRIKE HIM SOON BEFORE WE GET A MILE WITH HIM!! IN JESUS' NAME AND MUTUME MUHAMED WATUME WAFUASI WAKO ALSHABAAB NA BOKO HARAM, ISIL NA INTARAHAMWE, FDLR WAMMALIZIE MBALI..HATA JOSEFU KONNY POPOTE ULIPO TUSAIDIE...THANK YOU
Quinine, nimependa mtazamo wako!Siwezi kusherehekea kuingia kwa Magufuli kwa vile sijui anapotupeleka, 2005 nilifanya kosa la kusherehekea kuingia kwa Kikwete kitu ambacho leo nakijutia.
Kikwete is not going no where. He will be behind the scenes making decisions for JM. He will still have the same power...hii imejionyesha wazi kwenye teuzi alizofanya hapa mwisho. It looks like JM anajua already, otherwise ingekuwa kwa kiongozi mwingine it would have been an insult. JK used all the powers to put JM now it is time for JM to return favor.Nikwamba tumeishi miaka10 bila rais. Tuombe Mungu huyunaye asiwe garasa. Vinginevyo tutapiga 20 bila raisi.
Hata mimi hicho kilinishangaza kidogo! Kwani Rais Magufuli hawezi kubatilisha utehuzi huo? Mashirika ya UMMA ya umuhimu wa pekee kama TTCL alipaswi kufanyiwa mchezo, mimi kwa mfano sipati picha kwa nini baadhi ya Viongozi Serikalini walikuwa wanaipigia debe Kampuni ya simu ya VietNam wanawapatia projects ambazo zinapaswa kufanywa na TTCL kwani waliwambia TTCL haina uwezo wa kutekeleza projects hizo - wanapiga vita shirika la UMMA sijui kwa maslahi ya akina nani? Mh.Magufuli chunguza sana ujio nchini wa Kampuni hii ya VietNam na ijulikane bayana mkataba wake na Serikali ulihusu nini hasa,sio wanatumia mbinu za kutaka kuidhoofisha TTCL wakishirikiana na viongozi wenye ubinafsi - kuna kitu hakija kaa sawa hapa.
kama mimi nimefurahi huyu jamaa aondoke
Hata mi nimefurahi anavyoondoka.
unafuraha kumshinda john mnyika?
Tafadhali naomba utukumbushe hili tukio la Iringa, wengine hatukupata hii habari kipindi inaripotiwa. Ahsante.Nikikumbuka wale waliopandishwa vyeo baada ya lile tukio la Iringa, huwa nashindwa kabisa kumuelewa huyu mtu.
Sio hiyo tu, baada ya kubakiza siku 2 ofisini kaendelea kuteua maswahiba wake, ni juzi tu kateua m/kiti wa bodi ya wakurugenzi TTCL haya si matumizi mazuri ya ofisi halafu sio busara.
Wee dada unawadhalikisha wanawake wenzako kwa kua na mawazo mgando kila siku,inaonekana kama wanawake wato wapo kama wewe!!!
Kwa anayefikiri JK katoka ikulu anajidanganya,Magufuli pale kawekwa tu kutekeleza maagizo ya kikwete na mkapa ndio maana kaanza kuwarudisha watu wa kikeete.
Na ukistaajabu ya mussa utaona ya firauni...Utabaki umeduwaa utakapo sikia waziri mkuu ni Andrew Chenge!!
mafuriko yameelekezwa baharini!
Upinzani umefanya makosa mengi ya msingi na wengi wameshaandika haya - kuna kupokea makapi, kuna kuweka mayai yote kapu moja (kuachiana), kuna kushindwa kutangaza sera hata siku ya ufunguzi wa kampeni, kuna kudhulumiana ndani ya ushirika, kuna kutowafikia wananchi wengi vijijini kwa kupenda starehe na misifa ya helikopta, kuna kutokujibu tuhuma nzito dhidi ya afya ya mgombea wao, kuna kutojibu tuhuma kuhusu chama kikuu ndani ya Ukawa kununuliwa, kuna kudharau mpinzani wao mkuu kana kwamba kazeeka au kachoka sana, kuna kudharau umuhimu wa watumbuizaji katika jamii ya kiafrika na kuwaita fiesta, n.k. Makosa ni mengi mno. Ila hii ilitokana na nini? UNYUMBU!
Nyumbu inasadikika ndiye mnyama mwenye IQ (ufahamu) mdogo kuliko wanyama wengi mbugani. Ni mnyama ambaye mwindaji hasumbui akili yake sana japo nyumbu ana maguvu na mapembe makali! Kichwani hamna kitu! Nyumbu hujihami kwa kuotea! Huota kuwa simba au mwindaji mwingine yeyote akija atamla jirani yake na si yeye! Kwa hiyo aendapo nyumbu mwenzie na yeye huenda! Nyumbu mwenzie akipiga kona na yeye hupiga kona! Nyumbu mwenzie akisimama na yeye husimama! Nyumbu mwenzie akiruka na yeyehakawii!
Ndio maana katika lile ajabu mojawapo la dunia litokealo mtoMara kule Serengeti mamba hujilia nyumbu hadi wanakinai! Akitokea nyumbu mmoja akaruka mtoni au akamsukuma mwenzie basi nyumbu wote watarukia mtoni au watasukumana hadi wadumbukie mtoni.
Tabia hii ya nyumbu tumeiona katika kampeni za Ukawa! Wenyewe kwa vinywa vyao tumewasikia wakijinadi ALIPO NA SISI TUPO! Yaani hata akitumbukia mtoni na wao watajiloweka humo! Hata pale ilipokuwa dhahiri kipenzi chao ni mgonjwa taabani tumewasikia wakisema TUTAMPA KURA HUYOHUYO HATA KWA MACHELA TUTAMPELEKA IKULU! Ni unyumbu ulikuwa upo kazini! Ndioo! Nyumbu hawanamuda wa kufikiri hata kidogo! Husukumana na huigana matendo!
Ni katika unyumbu huu watu walishindwa kufanya tafakuri yakina! Hata pale nyumbu mkuu aliposema atawaachia watu waliohukumiwa na mahakama ya juu kabisa nchini kwa makosa mazito kabisa bado nyumbu wadogo walirukaruka kushangilia!Si nyumbu? Hata pale wawindaji walipotuhumu kuwa nyumbu mkubwa nimgonjwa badala ya kuweka mkakati wa kuwaaminisha wapigakura kuwa nyumbu mkuu yuko ngangari wao ndio kwanza wanasema TUNATAKA HUYO HUYO MGONJWA!
Tabia hii ya unyumbu imesababisha anguko kuu nililolitabiri liwe kweli! Hili ni anguko kuu kwa kuwa hakika mwaka 2020 watu watasita kugeuka nyumbu! Bahati mbaya sana barani Afrika ili upinzani uweze kushika dola unyumbu unahitajika.
Kwa kawaida huwa anatokea almaarufu (celebrity) ambaye anatengeneza manyumbu wengi! Huyu Almaarufu akijua kucheza politics of wildbeasts anawashangaza watawala. Akishindwa huwa anatoweka kama alivyochomoza! Ni kwa kuwa kwa bahati mbaya zaidi unyumbu haujirudii! Ukipita umepita.
Kati ya watu walioumia kuondoka kwa Kikwete ni pamoja na wewe, siku zote ulionekana kama zezeta kwa jinsi ulivyokuwa unamtetea.Sema roho zinawauma tu.
Mlijaribu kila hila kwa miaka 10, zote kapangua huku anacheka.
Kipigo nilichokipata tangu Kikwete aingie madarakani na 'declare' siku ya leo kama sikukuu kwangu, nasherehekea kwa sababu zifuatazo,
- Naachana na rais ambaye hakuwa serious kulingana na umuhimu wa ofisi yake,
Kipigo nilichokipata tangu Kikwete aingie madarakani na 'declare' siku ya leo kama sikukuu kwangu, nasherehekea kwa sababu zifuatazo,
- Rais aliyetumia zaidi ya nusu ya uongozi wake akiwa nje akitumia kodi yangu badala ya kuwatumikia wananchi wake,