Kristo anataka ukifunga ufanye kwa siri
Kafie mbali na kristo wenu?! Unataka na sisi tumfuate kristo ?! Sisi ni waislamu na funga zetu zinafuata misingi mitukufu ya Quran na Sunna za Mtume Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم.
Sisi ni wafuasi watiifu wa mtume Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم.
Na kwetu sisi funga zimegawanyika sehemu mbili.
Kuna funga za FARADHI ( funga za lazima ) ambazo ni kama vile funga ya mwezi mtukufu wa Ramadhani .
Hii ni funga ya lazima kwa kila muislamu isipokuwa watoto, wendawazimu, wagonjwa , wazee walioisha nguvu na wasafiri.
Halafu kuna funga za sunna ( funga za khiyari anayetaka anafunga asiyetaka halazimishwi ) .
Funga hizi zipo mwaka mzima na waislamu wanafunga swaumu hizo kila mmoja kwa nafasi yake na nguvu ya Imani yake.
Waislamu huwa wanafunga funga hizi huku wakiendelea na shughuli zao za kila siku na wagalatia huwa hamjui kuwa wahusika wamefunga kwa sababu hizo ni funga za khiyari hivyo huwa hakuna haja ya wao kujulikana kuwa wamefunga.
Mfano wa funga hizi ni kama vile :
A. Funga ya siku sita baada ya kumaliza mwezi wa ramadhani.
B . Funga ya kila jumatatu na kila alkhamisi.
C. Funga ya siku tati kila mwezi .
Hii huitwa funga ya masiku mweupe ambayo ni kila tarehe 13, 14,na 15 tarehe ya mwezi mwandamo siyo miezi hii ya kirumi.
D. Kuna funga ya siku ya arafa ( tarehe 9 ya mwezi wa 12 wa kiislamu unaojulikana kama Dhul hijja au mfungo TATU.
E. Funga ya siku ya Ashura ambayo ni tarehe 10 ya mwezi wa kwanza wa kiislamu unaojulikana kama Muharramu au mfungo nne.
Kwahiyo waislamu tunafunga mwaka mzima kwa tarehe tafautitafauti na masiku tafautitafauti lakini hatutangazi kwakuwa hizo ni funga za khiyari kwa kila anayetafuta thawabu kwa mwenyezimungu.
Funga hizi anayefunga anapata thawabu na asiyefunga hapati dhambi tafauti na mwezi wa Ramadhani ambao anayefunga anapata thawabu na asiyefunga bila udhuru wa kisheria anapata dhambi.
Kulingana na maelezo yenu KWARESMA KWENU SIYO FUNGA YA LAZIMA KWA WAKRISTO WOTE.
Anayetaka anafunga KWARESMA na asiyaka hafungi na hakuna wa kumuuliza kwanini hafungi.
Sasa msitake kufananisha Ramadhani na kwaresma.
Mwezi wa Ramadhani ni lazima kwa waislamu wote wasiokuwa na dharura za kisheria kufunga siku 30 au 29 kama Allaah alovyoamrisha kufunga pale aliposema katika Suuratul Baqara Aya ya 183 ya kwamba :
"{ يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡكُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ }
"Enyi mlio amini! Mmeandikiwa Saumu, ( mumefaradhishiwa kufunga )
kama waliyo andikiwa (walivyofaradhishiwa ) walio kuwa kabla yenu ili mpate kumchamungu.
Na katika Aya ya 185 Allaah akasema:
" { شَهۡرُ رَمَضَانَ ٱلَّذِيٓ أُنزِلَ فِيهِ ٱلۡقُرۡءَانُ هُدٗى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَٰتٖ مِّنَ ٱلۡهُدَىٰ وَٱلۡفُرۡقَانِۚ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ ٱلشَّهۡرَ فَلۡيَصُمۡهُۖ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٖ فَعِدَّةٞ مِّنۡ أَيَّامٍ أُخَرَۗ يُرِيدُ ٱللَّهُ بِكُمُ ٱلۡيُسۡرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ ٱلۡعُسۡرَ وَلِتُكۡمِلُواْ ٱلۡعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُواْ ٱللَّهَ عَلَىٰ مَا هَدَىٰكُمۡ وَلَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ }
Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo (ndani yake ) Qur'ani kuwa ni uwongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi. Basi ataye kuwa mjini katika mwezi huu naafunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika siku nyengine. Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa kuwa amekuongoeni ili mpate kushukuru.