Wewe kiboko
Kasie utakuwa mtamu sana machoni .Hahahahahahaa polee
Nafasi yako ilikuwa ndani ya basi ucheze karata zote ili binti asishuke Iringa uende nae hadi Dar angekuwa keshamuacha jamaa yake. Hehehehee polee.
Nakumbuka nilipokuwa kigori **** mkaka alishuka kwenye daladala kituo sio chake na alinisindikiza hadi nyumbani hehehe. Kote huko sijamjibu hata kimoja alichokuwa ananiongelesha. Nilipokaribia nyumbani nikamwambia skiza nipe namba ya simu ya kazini kwako na anuani ili mimi nikutafute maana enzi hizo geti kali na sikutaka apajue nyumbani. Nikimuacha anisindikize kutoka kituo cha daladala hadi karibu na nyumbani maana kigiza cha saa kumi na mbili jioni kilikuwa kimetanda hivo nilikuwa na woga wa kutembea mwenyewe.
Hahahaha nilikuwa nashangaa wanaume unaanzaje kumfatilia mschana hata humjui tena alinilipia nauli, simjibu chochote aniongeleshacho mie natembea tuu hahahah
Kwenye daladala sasa akishakulipua nauli utaona konda anauliza sheli. ... kimya.... kwa mpemba.... kimya... jamaa anasubiria binti aseme shusha ili naye ashuke.
Siku ingune nilikutana na jamaa wa hivi na nilimuuza maana nilikuwa natoka kawe naenda posta, baada ya kunilipia nauli nikasema leo atakoma maana ukimuangalia usoni anakutazama kwa macho ya kukutongoza tuu.
Kufika mbuyuni konda kuuliza mbuyuni nikasema shusha, yeye akatangulia kusimama na kushuka mie nikajichelewesha nilisimama kisha nilipoona kushuka nikainama na kurudi kukaa. Konda kuuliza mwingine kimyaa.... akaruhusu gari iondoke heheheheh nilichungulia nje jamaa macho yanamtoka maana mda ule kupata usafiri wa posta maeneo yale ni shida.
Poleni ila nilifanya yale kwakuwa ilikuwa utoto tuu hahahaha kweli wanaume mmeumbiwa mateso.
Wakati nasoma sekondari kuna mvulana flani alishanisindikiza toka tumeshuka kwwnye daladala hadi eneo la tuition wakati huo na yeye anasoma tuition ila kwingine. Siku hiyo alinisubiri hadi mie nimetoka tuition na tunarudi tumepanda daladala moja. Akanilipia nauli, sikutaka apajue nyumbani hivyo niliposhuka mwisho wa kituo nikamwambia nipe address ya shule unayosoma na jina tuandikiane barua si unajua home kuna mbwa wakali? Akanielewa ndo nikamtoa kihivyo daah.
Yaani mleta mada nimekuelewa sanaa. Pole kwa yaliyokusibu sio pekeyako ni wanaume wengi tuu huwakuta haya.
Yaani hujatengeneza mchongo ukiwa kwa basi haf ume dro ndo unaaza kunyatia. pole aiseWakuu nimeamini mapenzi yana nguvu kiasi kwamba waweza fanya mambo mengine kwa msukumo usiokua na tija. Juzi hapa nimekuwa nikisafiri kutoka mkoani kwenda Dar, but ndani ya bus kulikua na mrembo machachari mno kiasi kwamba nikajipa moyo kama atafanikiwa kushukia ninaposhukia basi siwezi mlazia damu.
Bahati mbaya akawa ameshuka Iringa, nami mtu mzima nikajitosa nika drop kwa vile nilimuelewa sana. Bus likaondoka, ile najiandaa kumsemesha mara ghafla akaja jamaa kajaa jaa hivi, yaonesha ni jamaa yake maana kwa zile hugs nikajua hapa sina changu, then wakatokomea kusikojulikana.
Basi mtu mzima nikaanza kuhaha pesa ya rum na usafiri wakunifikisha safari yangu ukizingatia nilikua nina interview ya kikazi.
Wanawake bwana, sijui mlinyunyuziwa sumaku ya aina gani!
Kasie utakuwa mtamu sana machoni .
I wish uje pm unizingue kama hizo "crush" zako[emoji3]
Mambo kasie?Hehehehee nilifanya vibaya ila ilikuwa uschana saa hizi siwezi kufanya hivo hahahah
Nimesoma comments mpaka page hii ya 5. Nimecheka mno. Ndivyo tulivyo
Kwenye simu yangu hafifu inasomeka tano [emoji54]Mmmh kweli umecheka ssna hadi 3 kwako imekuwa 5 hehehhee hongera kwa kufurahi na kuongeza maisha.
Mambo kasie?
Kumbe roho mbaya ulikuwa nayo kitambo tu na siyo kwa binamu yako.
Hahahahah!Mambo poa,
Hahahah hujanielewa tuu Kasie hana roho mbaya yuko peace tuu sema nj mkali akiona mizengwe na ndivyo sivyo.
Binamu kwakweli alinikosea adabu na kama ni roho mbaya kwa binamu acha niwe nayo asee tena akithubutu kurudia namnunia mazima.
Hahahahah!
Siyo vizuri hivyo..kasie
Hapo kidogo freshHaya kama hutaki iwe ivo heheheh.