Kiukweli umeongea point ya maana lakin walio wengi humu Kwa unafki wao hatokosa sababu ya kupinga hoja yako ila kiukweli mitaji ndio inawakwamisha sana vijana katika kufikia malengo
makande yanahitaji mtaji kiasi gani?wabongo kwa visingizio
Wewee, hivi unadhani alichukua tu mahindi na maharage akapika makande wateja wakaja? Yaani napata picha hapa uswahilini kwetu nipike tu makande watu waje kula? Kwanza jina lake tu ni mtaji tosha, umeenda kuangalia hayo makande anayauzia sehemu gani? Anayapikaje? Anayapack vipi?makande yanahitaji mtaji kiasi gani?wabongo kwa visingizio
Kwani kuna nini huko marekani watu wasirudi kuuza kande home kwao,ulitaka auze KFC au MacDonald.Yaani kwangu mtu yoyote aliefika kusoma au kuishi marekani au nchi za ulaya,halafu akarudi huku analialia habari za hela huo ni upopoma mkubwa,hata huyo anaeuza kande wakati amesoma marekani/kuishi marekani ni mpumbavu wa hali ya juu,siwatanii
Sent using Jamii Forums mobile app
Unaandika tu kirahisi anauza makande. Kama ambavyo mtu anaweza kuandika kirahisi Bakhresa anauza ice cream au unga wa ngano na tui la nazi.habari wadau...
nimekutana na habari ya nancy lema.. wa mwanza.. nikaona ni share nanyi wadau mtoe maoni.. je binti yupo sahihi au wrong...
kafanya degree yake st marys university of minnesota na masters university of minnesota huko usa..
baada ya kumaliza masomo yake akaamua kurudi nyumbani kujiajiri kwa kuuza makande kisasa...
na kwao ni mambo safi hasa hasa...
nawaza tu why dada zetu maskini hawapendi kujishughulisha huku washua hawachagui kazi...
nimemkumbuka na mercy kitomari nelwa gelato.. nae ana degree ya U.K ila amerudi tz anauza ice cream tu kisasa
Yaani kwangu mtu yoyote aliefika kusoma au kuishi marekani au nchi za ulaya,halafu akarudi huku analialia habari za hela huo ni upopoma mkubwa,hata huyo anaeuza kande wakati amesoma marekani/kuishi marekani ni mpumbavu wa hali ya juu,siwatanii
Sent using Jamii Forums mobile app