Binti wa kishua, mwenye shahada toka Marekani amejiajiri kuuza makande, dada zetu maskini wanachagua kazi

Wewe utakuwa zezeta wa karne na karne. Unaona mafanikio ni kuajiriwa na kukaa nyuma ya keyboard walizonunua vidume sio, au Unaona ujanja ni hicho kijishahara cha 2m sio? Utakufa masikini ww

Kwanza mimi siyo zezeta, pili siwezi kufa masikini nimeshapita huko, haitendei haki taaluma yake kwa hiyo miaka aliyopoteza si ungekaa nyumbani apike makande?yeye mwenyewe kakosa ajira kaamua kuwa mama ntilie wa makande, kwenye hiyo elimu yake ameshindwa kabisa kuja na kitu cha maana?

yule dogo wa NALA karudi nyumbani sasa ivi anavuna mamilioni kwa kuiifanyia haki elimu yake, hiyo ingekua ni chanzo kingine cha mapato hapo sawa, ila kumsifia ni upuuzi mwingine
 
Aisee, wasomi wetu ndio mnawaza haya kweli?
Je, sisi tusiosoma tuwazeje?
 
Unatetea upuuzi, kwa Tanzania nafasi za Project Management ni chache, asingeweza kuajiriwa .

Opportunities kwa watu waliosoma TZ zipo nyingi sana, Project Mgt kwa level ya masters unafungua ofisi na kujiita “Project Management Consultant” au “professional project manager” tafuta connection mbili tatu kisha uza ujuzi wako afu tuone kama utakosa kazi...tukiendelea hivi tutaishia kutukanwa na politicians
 
Kama mungu atatupa uhai, jambo hili nitakumbusha miaka minne ijayo. Mimi na wewe tutajua huyu bint ambae mm namuona ni very bright Atakuwa amefikia wapi?
 
Kama mungu atatupa uhai, jambo hili nitakumbusha miaka minne ijayo. Mimi na wewe tutajua huyu bint ambae mm namuona ni very bright Atakuwa amefikia wapi?

Sijasema kwamba hatafanikiwa na wala simuombei asifanikiwe ninataka sana afanikiwe Mungu ni Mwema, BUT ni upuuzi kumsifia na kuona anafanya maajabu kwa kwa kuuza makande kwa elimu aliyonayo kwamba anafanya kitu extra ordinary out of this world..tunamuongelea mtu mwenye exposure ya international education, countries, cities and lifestyle, kashindwa kung’amua fursa zilizopo katika eneo lake alilo master tunamsifia miaka minne baadae kaamua kuuza makande, really??
 
Kweli mkuu,hata mm nimeshangaa sana,degree USA,masters USA halafu unarudi home kuuza makande?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nilishasema pale juu kazi ambazo nyingi wazungu hawataki kuzifanya na ambazo na wewe hutaki kuzifanya eti zinakushushia hadhi,kazi zilizo nyingi kule ni kupanga mabox tunaita lakini ni kurudishia bidhaa zilizonunuliwa kurudishia zingine kwenye mashelvu. Hiyo ya kuosha mbwa wa wazungu ndio umeona ndio kazi iliyo femas sana ulaya? (Najua unachokifikiria,na unachotamani kuongea,kwamba unaweza kufanya na kazi fulani,akili za kibongo).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila la heri. Mimi sijafundishwa maadili ya kihivo. Tunaamini kuwa bora ufe nyaa kuliko kudhalilishwa. Soma habari za ndg yenu Kreluu ndo utaelewa.
 
Kila la heri. Mimi sijafundishwa maadili ya kihivo. Tunaamini kuwa bora ufe nyaa kuliko kudhalilishwa. Soma habari za ndg yenu Kreluu ndo utaelewa.
Wewe mbona unaongea kitu tofauti kabisa na ninachoongea?. Kudhalilishwa,wapi nimeongea kazi za kudhalilishwa? Uwe unasoma vizuri mada halafu ndio unatoa comment zako,usikimbilie kule unakotaka wewe. Kufanya kazi kwenye mashoprite wapi hiyo kazi inadhalilisha? Kweli akili ni nywele kila mtu ana zake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wewe unaonekana kichwa ngumu kweli rafiki yangu. Mimi hizo kazi za maboksi siwezi fanya hata iwaje. sasa unataka kulazimisha. Hayo mashoprite unayosema mimi siwezi kufanya huu ujinga mbona huelewi braza. Wewe na njaa zako nenda kafanye. Bila shaka umenipapata. Narudia tena sifanyi huo ujinga. Mimi nimekaa nje miaka 8 sijawahi gusa huu upuuzi. Utasema bishoo ni kweli mibishoo ila siwezi kuomba hela ya maji kwa jirani. FULL STOP. Usifikiri kila mtu anawaza kufanya kazi za mabox na ndoo mana unaanza kumdharau dada aliyejiongeza.
 
Nilijua tu naongea na mtu wa aina gani. Kuna mahala nimekulazimisha wewe? Any way tuachie hapo. Humu tunakutana vichwa na akili tofauti. Kila ninachoongea unakigeuza unavyotaka wewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli mkuu,hata mm nimeshangaa sana,degree USA,masters USA halafu unarudi home kuuza makande?

Sent using Jamii Forums mobile app
Uli afungue Saluni ya kike? Au awe analeta Mikoba kutoka Uturuki? make nazani mawazo yenu yako hapo.

Tuna safari ndefu vibaya mno na my be hata baada ya miaka 200 tunaweza tusifunguke akili.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nazani ni kikuambia Nitajie Furusa unazo unaso zijuia ya kwanza itakuwa Mpesa, Duka, Gest, saloon, Au Duka la Hard ware.

Tusha jijengea Mindset kwamba Aina fulani ya biashara aio biashara.

Mbona hamsemi Azam na pesa zote anauza Mandazi?

Ulitaka awe na Idea zile unazo zijua? yaani Idea zako unazo zijuia kama za saluni au kufungua Duka la Kuuza Mikoba au Ngua au Saa ulitaka afabye hizo


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeonaeee mkuu? Ni upuuzi kweli kweli,lakini bado watu wanaona ni kitu cha kukishangilia

Sent using Jamii Forums mobile app
wewe ndo Mpuuzi mkubwa sana, Umekoaa na Exposure mara Shiloprite.

uliraka afabye Zile biashara unazo zipenda?Ulitaka akufurahishe?

Au ulitaka aanzishe Duka la kuuza used Computer kutoka huko aliko kua?

Unasema ni Upuzi mwenzako anapiga pesa na huna namna ya kuweza kumfikia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona umekoaa na akaajiriwe kama wewe? Acha ujinga Dogo. Sio kila mtu ana waza kama wewe na usitake Yeye awaze vile unavyo waza wewe.

Wewe waza unavyo waza na yeye kawaza anavyo waza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila la heri. Mimi sijafundishwa maadili ya kihivo. Tunaamini kuwa bora ufe nyaa kuliko kudhalilishwa. Soma habari za ndg yenu Kreluu ndo utaelewa.
Mkuu tumia akili yako vizuri,hapa duniani hakuna kazi inayodhalilisha ili mradi tu iwe halali,kama ni hvo basi tunaweza kusema kazi unayo ona haidhalilishi mm naweza kuiona ya ovyo na inadhalilisha hvo usiseme kuna kazi zinadhalilisha....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
huyu dada hayo makande yake angeyauzia marekan tungemuelewa kidogo lakin kuwauzia wasukuma mmh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…